image

Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi

Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu.

Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi

Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi


Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu. Na hii imekuwa ni tabia ya watu wabaya kuwasingizia Mitume uovu ili wapate kuwapoteza watu na njia ya Allah. Nabii Suleiman katika jumla ya mambo aliyosingiziwa ni kuwa alikufuru akafundisha watu elimu ya uchawi. Qur'an inajibu shutuma hizo katika aya ifuatayo:




Wakafuata yale waliyoyafuata mashetani (wakadai kuwa yalikuwa) katika uflame wa Sulaiman; na Sulaiman hakukufuru, bali mashetani ndio waliokufuru, waliwafundisha watu uchawi (waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani) na (uchawi) ulioteremshwa kwa malaika wawili; Haruta na Maruta; katika (mji wa) Babil. Wala (Malaika hao) hawakumfundisha yeyote mpaka wambwambie: "Hakika sisi ni mtihani (wa kutazamwa kutii kwenu); basi usikufuru;" Wakajifunza kwao ambayo kwa mambo hayo waliweza kumfarikisha mtu na mkewe (na mengineyo). Wala hawakuwa wenye kumdhuru yeyoyte kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza ambayo yatawadhuru wala hayatawafaa. Na kwa yakini wanajua kwamba aliyekhiari haya hatakuwa na sehemu yoyote katika Akhera. Na bila shaka ni kibaya kabisa walichouzia nafsi zao. Laiti wangalijua (hakika wasingefanya hivi). (2:102)



Pamoja na aya hii kumtakasa Nabii Sulaiman na yale aliyokuwa akisingiziwa, mafundisho yafuatayo hapana budi tuyazingatie. Kwanza, tunafahamishwa kuwa elimu ya uchawi ipo; lakini ni mtihani kwa wanaadamu. Kujifundisha na kuufanyia kazi uchawi ni kufru na atakayehiari kuufuata hatakuwa na sehemu yoyote katika Akhera.



Jambo la pili tunalotakiwa tulizingatie ni kuwa Muislamu hana haja ya kubabaika anapopatwa na janga lolote. Mwenyezi Mungu anatufahamisha kuwa huo uchawi hauwezi kumdhuru mtu ila kwa idhini yake Allah(s.w).".............Wala hawakuwa wenye kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu….........." (2:102).



Kwa hiyo Muislamu amtegemee Allah(s.w) na alikabili tatizo lolote litakalomtokea kwa kuchunga mipaka ya Allah(s.w) na kuomba msaada wake.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 525


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA MTUME DAUD(A.S).
Nabii Daudi(a. Soma Zaidi...

Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo. Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Hud(a.s)
Waliomuamini Mtume Hud(a. Soma Zaidi...

Khalifa na Utungaji Sheria, na utiifu juu ya sheria na usimamiaji wa haki
Soma Zaidi...

tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...

Imam Muslim na Sahihul Mslim
Soma Zaidi...

Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi
Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu. Soma Zaidi...

Muhutasari wa sifa za wanafiki
Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo. Soma Zaidi...

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s. Soma Zaidi...