Pata majibu ya maswali yanayokuhusu
Nauliza kama aujui kusoma Quruani na unaswali kila kipidi cha swala je kunapungufu apo
27-03-2023 06:15:49
Swallat tahajjud ina rakaa ngapi?
24-03-2023 05:53:27
Assalamu alaikum je mwanamke kadai talaka naakainunua baadae akataka kurewa je rejea ipo nakama ipo kuhusu mahari je
04-03-2023 05:06:01
Je inafaa kuchoma sindano wakati umo kwenye funga?
28-03-2023 11:26:30
Nataman kujua Jins ya kujitwaharish kujua kuswali na kusoma Quan je unanisaidiaj?
29-04-2023 06:49:16
Swali langu Ni hili,,,
"Thibitisha kuwa khalifa Othman alimrejesha mjomba wake kutoka uhamishoni kwa lengo gani?
21-05-2023 06:10:10
Marehemu ameacha mke na mtoto miaka 10, wazazi wote baba na mama yake wamefariki mali ya marehemu itarithishwa nani na kwa mafungu gani
10-02-2023 04:22:35
Mimi ni mwanamke wa miaka 25..Nilikuwa nina kipindi kirefu kama miaka 3..Sijafanya mapenzi..Sasa baada ya kufanya wakati siku naingia Kwenye siku zangu nilipata maumivu makali sana ambayo kabla sikuwa nayo..Lakini pia nimeanza kupata maumivu ya chini ya kitovu na kiuno ambapo inaambatana na gesi wakat mwingine hadi kichwa kinauma na misuli ya miguuni..Naomba unisaidie shida ni nini?
24-04-2023 13:01:04
Madhara ya kufanya mapenzi na mama mjamzito
18-02-2023 12:08:12
Samahn mwalim naomba unisaidie aina Saba za usomaji wa Quran
Taja aina saba za usomaji na mashehe wake na nchi zake kabla ya kuhifadhiwa quran katk msahafu lakwanza ilo
08-02-2023 12:34:23
Mm nauliza sual kwann baada ya mtume Muhammad hakuletwa mtume mwengine
30-03-2023 06:33:59
Unawezaje kufunga swaumu na hali yakua una mke hujafunganae ndoa
27-03-2023 05:27:04
asalam aleykum samah naomba kuuliza,endapo nimemkuta imamu anaswalisha ile nimefika tu akarukuu na mimi nikarukuu je nitaesabika niko nae sawa kama ni swala ya adhuhuri.
06-04-2023 12:07:39
Swali langu Tofautisha maadili kwa mtazamo wa uislamu na kitwaghuti
18-02-2023 16:17:43
Nataka kujua nini mtazamo wa kikafiri juu ya dini
15-03-2023 08:49:04
lengo la qur-an ni lipi?
02-04-2023 04:26:47
Jana alikuja alielua mume wangu akawaambia watu kua nimemuacha s mke wangu je nataka kujua ikiwa ni lazima akicha kue na mshahid wa kweli je hapo talaka imepita na kama imepita anafaa kunipa karatas au haifai
28-02-2023 05:57:10
Habari, samahani, naomba kuuliza ukisha tamka shahada ndo tayari kusilimu ama kuna utaratibu mwingine?
21-05-2023 13:27:54
Asante na kama ukipata haja kabwa au ndogo na ukastanji ni lazima kuchukua udhu tena ?
19-02-2023 17:53:16
Sababu zinazopelekea kutofikia lengo la zakka na sadaka
14-03-2023 05:46:47
Kuna mafunzo ambayo waislamu wanayapata kutokana na historian ya maimamu wa fiqhi
24-02-2023 08:13:39
Je,ni ipi dalili itakayonijulisha kua Leo ni usiku wa lailatu likadri ili niombe hiyo dua?
20-04-2023 05:33:47
Uislamu wakati wa makhalifa ulipata changamoto nyingi sana ambazo zilipelekea kuwatia khofu waislamu wanafikiria mambo gani yaliopelekea kuondosja changamoto izo
25-02-2023 04:23:33
Assalamualaikum warahmat llah wabarakat... Samahan nlikuw naswali ni ipi hukmu ya mwanamke kupaka dawa Kam pambo Kwa mme wake
06-05-2023 06:34:27
Suali langu kwanini mwanamke anatolewa mahari?
26-02-2023 08:39:14
Asalam aleikum warahmatullah wabarakatuhu, mimi nimemuachia mke wangu zakatul fitri aigawe ,bahati mbaya mlengwa katafutwa zaidi ya mara mbili hakupatikana ,kaja kupatikana baada ya swala ya iddy, nini hukumu ya hiyo zaka?
