HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)

Nabii Shu’ayb(a.

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)

Nabii Shu’ayb(a.s) alitumwa kwa watu wa Madian waliokuwa wakikaa pande za pwani ya Shamu (Syria). Watu hawa walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa zama hizo. Mji wao ulikuwa katika njia kuu (Highway) ya misafara ya biashara kutoka sehemu mbali mbali za Mashariki ya kati kuelekea pwani ya bahari ya Mediterranean.



Tabia ya watu wa Madian


Wamadian pamoja na kuwa wafanyabiashara mashuhuri walikuwa na tabia ya kupunja vipimo wakati wa kuuza. Pia walikuwa wababe wakifanya uharibifu katika ardhi, walikuwa majambazi wakipora na kunyang’anya watu mali zao. Vile vile walikuwa washirikina na kuzuia watu kufuata Dini ya Allah(s.w).


Ujumbe wa Nabii Shu’ayb kwa Watu Wake


Nabii Shu’ayb(a.s) kama walivyofanya Mitume waliomtangulia aliwanasihi watu wake kumwamini na kumuabudu Allah(s.w) ipasavyo katika maisha yao ya kila siku na kusimamisha uadilifu katika jamii.




Na kwa watu wa Madian (tulimpeleka) ndugu yao, Shuaibu. Akasema: “Enyi watu wangu! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Msipunguze kipimo (cha vibaba) wala (cha) mizani. Mimi nakuoneni mumo katika hali njema (basi msiiharibu kwa kufanya dhulma).Nami nakukhofieni adhabu ya siku (kubwa) hiyo itakayokuzungukeni.” (11:84)



Nabii Shu’ayb(a.s) aliendelea kuwaasa watu wake:

“Wala msikae katika kila njia kuogopesha (watu) na kuwazuilia na Dini ya Mwenyezi Mungu (wale) wenye kuamini, na kutaka kuipotosha Na kumbukeni mlipokuwa wachache, Naye akakufanyeni kuwa wengi (sasa).Na tazamneni jinsi ulivyokuwa mwisho wa waharibifu.” (7:86)HISTORIA YA NABII



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2763

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu
Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Soma Zaidi...
Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi
Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi

Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.

Soma Zaidi...
Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake

Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.

Soma Zaidi...