2.
2. JAMII ZA MASHARIKI
Kila jamii utakayoichunguza utakuta kunyanyaswa na kudhalilishwa kwa mwanamke kuko pale pale. Ukichunguza hata zile nchi zilizohesabika katika historia kuwa mbele katika maendeleo ya mwanaadamu kama vile China, India, Iraq na Iran, utasikitishwa na vitimbwi alivyokuwa akifanyiwa mwanamke. Hebu tuanglie baadhi ya jamii chache za nchi za Mashariki.
Uchina
Mwanamke wa Uchina alikuwa hana haki yoyote katika jamii. Hata watoto wake aliowazaa mwenyewe hakuwa na haki nao. Mume wake aliweza kuuza mwili wake kwa mume mwingine. Baada ya mumewe kufariki alirithiwa kama mali na ndugu wa mumewe na haikuwezekana kwake kuolewa tena. Juu ya yote hayo, wanawake waliuzwa na kufanywa watumwa. Mpaka kufikia 1937, Uchina ilikuwa na wasichana watumwa milioni mbili.
Katika kitabu chao kiitwacho, Marriage East and West (New York, 1960) David na Mace wanasema hadhi ya mwanamke huko Uchina ilikuwa duni sana. Mshairi mashuhuri wa China aliyeitwa Xuan,(100B.C) aliandika katika shairi moja:
Ni huzuni ilioje kuwa mwanamke Duniani hakuna kilicho duni Duniani hakuna kilicho duni kuliko mwanamke.
Mwana falsafa wao mkubwa, Bwana Confusious ambaye alikuwa pia kiongozi wa kidini aliwafundisha watu kuwa wajibu mkuu wa mwanamke ni utii. Akiwa mototo amtii baba yake, akiolewa amtii mumewe na akifiwa na mumewe basi amtii mwanawe wa kiume. Na atii kila kitu bila kuhoji. Wachina pia waliamini kuwa mtu akipata mtoto wa kiume amepata hidaya kutoka kwa Mwenyezi Mungu lakini akipata binti, basi ni nuksi.
India
Katika jamii ya India mwanamke hakuthaminiwa kabisa. Mwanamke alihesabiwa kama mashine ya uzazi. Iwapo mwanamke hakujaaliwa kupata mtoto wa kiume kwa mume aliyemuoa, alilazimishwa azini na mume asiyemjua iii apate mtoto wa kiume.
Budha, kiongozi wa kidini huko India aliwafundisha wafuasi wake kuwa mwanamke ni kiumbe duni aliyejawa na dhambi. Hakuna kiumbe anayefaa kuhofiwa na kuepukwa kama mwanamke. Na kwa mujibu wa sheria ya Manu wa huko huko India, wanawake ni lazima wabanwe na kudhibitiwa vikali kwani wao ndio chanzo cha madhambi yote na ufisadi.
Mwanamke hakuna na haki ya urithi bali urithi ulikuwa ni haki ya watoto wa kiume tu. Mke alitakiwa amwite mume wake ama Bwana wangu au Mungu wangu kwani mume alihesabiwa kuwa ni mungu wake hapa duniani. Ilikuwa marufuku mke kula pamoja na mumewe. Jimai hata kati ya mtu na mkewe ilihesabika kuwa ni kitu kiovu na kichafu. Mke mwema alikuwa yule ambaye akili zake, kauli yake na mwili wake si huru. Mke hakuruhusiwa kuolewa tena pindi mumewe akifariki. Ilibidi afanye moja katika mawili, ama ajichome moto ili afe na kumfuata mumewe au awe mtumishi wa shemeji zake hadi atakapo fariki. Mwenendo huu wa kujichoma moto au kuchomwa moto na mashemeji zake bado unaendelea hadi leo. Gazeti liitwalo "The Economist" 27 August - 2 September 1983 liliandika hivi:
The grisly practice of wife burning in India shows no sign of succumbing on its own to modern ideas about the value of a womans ' life. Many women are donsed with kerosene and set aflame by in-laws greedy for more dowries... The official figures shows 610 burnings in 1982.
Tafsiri:
Mwenendo wa kutisha wa kuwachoma moto wanawake huko India hauonyeshi dalili za kukoma kutokana na fikra za kisasa juu ya thamani ya uhai wa mwanamke. Wanawake wengi humwagiwa mafuta ya taa na kuchomwa moto na mashemeji kwa uroho wa kutafuta mahari nyingine. Taarifa rasmi ya serikali yaonyesha kuwa wanawake 610 walichomwa moto mwaka 1982. Hali ilikuwa hivyo hivyo huko Japan.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 487
Sponsored links
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
kitabu cha Simulizi
HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...
Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...
Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W KABLA YA UTUME
MAISHA YA MTUME (S. Soma Zaidi...
tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...
KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S. Soma Zaidi...
Jifunze historia ya uislamu toka mitume na manabii, kuja kwa makhalifa na maimamu hadi leo
Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUUMBWA KWA NABII ADAMU (A.S)NA HADHI YAKE NA HADHI YA WANAADAMU DUNIANI
Adam(a. Soma Zaidi...