21-04-2023 15:03:14
Naomba unifundishe namna ya kusimamisha sala ya tarawehe na witir
23-03-2023 12:45:03
Asalam alykum nataka kujua inakuwaje hukumu ya mwanamke alotoka nje ya ndoa.na mumewe kamwambia ikitoka nje ya ndoa ndo talaka yako.na akatoka nje ya ndoa.je VP hapo ndoa Bado ipo au ndo talaka tayari ishatoka km mume alivyosema?na je baada ya mwanamke huyo kule
11-03-2023 06:28:37
Kuna Jambo lini ni tatiza ya kutofautisha ibada naعادي kwa mfano kula chakula hii ni ibada Au عادي ?
09-03-2023 12:34:57
Kwanin mwanaume anaoa wanawake zaid ya mmoja Kwan uyo mmoja hamtoshi
24-03-2023 19:21:48
Aesalam alaykum je kur an imeshushwa kwa mudagan
05-05-2023 07:13:24
Asalaam alaykum w wabarakat ustadh je kama umeshiriki tendo la ndoa ktk mwez wa ramadhan kisha ukapitiwa na usingiz mpaka alfajir ikafika ukawa ujajitwaharish je unaweza kuendelea na swaum bi maana swaumu yako itaswihi
25-03-2023 08:21:08
Je km mtu aliishi miaka mingi bila kufunga na anamke wake halali wakati wakiishi walikuwa wanafanya matendo yote ikiwemo kujamiiana kipindi chote cha ramadhan kwa mda wowote iwe Asubuhi au mchana Sasa wameamua waanze kufunga swaum je Hawa watu watahusika na ile hukumu ya kufunga siku 60 mfurulizo? Au kuzilipa zile ramadhan walizo ziacha huko nyuma?
23-03-2023 08:34:42
Assalaam Alaykum,namna yakutoa talaka ya tatu na taratibu zake
29-01-2023 19:21:47
Naomb kuuliza ukiswali witri katika baada ya ishaa vipi unaruhusiwa kuamka usik kwa ajili ya sunna nyingne
05-04-2023 17:24:41
As salaam alaykum warahmatullaahi wabarakaatuh. Tukio la mwanzo la kuvunjwa Al qaaba lilikuaa mwaka gani?
28-02-2023 05:40:54
Assalamualaikum naomba kuhuliza kula kitu ambacho kimechinjwa na mtu anae kunywa pombe ni sawa
22-02-2023 13:32:00
Asalam aleykhum ,he mtu huweza kudumu na udhu kwa swala zote tano kama hatopatwa na moja ya yayotengua udhu ?
19-02-2023 17:50:42
Assalaam a'laykum warahmatullãhi wabarakaatuh! Shaikh nauliza; ivi inawezekana mke kuslimu na kufunga ndoa ya kiislam siku hiyo?hiyo
04-02-2023 14:28:28
Swali saut yangu inakwaruza nina kama miez 2 iv shda n nn?
28-03-2023 11:29:12
Assalamu 'alaikum warahmatullah wabarakatuh. Na swal. Je, inaswihi kwa muislamu kuswali juu ya kaburi kwa lengo la kumuuombea maiti iliyomo ndani ya hilo kaburi
10-02-2023 04:39:32
Kwanin uislam unapinga kampen juu ya kudhibit uzazi
14-03-2023 16:30:09
Assalam aleykum nilikuw nauliza je Kuna dua yyote ya kumsomea mait wakati wakumuosha??
04-03-2023 05:04:48
Naomba kujuwa Masharti 5 ya vazi la kiislam
23-02-2023 05:26:34
Kama mwanamke amepewa talaka ya kwanza,yapili n yatatu.baina talaka ya2 n 3 akawa n ujauzito
02-05-2023 06:33:01
nyenzo anazotumia mwanaadamu kujielimisha ambazo ni dhaifu
30-01-2023 16:11:05
Naomba nielekezwe ikhfau Shafawiya katka hukumu za kusoma Quran
04-03-2023 18:24:23
A.alaykuuu swalii.....kwa mujibuu wa suratul,asri aliefelii na na alifauluu ni nani
28-01-2023 20:03:10
Naitaji mwalimu video lamda Kwa uelewa zaidi juu ya sanda ya mwanamume na mwanamke
25-03-2023 18:30:45
Je damu ya vidudu vidogo vidogo ina toa udhu mfano kama damu ya mbu nk
08-05-2023 07:49:56
Assalam alaykum nauliza eda ya khulu Ni muda gani? Na wanaweza kuregeana?
