image

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)

Ayyuub(a.

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)


Ayyuub(a.s) ni katika Mitume wa Allah(s.w) waliotajwa katika Qur-an kwa umadhubuti wake katika imani juu ya Allah(s.w) na Subira.

Ayyuub(a.s) aliishi Kaskazini Mashariki ya Bara Arabu. Alikuwa tajiri sana mwenye mali nyingi, watoto wengi na watumishi wengi. Lakini hakutakabari bali alimuabudu Mola wake na kumshukuru ipasavyo

Mitihani Iliyomfika Ayyuub(a.s)


Nabii Ayyuub(a.s) alitahiniwa na Mola wake kama ifuatavyo:

(1) Mali yake, watoto wake na watumishi wake wote walipatwa na majanga wakatoweka. Akabakia yeye na mkewe ambaye naye alikuwa mcha-Mungu.

(2) Pamoja na kupotelewa na mali yake na watu wake wote, alishikwa na maradhi mabaya ya kuota vidonda mwili mzima kuanzia kichwani hadi miguuni. Alijaribu kutumia dawa zote alizoweza, lakini hakupata nafuu yoyote


Nabii Ayyuub(a.s) hakutetereka katika imani yake kutokana na majanga yaliyomfika bali alisubiri na kuwa karibu zaidi na Mola wake kuliko hata wakati alipokuwa katika hali yake ya mwanzo ya utajiri na afya nzuri. Na Allah(s.w) anamsifu mjawake, Ayyuub kama ifuatavyo:

“…. Bila shaka tulimkuta ni mwenye subira mja mwema; kwa hakika alikuwa mnyenyekevu sana.” (38:44)

Nabii Ayyuub(a.s) aliona kuwa aliyempa mali, watoto na wale watumishi aliokuwa nao ni Allah(s.w) kama amana. Hivyo, aliona hapakuwa na kosa lolote kwa Allah(s.w) kuchukua amana yake. Pia aliridhika na hali ya ugonjwa aliyokuwa nayo. Kwa ujumla Nabii Ayyuub (a.s) aliridhika na kusubiri juu ya matatizo yote yaliyomfika na kupata matunda ya subira kama Allah(s.w) anavyotubashiria:

Na tutakutieni katika msukosuko wa (baadhi ya mambo haya); hofu na njaa na upungufu wa mali na wa watu na wa matunda. Na wapashe habari njema wanaosubiri.(2:155) Ambao uwapatapo msiba husema: “Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye tutarejea (atatupa jaza yake).(2:156)

Hao juu yao zitakuwa baraka zitokazo kwa Mola wao na rehema; na ndio wenye kuongoka. (2:157)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1318


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISA
Soma Zaidi...

Kuendeshwa kwa dola ya kiislamu, Uchumi, ulinzi, haki na sheria, siasa na vikao vya shura
Uendeshaji wa Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake
Mkewe Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII MUSA NA HARUNA
Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

Njama za Mayahudi Kutaka Kumuua Nabii Isa(a.s)
Njama za kutaka kumuua Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NI IPI FAMILIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA NI IPI NASABA YAKE, UKOO WAKE NA KABILA LAKE
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Khalifa ‘Umar bin Abdul Aziz
Soma Zaidi...