Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume


image


Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


  • Kuandaliwa Muhammad (s.a.w) wakati na baada ya kupewa Utume.

-    Maandalizi haya yalikuwa ya kimafunzo (maelekezo) yaliyotokana na wahay moja kwa moja ulipokuwa unamshukia, ulianza katika sura tatu zifuatazo;

 

  • Suratul-A’laq (96:1-5).

-  Huu ulikuwa wahay wa kwanza kabisa kumshukia Muhammad (s.a.w) 

   kama ifuatavyo;

              “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba, Amemuumba mwanaadamu kwa Alaq (pande la damu). Soma, na Mola wako ni Karimu sana. Ambaye amemfundisha (elimu zote) kwa msaada wa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu (chungu ya) mambo aliyokuwa hayajui.”

       

  • Suratul-Muzzammil (73:1-10).

-   Huu ulikuwa wahay wa pili kumshukia Mtume (s.a.w) kama ifuatavyo;

“Ewe uliyejifunika maguo! Simama usiku (kucha kufanya ibada), ila muda mdogo (tu hivi) nusu yake au ipunguze kidogo au izidishe na soma Qur’an vilivyo. Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito. Hakika kuamka usiku (na kufanya ibada) kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi. Hakika mchana una shughuli nyingi. Na litaje jina la Mola wako na ujitupe kwake kwa kweli. (Yeye ndiye)  Mola wa mashariki na magharibi, hakuna muabudiwa wa haki ila Yeye, basi mfanye kuwa mlinzi (wako). Na subiri juu ya hayo wasemayo (hao makafiri) na uwaepuke mwepuko mwema.” 

 

  • Suratul-Muddaththir (74:1-7).

-  Huu ulikuwa ni wahay wa tatu kumshukia Mtume (s.a.w) kama 

    ifuatavyo;

                      “Ewe uliojifunika maguo. Simama na uonye (watu) na Mola wako umtukuze. Na nguo zako uzisafishe (uzitwaharishe). Na mabaya yapuuze. Wala usiwafanyie watu ihsani (viumbe) ili upate kujikithirisha. Na kwa ajili ya Mola wako fanya subira.”



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?
Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu) Soma Zaidi...

image Tawhiid
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...

image Uchambuzi wa hadithi za mtume
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Haki za nafsi
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.
Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake. Soma Zaidi...

image Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya zakat
Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...