15-03-2023 16:29:34
Lakaa za swala yaani kwa mfano swala ya asubuhi inalaka ngapi saa Saba inalakaa ngapi saa kumi inalakaa ngapi saa mbilo usk inalakaa ngap
23-03-2023 14:03:43
Nashukuru Swali langu ni kuhusu maana. Ya kijakazi atamzaa bibi yake Katika hadithi ya pili kati ya hadithi arobaini zak imamu annawawiy
21-05-2023 06:04:02
Kifo cha bi khadija kilitokana na nini
24-04-2023 13:49:51
Nauliza mke wa Nabii Nuhu alikuwa anaitwa nani?
17-02-2023 09:42:20
Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji
30-01-2023 15:49:31
Aslm alykum naombakuuliza,Kam mine ana wake 2 ikitokea mwenyezamu hayupo keep mine anahaki ya kulala kwa Yule asiyekua zamu yake
29-01-2023 19:22:59
Je? Unaswaumu halafu umezaa nje mtoto mama kaomba hela unaruhusiwa kuto?
07-04-2023 03:39:07
Asalaaam aleykum ndugu naweza kupata. Maana ya jina la Ulya ndani ya quran tukufu. Sura na ayat
26-02-2023 09:48:26
Je itaondokaje hadathi kubwa kama pakikosekana maji
28-02-2023 03:46:50
Ukitaka kujifanza Quran kwe njia yacm Ina wezekana
26-02-2023 13:16:21
Mimi nina mchumba wangu lakini nimezaa mtoto mmoja sasa tulikuwa tunataka tufunge ndoa kabla ya ramadan lakin ikashindika sasa je inaswihi kufunga ndoa wakati wa ramadhani
29-03-2023 11:46:42
Ninapo fanyia kazi niwa kristu mana nyumba nzima ime zunguukwa na misalaba na biblia je inaswihi kuswali katika nyumba hiyo
05-04-2023 08:48:03
Mimi ni mwanaume na ninamiaka 32 naomba kujua maneno ya kikao cha tahyatu
06-03-2023 11:06:49
Asalam aleykum,, samahan naomb kujua nini nifanye napokumbka marehemu
01-02-2023 12:27:27
je ninapochukua udhu naruhusiwa kuongea?
25-02-2023 19:22:07
Samahani nilikua nauliza sunnah na mpangilio wake sijauelewa
31-01-2023 15:58:37
Faida za kusali Sala za sunna zichambuwe
19-02-2023 14:41:52
Je najisi ya mbwa kukuramba inaenea? Kwa mfano akakulamba ww kwenye mkono halafu wewe ukaja kunisalmia mimi nikakushika sehem ileile alokulamba mbwa
26-03-2023 10:20:10
Nimeona darsa kidogo juu ya suala la talaka.swali langu ni je??..kama umempa talaka moja mkeo bila ya mashahidi waadilifu.je kuna tatizo katika uhalali wake??
04-05-2023 12:25:39
Assalamualaikum napenda kuhuliza kwenda kwa mganga kuchukua dawa ambayo sio ya kumzulu mtu niya matibabu tu je ni sawa
26-03-2023 10:30:08
swali mim nahitaji kujua herf zakuruani
31-01-2023 06:04:05
Samahn,,ati ni mwaka wa ngapi ilifaradishwa funga?
23-03-2023 10:44:50
Assalaam alaykum...mimi nauliza endapo mmeshazaa mtoto na we mwanamke ukadai talaka je mwanaume ana haki ya kudai mahari yake ingawa umeshazaa nae?
09-03-2023 13:20:51
Kwan mbon wanasema kusom dua kabr yakumuswalia Mtume nakabr yakutoa slm nidua gan nakuomb nisayidie
10-02-2023 08:22:59
Neno kusai lina maana gani katika hijja?
29-03-2023 05:31:53
Je naruhusiwa kuchinja nikiwa nimefunga ramadhani?
15-04-2023 04:22:37
NAOMBA USINAIDIE MASHAGANZI ZAKE NA MTUME S,aw WALIKUWA WANGAPI NA MAJINA YAO WALIITWAJE??
25-03-2023 11:17:07
Mm naomba ufafanuzi ikiwa mume alikaa sehemu nakusema maneno haya " mm mke wangu nishamuwacha" na mke wake hakumwambia hilo lkn ameisema kauli hio. Jee talaka hii itakuwa imesihi ?
