image

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake

Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake


Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.Watu wakamiminika Misri kuhemea chakula. Miongoni mwao wakawa ni wale ndugu zake Yusufu(a.s).



Wakaja ndugu zake Yusufu, na wakaingia kwake akawajua(12:58)

Wakapewa chakula na wakarejeshewa bidhaa zao walizoleta kubadilisha na chakula. Kisha Yusufu (a.s.) akawaagiza:





Na alipowapatia chakula chao alisema. (mkinijia mara ya pili) Nijieni na ndugu yenu wa kwa baba. Je hamuoni ya kwamba mimi ninatimiza kipimo, na ni mbora wa wakaribishao. (12:59)

Basi waliporejea kwa baba yao, walisema: “Ewe baba yetu! Tutazuiliwa (chakula mara ya pili mpaka twende na ndugu yetu); basi mpeleke ndugu yetu pamoja nasi ili tupate kupimiwa; na yakini sisi tutamlinda.” (12:63).



Mzee Ya‘aquub(a.s), akasema:-Sitampeleka pamoja nanyi mpaka munipe ahadi kwa jina la Allah kwamba lazima mtamrejesha kwangu, isipokuwa nyote mzungukwe (na hatari au kufa). Basi walipompa ahadi yao alisema: Mwenyezi Mungu ndiye mlinzi juu ya haya tuyasemayo (12:66)



Baada ya kuchukua ahadi hii, Mzee Ya‘aquub aliwaambia wanawe kuwa wasiingie Misr kwa kutumia mlango mmoja,bali kila mmoja apitie mlango wake katika milango inayoingia humo(rejea Qur’an 12:67).



Kwa kuingia milango tofauti, Yusufu(a.s) alipata fursa ya kukutana na ndugu yake,Bin-Amin (wa kwa baba na mama) kabla ya wale wengine na kujitaambulisha kwake kisha kumfahamisha dhamira yake ya kumbakisha Misr-(rejea Qur’an 12:69)



Yusufu(a.s) alifanya hila ya kumbambikizia wizi ndugu yake kwa kuweka pishi ya kupimia ndani ya mzingo wake. Mara tu ya kuchukua mizigo yao na kuaga, palinadiwa kupotea kwa kipimo cha mfalme. Wote ndugu zake Yusufu(a.s) walikataa kuwa hawakuhusika na wizi wa chombo kile. Ikabidi ipitishwe sachi(search) na kikakutwa kwenye mzigo wa Bin Amin ambaye alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Misr. (rejea Qur’an 12:70-75).



Ndugu zake Yusufu(a.s) waliporejea nyumbani walimfahamisha mzee wao mkasa uliowapata. Mzee Ya‘aquub(a.s) alizidi kupata majonzi kwa kupotelewa na watoto wawili, lakini baadae alikuwa na matumaini ya kuwapata wote, ndipo akawaagiza wanawe:



Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusufu na nduguye, wala msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hawakati tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri (12:87)



Walipofika Misri walimtaka Yusufu(a.s) awafanyie ihsan kwa kuwapa chakula bure kwa vile hawakuwa na fedha ya kulipa huku wakimkumbusha kuwa Mwenyezi Mungu huwalip a watu wanaowatendea wema mwenzao. Hapo Y usufu(a.s) akawakumbusha:



Akasema: Je! Mnajua mliyomfanyia Yusufu na nduguye mlipokuwa ujingani?(12:89)

Wakasema: Je! Wewe ndiye Yusufu? Akasema: Mimi ndiye Yusufu, na huyu ni ndugu yangu. Mwenyezi Mungu ametufanyia hisani. Hakika anayemcha Mungu na kusubiri , basi Mwenyezi Mungu hapotezi malipo ya wafanyao mema(12:90)



Nduguze wakakiri makosa yao waliyomfanyia Yusufu(a.s) na kumuomba awasamehe. Wakasema: Wallahi! Mwenyezi Mungu amekuchagua juu yetu, na hakika sisi tulikuwa wenye makosa. (12:91)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 490


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake. Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...

Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam
“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”. Soma Zaidi...

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...

MASWALI MUHIMU KUHUSU HISTORIA NA MAISHA YA MTUME (S.A.W)
1. Soma Zaidi...

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

Shukurani za Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Allah(s.w)
Kwa neema hii ya kuruzukiwa watoto wawili - Ismail na Is- haqa(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISMAIL
Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...