Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuandaliwa Muhammad (s.a.w) wakati na baada ya kupewa Utume.
- Maandalizi haya yalikuwa ya kimafunzo (maelekezo) yaliyotokana na wahay moja kwa moja ulipokuwa unamshukia, ulianza katika sura tatu zifuatazo;
- Suratul-A’laq (96:1-5).
- Huu ulikuwa wahay wa kwanza kabisa kumshukia Muhammad (s.a.w)
kama ifuatavyo;
“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba, Amemuumba mwanaadamu kwa Alaq (pande la damu). Soma, na Mola wako ni Karimu sana. Ambaye amemfundisha (elimu zote) kwa msaada wa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu (chungu ya) mambo aliyokuwa hayajui.”
- Suratul-Muzzammil (73:1-10).
- Huu ulikuwa wahay wa pili kumshukia Mtume (s.a.w) kama ifuatavyo;
“Ewe uliyejifunika maguo! Simama usiku (kucha kufanya ibada), ila muda mdogo (tu hivi) nusu yake au ipunguze kidogo au izidishe na soma Qur’an vilivyo. Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito. Hakika kuamka usiku (na kufanya ibada) kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno (yake) yanatua zaidi. Hakika mchana una shughuli nyingi. Na litaje jina la Mola wako na ujitupe kwake kwa kweli. (Yeye ndiye) Mola wa mashariki na magharibi, hakuna muabudiwa wa haki ila Yeye, basi mfanye kuwa mlinzi (wako). Na subiri juu ya hayo wasemayo (hao makafiri) na uwaepuke mwepuko mwema.”
- Suratul-Muddaththir (74:1-7).
- Huu ulikuwa ni wahay wa tatu kumshukia Mtume (s.a.w) kama
ifuatavyo;
“Ewe uliojifunika maguo. Simama na uonye (watu) na Mola wako umtukuze. Na nguo zako uzisafishe (uzitwaharishe). Na mabaya yapuuze. Wala usiwafanyie watu ihsani (viumbe) ili upate kujikithirisha. Na kwa ajili ya Mola wako fanya subira.”
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.
Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a.
Soma Zaidi...