Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.
Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.Watu wakamiminika Misri kuhemea chakula. Miongoni mwao wakawa ni wale ndugu zake Yusufu(a.s).
Wakaja ndugu zake Yusufu, na wakaingia kwake akawajua(12:58)
Wakapewa chakula na wakarejeshewa bidhaa zao walizoleta kubadilisha na chakula. Kisha Yusufu (a.s.) akawaagiza:
Na alipowapatia chakula chao alisema. (mkinijia mara ya pili) Nijieni na ndugu yenu wa kwa baba. Je hamuoni ya kwamba mimi ninatimiza kipimo, na ni mbora wa wakaribishao. (12:59)
Basi waliporejea kwa baba yao, walisema: “Ewe baba yetu! Tutazuiliwa (chakula mara ya pili mpaka twende na ndugu yetu); basi mpeleke ndugu yetu pamoja nasi ili tupate kupimiwa; na yakini sisi tutamlinda.” (12:63).
Mzee Ya‘aquub(a.s), akasema:-Sitampeleka pamoja nanyi mpaka munipe ahadi kwa jina la Allah kwamba lazima mtamrejesha kwangu, isipokuwa nyote mzungukwe (na hatari au kufa). Basi walipompa ahadi yao alisema: Mwenyezi Mungu ndiye mlinzi juu ya haya tuyasemayo (12:66)
Baada ya kuchukua ahadi hii, Mzee Ya‘aquub aliwaambia wanawe kuwa wasiingie Misr kwa kutumia mlango mmoja,bali kila mmoja apitie mlango wake katika milango inayoingia humo(rejea Qur’an 12:67).
Kwa kuingia milango tofauti, Yusufu(a.s) alipata fursa ya kukutana na ndugu yake,Bin-Amin (wa kwa baba na mama) kabla ya wale wengine na kujitaambulisha kwake kisha kumfahamisha dhamira yake ya kumbakisha Misr-(rejea Qur’an 12:69)
Yusufu(a.s) alifanya hila ya kumbambikizia wizi ndugu yake kwa kuweka pishi ya kupimia ndani ya mzingo wake. Mara tu ya kuchukua mizigo yao na kuaga, palinadiwa kupotea kwa kipimo cha mfalme. Wote ndugu zake Yusufu(a.s) walikataa kuwa hawakuhusika na wizi wa chombo kile. Ikabidi ipitishwe sachi(search) na kikakutwa kwenye mzigo wa Bin Amin ambaye alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Misr. (rejea Qur’an 12:70-75).
Ndugu zake Yusufu(a.s) waliporejea nyumbani walimfahamisha mzee wao mkasa uliowapata. Mzee Ya‘aquub(a.s) alizidi kupata majonzi kwa kupotelewa na watoto wawili, lakini baadae alikuwa na matumaini ya kuwapata wote, ndipo akawaagiza wanawe:
Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusufu na nduguye, wala msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hawakati tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri (12:87)
Walipofika Misri walimtaka Yusufu(a.s) awafanyie ihsan kwa kuwapa chakula bure kwa vile hawakuwa na fedha ya kulipa huku wakimkumbusha kuwa Mwenyezi Mungu huwalip a watu wanaowatendea wema mwenzao. Hapo Y usufu(a.s) akawakumbusha:
Akasema: Je! Mnajua mliyomfanyia Yusufu na nduguye mlipokuwa ujingani?(12:89)
Wakasema: Je! Wewe ndiye Yusufu? Akasema: Mimi ndiye Yusufu, na huyu ni ndugu yangu. Mwenyezi Mungu ametufanyia hisani. Hakika anayemcha Mungu na kusubiri , basi Mwenyezi Mungu hapotezi malipo ya wafanyao mema(12:90)
Nduguze wakakiri makosa yao waliyomfanyia Yusufu(a.s) na kumuomba awasamehe. Wakasema: Wallahi! Mwenyezi Mungu amekuchagua juu yetu, na hakika sisi tulikuwa wenye makosa. (12:91)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s.
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija.
Soma Zaidi...