Menu



Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.a.w.) alishikwa na ugonjwa wa kuumwa kichwa na homa. Lakini muda wote alikuwa akijitokeza kufanya shughuli zake kama kawaida. Katika hali hiyo hiyo ya kuumwa, alikwenda Uhud na kuwaombea dua mashahidi waliozikwa mle. Pale alitoa khutuba ifuatayo:



“Siwahofii kuwa mtajihusisha na kuabudu masanamu baada yangu, lakini nahofia kuwa mtajihusisha sana na dunia kiasi cha kufikia hatua ya kuuana wenyewe kwa wenyewe. Kisha, mkishafanya hivyo, mtaishia kwenye maangamivu kama walivyoangamia wa kabla yenu”.



Mtume(s.a.w.) pamoja na maradhi yake aliendelea kuswalisha swala za jamaa msikiitni na bado alikuwa akitimiza ngono za wake zake wote tisa. Ugonjwa ulipozidi kushitadi, aliwaomba wakeze kuwa waje kumuuguza kwa Bibi Aysha(r.a.) palipo kuwa karibu na msikiti. Wakeze walikubali kwa moyo mkunjufu. Ugonjwa ulivyoendelea Mtume(s.a.w.) alizidi kuwa dhaifu na hatimaye alishindwa hata kuhudhuria swala za jamaa msikitini. Aliposhindwa kuhudhuria msikitini alitoa amri Abubakar awe anaongoza swala ya jamaa, alifanya hivyo kwa siku kadhaa.



Siku nne kabla ya kufariki kwake, Mtume(s.a.w.) alijisikia nafuu kidogo na akakoga kabla ya swala ya Dhuhuri. Baadaye alikuja msikitini akiwa amesaidiwa na watu wawili, Abbas(r.a.) na Ally(r.a.). Abubakar alikuwa anaendelea kuongoza swala kama kawaida. Alipomuona Mtume(s.a.w.) anakuja alianza kuondoka, lakini Mtume alimuambia abakie pale pale naye akakaa pembeni mwake. Baada ya swala alihutubia kama ifuatavyo:



“Allah amempa mja wake achague kati ya dunia na akhera. Akachagua akhera. Ninawausia, Enyi Waislamu (Muhajirina) muwe wema kwa Ansar. Hakika wametekeleza wajibu wao vizuri. Waislamu kwa ujumla wao idadi yao itaongezeka lakini Ansar watapungua na kuwa kama chumvi katika chakula. Zimeangamia umma zilizotangulia ambazo ziliabudu makaburi ya Mitume wao na ya watu wema. Ninawakatazeni kufanya hivyo. Nina deni kubwa (la Ihsani) kwa Abubakar. Kama ingekuwa nimfanye yeyote kuwa rafiki yangu, angalikuwa Abubakar, lakini uhusiano (udugu) wa Uislamu unatosha. Ee, binti yangu Fatimah na Ee, shangazi yangu mpendwa, Swafiyah, fanyeni amali kwa ajili ya akhera kwani sitaweza kuwasaidia chochote dhidi ya hukumu ya Allah.23



Hii ilikuwa khutuba ya mwisho ya Mtume (s.a.w.). Kisha ugonjwa ulishitadi. Alijisikia nafuu kidogo asubuhi ya Jumatatu ya mwezi 12 Rabi’ul-Awwal, 11 A.H, lakini ilipofika adhuhuri hali ilibadilika tena kuwa mbaya. Alikuwa akizimia kila baada ya muda mfupi. Hata alipokuwa katika hali hii ya sakaratul-maut, bado hakumsahau Mola wake. Muda wote alikuwa akisema “Nisamehe Bwana wangu”. Wakati wa alasiri alipokuwa anapumua pumzi za mwisho mwisho, alisikika kwa sauti ndogo akisema:

“Shikamana na swala na wafanyieni wema watumwa (wafungwa)”.



Palikuwa na beseni la maji lililowekwa karibu na Mtume (s.a.w.). Alikuwa akilowesha viganja vyake mara kwa mara kwenye maji haya na kufuta uso wake, huku akisema, “Enyi watu! Hakika kutoka roho kuna machungu makubwa”. Wakati huo aliingia mtu mmoja na mswaki mkononi mwake. Mtume akaashiria apewe mswaki huo. Alitafuniwa na Bibi Aysha, ambaye alimpakata mapajani mwake, na kumpa akawa anaswakia kidogo kidogo. Kisha akiwa ameashiria kwa kidole (cha shahada) na huku ametazama juu alisema mara tatu:



“Nakwenda kwa rafiki yangu mtukufu,

Nakwenda kwa rafiki yangu mtukufu,

Nakwenda kwa rafiki yangu mtukufu”.



Roho yake ilirudi kwa Bwana na Mola wake mtukufu wakati wa jioni ya Jumatatu ya mwezi 12 Rabi’ul Awwal, 11 A.H, Sawa na tarehe 8 Juni 632 A.D. Mtume(s.a.w.) alifariki akiwa na umri wa miaka 63. Mazishi yake yalifanyika siku iliyofuatia. Waliomwosha ni jamaa zake wa karibu – Fadhil bin Abbas, Ally bin Abu Talib na Usamah bin Zaid(r.a.). Kisha alizikwa kwenye chumba cha Bibi Aysha(r.a.) pale pale alipofia. Hivi sasa kaburi la Mtume(s.a.w.) limo ndani ya Msikiti wa Madinah.




“Ee Allah! Mrehemu Muhammad na wafuasi wa Muhammad kama ulivyomrehemu Ibrahim na wafuasi wa Ibrahim. Hakika wewe U-mtukufu na Msifiwa wa haki “Ee Allah! mbariki Muhammad na wafuasi wa Muhammad kama ulivyombariki Ibrahim na wafuasi wa Ibrahim. Hakika wewe U-mtukufu na Msifiwa wa haki.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1085


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mateso waliyoyapata waislamu wa mwanzo Maka, na orodha ya waislamu walioteswa vikali
Pili, Maquraish walimuendea Mtume(s. Soma Zaidi...

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s. Soma Zaidi...

Sababu za makafiri wa kiqureish kuupinga ujumbe wa uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SALEHE
Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri
Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji. Soma Zaidi...

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri? Soma Zaidi...