Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuandaliwa Muhammad (s.a.w) wakati na baada ya kupewa Utume.
- Maandalizi haya yalikuwa ya kimafunzo (maelekezo) yaliyotokana na wahay moja kwa moja ulipokuwa unamshukia, ulianza katika sura tatu zifuatazo;
- Suratul-A’laq (96:1-5).
- Huu ulikuwa wahay wa kwanza kabisa kumshukia Muhammad (s.a.w)
kama ifuatavyo;
“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba, Amemuumba mwanaadamu kwa Alaq (pande la damu). Soma, na Mola wako ni Karimu sana. Ambaye amemfundisha (elimu zote) kwa msaada wa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu (chungu ya) mambo aliyokuwa hayajui.”
- Suratul-Muzzammil (73:1-10).
- Huu ulikuwa wahay wa pili kumshukia Mtume (s.a.w) kama ifuatavyo;
“Ewe uliyejifunika maguo! Simama usiku (kucha kufanya ibada), ila muda mdogo (tu hivi) nusu yake au ipunguze kidogo au izidishe na soma Qur’an vilivyo. Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito. Hakika kuamka usiku (na kufanya ibada) kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi. Hakika mchana una shughuli nyingi. Na litaje jina la Mola wako na ujitupe kwake kwa kweli. (Yeye ndiye) Mola wa mashariki na magharibi, hakuna muabudiwa wa haki ila Yeye, basi mfanye kuwa mlinzi (wako). Na subiri juu ya hayo wasemayo (hao makafiri) na uwaepuke mwepuko mwema.”
- Suratul-Muddaththir (74:1-7).
- Huu ulikuwa ni wahay wa tatu kumshukia Mtume (s.a.w) kama
ifuatavyo;
“Ewe uliojifunika maguo. Simama na uonye (watu) na Mola wako umtukuze. Na nguo zako uzisafishe (uzitwaharishe). Na mabaya yapuuze. Wala usiwafanyie watu ihsani (viumbe) ili upate kujikithirisha. Na kwa ajili ya Mola wako fanya subira.”
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 ai web app 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Kisa cha Israa na Miraji na kufaradhishwa swala tano
Safari ya Mi'rajKatika mwaka wa 12 B.
Soma Zaidi...Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi
Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.
Soma Zaidi...Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mji wa Makkah na kabila la kiqureish
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...