25-04-2023 05:34:30
Asalaam Aleykum warahmatulahi wabarakatuhu, mimi swali langu ni kuhusu Rukuu, ukiwa kwenye Rukuu macho unafaa kuangazia wapi? kunao wanao sema unafaa kuangalia unako enda kusijudu na wengine husema unafaa kuangalia vidole vya miguu zako. ni ipi sahihi naomba kufahamu. Shukran wabillahi tawfiq
28-01-2023 20:04:16
Nahitaji kujua UDUGU ni nini? Faida za udugu na hasara za kuvunja udugu katika uislam
31-03-2023 07:36:12
A,aleikum
Mwanamke akiwa kwa eda ndo kwanza anaanza kuuachwa je inarusikika mke uyo kwenda kwa kadhi na kudai talaka ?
30-01-2023 16:58:22
Eleza kwa muhtasari kwa nni waislamu ktk jamii yako hawafikii lengo la kwao pamoja.na kutekeleza ibada maalum
30-01-2023 15:53:28
Dai lakuea mtume muhammad anafundishwa quran na watu na udhaifu wa madai haya
14-02-2023 06:09:48
Às/alaikum.naomba kuuliza kupagiwa formula ya mgao wa mirathi..marehem kaacha mil 18 kaacha watoto wa kiume 5 na wa kike 6
20-02-2023 11:02:34
Bainisha sifa za dini sahihi amboyo anastahili kufuata
30-01-2023 15:52:44
Asalam alaykum nataman kujua zaidi kuhusu kisimamo Cha usiku
08-03-2023 05:32:40
Kijiji chao nabii ibrahim kinaitwaje..? Na kilikua kikaliwa na watu gani.?
14-02-2023 10:54:43
Kueleza wasifu wa malaika
31-01-2023 06:05:41
Assalaam alayka je' kwa yule ambaye anakipato cha chini anapaswa atoe zaka kiasi gani na kwa kipindi gan?
07-04-2023 03:45:09
As,alykum,فتنةا،نقلب علاوجهه ndugu .muislamu,naomba,nisaidie,endapo nitasimama kwenye,neno fitnatun.neno la mbele nitalianzaje?
31-01-2023 05:28:29
Aww ninaweza kupata clips za namna ya kuswali swala vita, namna ya kuosha maiti
27-02-2023 07:36:41
Asalam aleyikum warahmatullah wabarakatuh swali langu ni hivi mimi nimeolewa miaka 8 iyopita ila mwaka juzi mwezi12 Allah akanitahin nimepatatihani wa maradhi ya ganzi yamepelekea kutokutembea mama zamani,mume wangu ameniuguza mpaka mwezi wa 7 mwaka jana akanitelekeza yani aniudumii mimi wala mtoto na nikimpigia simu anaongea hovyo tu nimeamua kumdai talaka ataki kunipa lakini hivi karibuni ameniatamkia maneno Machafu kua ataki kunipa talaka kwakua ajawahi kunioa na ajanopenda hata siku1 mimi nikampiga mshenga na shahidi nao wakajaribu kizungumza nae akawakatia Simu swalilngu je,naweza kujivua kwenye ndoa hii?au nifanyeje mpaka nipate haki yangu ya talaka
11-02-2023 03:10:15
Mm na tanataka kujenga nyumba kama ya mtume Muhammad swalallahu aley wasalam ❤️. Je nitapataje ramani ya nyumba ya mtume Muhammad swalallahu aley wasalam
10-02-2023 16:21:17
Je ni Sahihi kufunga mwezi wa shaaban katika siku 15 za mwisho
13-03-2023 13:59:48
nilitaka uniambie umuhimu wa kuamini qadar ktk maisha ya kila siku
26-01-2023 04:55:53
Swali kangu ni: Je Mwanamke mwenye heidh aweza kushika msahafu?
12-02-2023 14:10:16
Nauliza hv unaposwali swala yeyoe kuna dua yake au unaweza soma sura yoyote unayoijua
19-02-2023 13:19:24
Kuna watu wameona bomani mwanamke amefariki muislam mume mkristo katika utaratibu wa mirathi hapa ikoje na ameacha wazazi wawili yaani baba na mama na watoto watatu walizaa katika hiyo ndoa yao ya bomani
23-03-2023 07:20:57
Je ni yapi masharti ya funga/saum
26-03-2023 04:24:33