Nabii Shu’ayb(a.
Nabii Shu’ayb(a.s) alitumwa kwa watu wa Madian waliokuwa wakikaa pande za pwani ya Shamu (Syria). Watu hawa walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa zama hizo. Mji wao ulikuwa katika njia kuu (Highway) ya misafara ya biashara kutoka sehemu mbali mbali za Mashariki ya kati kuelekea pwani ya bahari ya Mediterranean.
Wamadian pamoja na kuwa wafanyabiashara mashuhuri walikuwa na tabia ya kupunja vipimo wakati wa kuuza. Pia walikuwa wababe wakifanya uharibifu katika ardhi, walikuwa majambazi wakipora na kunyang’anya watu mali zao. Vile vile walikuwa washirikina na kuzuia watu kufuata Dini ya Allah(s.w).
Nabii Shu’ayb(a.s) kama walivyofanya Mitume waliomtangulia aliwanasihi watu wake kumwamini na kumuabudu Allah(s.w) ipasavyo katika maisha yao ya kila siku na kusimamisha uadilifu katika jamii.
Na kwa watu wa Madian (tulimpeleka) ndugu yao, Shuaibu. Akasema: “Enyi watu wangu! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Msipunguze kipimo (cha vibaba) wala (cha) mizani. Mimi nakuoneni mumo katika hali njema (basi msiiharibu kwa kufanya dhulma).Nami nakukhofieni adhabu ya siku (kubwa) hiyo itakayokuzungukeni.” (11:84)
Nabii Shu’ayb(a.s) aliendelea kuwaasa watu wake:
“Wala msikae katika kila njia kuogopesha (watu) na kuwazuilia na Dini ya Mwenyezi Mungu (wale) wenye kuamini, na kutaka kuipotosha Na kumbukeni mlipokuwa wachache, Naye akakufanyeni kuwa wengi (sasa).Na tazamneni jinsi ulivyokuwa mwisho wa waharibifu.” (7:86)HISTORIA YA NABII
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1958
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Kitau cha Fiqh
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 kitabu cha Simulizi
Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...
Mtume amezaliwa mwaka gani?
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...
Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...
HISTORIA YA BI KHADIJA (HADIJA) MKE WA KWANZA WA MTUME MUHAMMAAD (S.A.W)
HISTORIA YA BI KHADIJABi Khadija jinalake halisi ni Khadija bint Khuwald bin Asab baba yake alikuwa ni mfanya biashara. Soma Zaidi...
Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...
Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...
KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI
KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka. Soma Zaidi...
Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...
tarekh 4
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji. Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri
Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...
Zakaria(a.s) Akabidhiwa Ulezi wa Maryam
Baada ya kupigwa kura juu ya nani awe mlezi wa Maryam, Nabii Zakaria akachaguliwa kuwa mlezi wa Maryam. Soma Zaidi...