image

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume

Warumi (Wakatoliki)


Warumi mpaka kufikia 7 A.H. sawa na 629 A.D. walikuwa ni Taifa kubwa (super Power) lililokuwa likitamba kwa nguvu za kishindo katika ulimwengu wa wakati huo. Baada ya mkataba wa Hudaybiyah Mtume(s.a.w) alituma wajumbe katika nchi mbali mbali za ndani na nje ya Bara Arabu. Miongoni mwa watawala waliopelekewa ujumbe na Mtume(s.a.w) ni mfalme wa Basra aliyepelekewa barua na Haarith bin ‘Umar Azid. Haarith alipofika Muttah aliuliwa na Shurahbil Ghassaany aliyekuwa Gavana wa Dola ya Kirumi chini ya Mfalme Heracleus.



Kumuua mjumbe lilikuwa ni kosa kubwa sana kwa sheria ya makabila ya Kiarabu wakati ule. Hivyo , Mtume(s.a.w) alipopata habari ya kuuliwa mjumbe wake, aliandaa jeshi la watu 3,000 chini ya Uamiri wa Zaid bin Harith kwenda Muttah kupambana na Gavana wa Warumi, Shurahbil Ghassaany. Wakati Mtume anatuma jeshi hili aliagiza:



“Kama Zaidi atauliwa, Ja’far bin Aby Taalib atakuwa Kamanda wenu, na kama naye atauliwa, ‘Abdullah bin Rawahah atachukua ukamanda. Kama naye atakufa mumchague kamanda kutokana na nyinyi.”



Shurahbil alipopata habari za kuja kwa jeshi la Waislamu aliandaa jeshi la askari laki moja (100,000) Jeshi la waislamu lilipofika njiani lilipata uvumi kuwa Heracleus anakuja na jeshi lingine la askari 100,000. Jeshi la Waislamu lilisita njiani siku mbili ili kuweka mikakati ya namna ya kupambana na jeshi kubwa kiasi hicho. Baada ya kushauriana Waislamu wote 3,000 katika kikosi kile waliamua kupambana na maadui zao na maadui wa Allah(s.w) kwa gharama yoyote ile.



Zaid aliongoza vita na mapambano makali yakaanza. Si muda mrefu kaka wa Shurahbil aliuliwa na yeye mwenye akakimbilia mafichoni kwenye ngome. Shurahbil alituma ujumbe kwa Mfalme Heracleus ambaye mara tu alituma jeshi lenye nguvu la askari 100,000 kujiunga katika mapambano dhidi ya Waislamu
3,000 tu. Waislamu wachache sana (3,000) wakawa wanapigana na jeshi kubwa sana (200,000) lenye nguvu na uzoefu wa vita. Uwiano wa jeshi la Waislamu na jeshi la Warumi ulikuwa 3,000:200,000 = 3:200 ni sawa na1:67


Zaid bin Harith aliuliwa na Ja’afar akachukua nafasi yake. Naye alipiganisha kwa ushujaa mpaka akafa shahidi. Baada ya Ja’afar, ‘Abdullah bin Rawahah alichukua bendera ya vita naye akafa shahidi. Baada yake Waislamu walimchagua Khalid bin Walid kuwa kamanda wao. Waislamu chini ya uongozi wa Khalid waliendelea kupigana kwa ushujaa mkubwa. Katika mchana mmoja wa mapigano Khaild alichakaza panga nane na katika usiku wake, ilibidi Warumi waombe kuakhirisha vita mpaka kesho yake.



Siku iliyofuatia Khalid aliwapanga askari wake katika mstari mrefu kama vile anataka kuwazingira maadui na kuwaweka katikati. Warumi waliogopa kujitokeza kwenye uwanja wa mapambano siku ile. Naye Khalid kama mbinu ya kivita, alilirejesha jeshi lake Madina. Warumi walifurahi sana kuona vita vimekwisha, kwani hawakuwa na nguvu tena ya kupambana na Khalid. Kwa upande mwingine, Waislamu wa Madina hawakufurahishwa na kitendo cha jeshi la Waislamu kuacha mapigano na kurudi Madinah bila ya kupata ushindi. Waliwatupia michanga ya usoni huku wakiwasimanga.

