image

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)



“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. (12:7).

Baadhi ya mazingatio kutokana na kisa hiki ni haya yafuatayo:



(i) Mitume huzaliwa Mitume na maisha yao yote kuanzia utotoni ni kiigizo cha tabia njema kwa waumini



(ii) Wazazi hatunabudi kuwafunza watoto wetu tabia njema na kuwalea hivyo mpaka utuuzima wao.



(iii) Watoto wenye tabia njema tuwapende na tuwashajiishe kubakia na mwenendo huo.



(iv) Si vema kutangaza neema tulizo nazo kwa watu hata wale wa karibu yetu ili kujikinga na husuda.



(v) Uislamu ni neema kubwa, hivyo kila atakayejaaliwa kufuata Uislamu vilivyo na kufanya jitihada za kuusimamisha katika jamii,ajiandae kuhusudiwa na makafiri na wanafiki.



(vi) Hila za watu wenye roho mbaya na husuda dhidi ya watu wema wenye kujitahidi kusimamisha Uislamu katika jamii mwisho wake huwafedhehesha wenyewe hapa hapa duniani kama walivyofedheheka ndugu zake Yusufu na mkewe Al-aziz.



(vii) Kutenda mema, ukweli na subira humnyanyua mtu daraja hapa duniani na huko akhera.



(viii) Ukweli ukidhihiri uwongo hujitenga kama tulivyoona kwa nduguze Yusufu na mkewe Al-Aziz.



(ix) Muungwana katika watu ni yule anayekiri makosa yake na kuomba msamaha kama walivyofanya nduguze Yusufu(a.s).



(x) Waumini wanatakiwa wamuige Yusufu(a.s) kwa kuwa wepesi wa kusamehe na kulipa wema badala ya kulipiza kisasi baada ya kufanyiwa ubaya na kisha kuombwa msamaha. Pamoja na Yusufu kuwasamehe ndugu zake, aliwapatia chakula wakati wa njaa na kuwakaribisha Misr katika makazi ya Kifalme.



(xi) Ngao dhidi ya mahasidi, mafatani, n.k. ni kumcha – Mungu, subira,kujitegemeza kwa Allah(s.w) na kuomba kinga yake.



(xii) Hatunabudi kutumia fursa zinazojitokeza katika kulingania Uislamu, kama Yusufu(a.s) alivyoitumia fursa ile alipokutana na wale wafungwa wawili.



(xiii)Matwaaghuuti daima hawawezi kuhukumu kwa uadilifu na kutoa haki sawa hasa pale kesi itakapokuwa ni baina ya mdau wa nchi na raia wa kawaida. Ilidhihirika kwa ushahidi wa wazi kuwa Yusufu(a.s) ndiye aliyekosewa na yule mkewe Al-Aziz, lakini kwa kumlinda na kashfa ile ilibidi Yusufu(a.s) ahukumiwe kwenda gerezani.



(xiv)Waumini wanapobambikiziwa maovu na machafu kutokana na husuda na chuki ya makafiri na wanafiki, wasitengeneze majukwaa ya kujitetea bali waendelee kufanya wema kama Allah(s.w)anavyoagiza:




Na sema(uwaambie): “Tendeni mambo (mazuri). Mwenyezi Mungu atayaona mambo yenu hayo na Mtume Wake na Waislamu. Na mtarudishwa kwa Mjuzi wa siri na dhahiri; naye atakwambieni (yote) mliyokuwa mkiyatenda.” (9:105)


(xv)Tunapokubalika na kuhitajika kuongoza jamii hatunabudi kupendekeza tukabidhiwe kuongoza katika maeneo tunayoyamudu vizuri kitaaluma, kiuzoefu na kiuadilifu na hasa pale tutakapoona hapana watu wengine wa kuongoza kwa uadilifu katika maeneo hayo.



(xvi)Tuchague viongozi waadilifu na wenye tabia njema bila ya kujali ukabila, utaifa, n.k. Yusufu(a.s) alikuwa mtu wa kuja na mtumwa lakini alipewa Uongozi Misr kutokana na elimu yake, tabia yake njema na uadilifu wake.



(xvii)Kiongozi Muumini ni yule anayekumbuka na kuzingatia kuwa wadhifa alionao ni amana aliyokabidhiwa na Allah (s.w) kwa manufaa ya jamii, hivyo hujiepusha na kibri,

majivuno, kujikweza au tabia yoyote inayoashiria dharau kwa wenzake. Funzo hili tunalipata kwenye dua ya Nabii Yusufu(a.s).



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 638


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s. Soma Zaidi...

NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA) BINTI KHUWALD
MTUME Muhammad (s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W KABLA YA UTUME
MAISHA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...

Watu wa Mji Waliomuua Muislamu kwa Kuwa Amewasadikisha Wajumbe wa Allah(s.w)
Katika Suratul Yassin Allah(s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISA
Soma Zaidi...

tarekh 07
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...

Kifo cha Nabii Sulaiman
Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine. Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)
Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...

Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...