image

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)

Baada ya Nabii Salih(a.

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)


Baada ya Nabii Salih(a.s) kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa ufasaha na kwa uwazi, watu wake waligawanyika makundi mawili.

Wachache wao waliamini, wengi katika hao wakiwa dhaifu.Wengi wao wakiongozwa na wakuu wa jamii walikufuru. Makafiri wa Kithamud waliukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.s) kwa sababu zifuatazo:



Kwanza, Walimuona Salih(a.s) kuwa ni mwongo, kuwa hapana cha kuwepo Allah wala adhabu kutoka kwake.

Wakasema wale waliotakabari “Sisi tunayakataa yale mnayoyaamini. Na wakamtumbua (wakamuua) yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao na wakasema: “Ee Salih! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa Mitume. (7:76-77)



Wakamchinja. Basi (Salih) akasema: “Stareheni katika mji wenu huu (muda wa) siku tatu (tu, kisha mtaadhibiwa); hiyo ni ahadi isiyokuwa ya uwongo.” (11:65)



Pili,hawakuwa tayari kuacha miungu ya Babu zao:

Wakasema: “Ewe Salih! Bila shaka ulikuwa unayetarajiwa (kheri) kwetu kabla ya haya (Sasa umeharibika). Oh! Unatukataza kuabudu waliowaabudu baba zetu? Na hakika sisi tumo katika shaka inayotusugua (katika nyoyo zetu) kwa haya unayotuitia.” (11:62)



Tatu, walimuona Salih(a.s) kama mtu aliyerogwa na wakamdai kuleta muujiza:

Wakasema “Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa (wakakosa akili).” “Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi; basi lete muujiza ikiwa ni miongoni mwa wasemao kweli.” (26:153-154)





Nne, walidai kuwa Salih(a.s) na wale waliomuamini pamoja naye wameleta nuksi katika nchi kwa kule kuikataa kwao miungu ya masanamu. Wakasema: “Tumepata bahati mbaya, (ukorofi) kwa Sababu yako na kwa Sababu ya wale walio pamoja nawe.” Akasema: “Ukorofi wenu uko kwa Mwenyezi Mungu (kwa ajili ya ubaya wenu;) lakini nyinyi ni watu mnaojaribiwa (na Mwenyezi Mungu kuwa mtafuata au hamfuati).” (27:47)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 488


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

MASWALI MUHIMU KUHUSU HISTORIA NA MAISHA YA MTUME (S.A.W)
1. Soma Zaidi...

Ijuwe Dua ya Ayyuub(a.s)
Nabii Ayyuub(a. Soma Zaidi...

tarekh 3
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta
Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta Soma Zaidi...

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUNUS
Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

Imam Muhammad Idris al-Shafii
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)
Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W KABLA YA UTUME
MAISHA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Ghasia na chokochoko za Makhawariji na kuuliwa kwa Ally
Soma Zaidi...