“Enyi mliokimbia vita! Mnakimbia njia ya Allah”!



Mtume(s.a.w) aliwaliwaza na kujibu mashambulizi kwa niaba yao, “Sio wakimbizi, Inshaa Allah watarudi tena”. Ni kweli kuwa hawakuwa na dhamira ya kukimbia vita bali walirejea Madina ili kukusanya nguvu upya. Mtume(s.a.w.) na Waislamu walipata majonzi makubwa kwa kuwapoteza mashujaa wengi na hasa wale makamanda watatu.



Mafunzo Yatokanayo na Vita vya Muttah


Waislamu hawakufurahia kuwaona wenzao wanarudi bila ya ushindi. Kwa Waislamu, walikuwa na mawili tu ya kupata katika vita, ushindi au kufa shahidi katika njia ya Allah. Hawakuzoea kabisa kurudi nyuma, ila iwe kama mbinu ya kivita ili kutafuta nguvu zaidi kama alivyofanya Khalid ambayo inaruhusiwa:
“Enyi mlioamini! Mkutanapo vitani na wale waliokufuru basi msiwageuzie migongo (mkakimbia). (8:15)




Na atakayewageuzia mgongo wake siku hiyo – isipokuwa amegeuka kwa kushambulia au amegeuka akaungane na sehemu nyingine ya jeshi hili hili la Waislamu (ikiwa si hivyo) – atastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na mahali pake ni Jahanamu. Napo ni mahali pabaya pa kurejea (mtu). (8:16)



Wakristo katoliki (Warumi) hawakujiona kuwa wameshinda wala kushindwa. Hawakushinda kwa sababu wao ndio waliogopa kukabiliana na Waislamu na wakakataa kujitokeza kwenye uwanja wa mapambano. Hawakushindwa kwa sababu Waislamu hawakuendelea kupambana nao mpaka kuwafikisha katika kilele cha kushindwa. Hata hivyo Warumi (Wakristo) walishangazwa sana na ushujaa wa Waislamu. Waliona kuwa ni jambo la hatari kubwa kupigana na Waislamu ambao walishambulia kama simba na kila mmoja alikuwa kama vile ana maisha mengi (uhai mwingi).



Walishuhudia nguvu za Waislamu kwa mifano waliyoipata kwa watu kama Ja’far ambaye aliendelea kupigana baada ya mikono yake yote miwili kukatwa; na Khalid ambaye alichakaza panga nane katika kipindi kifupi cha mchana mmoja wa mapambano. Hivyo, walishafikia hatua ya kukata tamaa na walipendelea kuomba suluhu lakini kutokana na kibri chao waliona haya kufanya hivyo. Kwa hiyo walifurahi sana walipoona Waislamu wenyewe wameamua kuondoka na hawakuamini macho yao.



Kwa upande mwingine, Mayahudi na washirikina walifurahi sana kwa msiba uliowapata Waislamu. Walifikia hatua ya kujiwa na mawazo kuwa nuru ya Uislamu itazimwa na Wakristo (Warumi). Wakati vita baina ya Waislamu na Warumi vinaendelea, Mayahudi na washirikina walikuwa wakifanya njama za kuwahujumu Waislamu.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 252


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani
Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a. Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Kifo cha Nabii Sulaiman
Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine. Soma Zaidi...

NASABA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABILA LAKE, UKOO WAKE NA FAMILIA YAKE
NASABA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII HUD(A.S) NA WATU WA 'AD
Baada ya Nuhu(a. Soma Zaidi...

Uendeshaji na Kupanuka kwa Dola ya Kiislamu Kipindi cha Makhalifa Waongofu
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII HUD
Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)
Ismail(a. Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA BANI ISRAIL
Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...