image

Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal

Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal

Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal


Imam Abu Abdallah Ahmad bin Muhammad bin Hambal alizaliwa huko Marwa mwezi 20 Rabi-al-Awwal 164 A.H. Baba yake Muhammad alikuwa mujahid aliyesifika wakati akiishi Basra, Iraq. Baba yake alihamia Baghdad ambapo alifariki muda mfupi baadae na kumuacha Ahmad bin Muhammad akiwa bado mchanga. Pamoja na uyatima wake, kijana Ahmad alikuwa mwenye akili na akautumia ujana wake wote katika kujielimisha. Alisoma zaidi Hadith na akawa mwanasheria na mtaalam wa fiqh katika zama zake. Kwa hiyo Imam Shafii na Imam Ahmad Hambal walikuwa karibu sana. Imam Hambal alimheshimu mwalimu wake Shafii, na Imam Shafii alimheshimu mwanafunzi wake mashuhuri Hambal.


Imam Ahmad Hambal alikuwa mwanachuoni Mcha Mungu sana aliyejitoa maisha yake yote kusoma na kufundisha Hadith na Fiqh. Kwa ucha Mungu wake alikataa kufanya kazi Serikalini, kwani aliona Serikali ilikuwa haiongozwi kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah. Zaidi ya hivyo alivunja uhusiano wa karibu na wote wale waliokubali kuwa ndani ya Serikali ya kidhalimu. Alikataa hata kupokea fedha au chakula kutoka kwa mtoto wake ambaye alikuwa akifanya kazi katika Serikali ile ya kidhalimu. Hata wakati alipokabiliwa na hali ngumu ya uchumi hakukubali kupokea msaada wowote ila kwa kuufanyia kazi.


Katika kipindi cha uhai wa Imam Ahmad waliibuka wanafalsafa waliokuja na falsafa iliyoitwa Mu’tazili. Falsafa hii iliwaita watu wawe huria katika fikra. Walichanganya imani na kufr hata kufikia kuleta hoja kuwa Qur’an imetengenezwa tu. Harakati hizi za kuleta kufr ndani ya Uislamu zilitokana na athari ya falsafa za Wagiriki zilizowalevya baadhi ya Waislamu wa zama hizo.


Bahati mbaya watawala wa zama hizo nao waliathiriwa na falsafa hizo za Kigiriki na wakataka kuifanya kuwa imani rasmi ya dola ya Kiislamu. Viongozi waliotaka kuisimika imani hiyo ni Khalifa Ma‘mun al-Rashid; Mu’taslim Billah na Al-Wathiq. Imam Ahmad bin


Hambal alikataa kuikubali imani hiyo mpya ya watawala na akaendesha harakati kuipinga. Mtawala Mu’taslim alitoa amri akamatwe afungwe minyororo na kuhamishiwa Tarsus toka Baghdad. Huko alitupwa gerezani na kuteswa sana mpaka viungo vyake vingi vikavunjika. Imam Ahmad aliachwa adumu amefungwa minyororo mizito ndani ya chumba chenye giza gerezani. Pamoja na kuteswa sana ikiwa ni pamoja na kuchapwa mpaka kutoka damu, Imam Ahmad hakutetereka katika msimamo wake. Msimamo huu wa Imam Ahmad ulimstua Khalifa Mu’taslim. Aliikumbuka Akhera akahofia khatima yake. Aliamuru Imam Ahmad atolewe gerezani mwezi 25 Ramadhan mwaka 221 A.H na akamuomba msamaha, Imam Ahmad akamsamehe.


Miongoni mwa kazi muhimu alizofanya Imam Ahmad ni kuandika vitabu vifuatavyo: Kitab al-Amal al-Tafsir; Kitab al- Nasikh wal-Mansukh na kadhalika. Lakini kazi muhimu zaidi aliyoiacha Imam Ahmad ni ukusanyaji wa Hadith elfu nyingi na kuandika kitabu cha Hadith cha Musnad ya Ibn Hambali. Ulipofika mwaka wa 241 A.H Imam Ahmad alifariki dunia. Maelfu ya watu wa Baghdad walifurika kumzika.





                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 633


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.
Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s. Soma Zaidi...

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini
Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika Surat Ar-Raad (13:19-26)
Soma Zaidi...

Miujiza Kama Ushahidi wa Utume wa Nabii Musa(a.s)
Allah(s. Soma Zaidi...

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume
Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili. Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s. Soma Zaidi...

Vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuhifadhiwa kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...