Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.
Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.s) tunajifunza yafuatayo:
(i) Tunajifunza kuwa ni muhimu kuweka mipango katika kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii. Allah(s.w) anauwezo wa kukiamrisha kitu “kiwe” na kikawa pale pale, lakini bado tunaona ameweka mpango wa muda mrefu wa
(ii) Vile vile mpango huu wa Allah(s.w) wa kuwakomboa Bani Israil,unatufunza kuwa kuibadilisha jamii ya kijahili kuwa ya Kiislamu ni jambo linalohitaji muda na subira.
(iii) Elimu na siha ni nyenzo muhimu za kumuwezesha mtu kuwa khalifa katika ardhi. Nabii Musa alipewa siha nzuri na kuruzukiwa akili na elimu.
(iv) Hakuna hila wala nguvu zinazoweza kuzuia jambo analotaka Allah(s.w) liwepo au lisiwepo katika jamii, yeye anazo namna nyinyi za kumlinda mja wake na vile vile anaweza kumuangamiza mbabe yeyote awaye.
(v) Tabia njema na kuwatendea watu wema ni nyenzo muhimu katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii. Nabii Musa(a.s)kwa wema wake aliletewa taarifa ya mipango ya Firaun dhidi yake; pia kwa huruma yake alipata hifadhi kwa mzee wa Madian.
(vi) Hakuna binaadamu asiyeteleza na kumkosea Allah(s.w), lakini muumini anakuwa mwepesi wa kurejea kwa Allah (s.w).Musa(a.s) aliteleza kwa kuingilia ugomvi asioujua na kumuua mtu,alirejea kwa Mola wake haraka haraka–Qur-an (28:16).
(vii)Muumini wa kweli hanabudi kuchukia vitendo vya dhuluma na kuwa tayari kuwatetea wanaodhulumiwa haki zao kwa kadiri ya uwezo wake.
(viii)Ni muhimu kuwekeana mikataba ya kazi tunapoajiri au kuajiriwa. Nabii Musa(a.s) aliwekeana mkataba wa kazi na mzee wa Madian.
(ix) Nyenzo muhimu ya kutuwezesha kusimamisha Uislamu katika jamii baada ya Elimu ni kusimamisha Swala za Faradh na sunah,Qiyamullayl na kuleta dhikiri kwa wingi – Qur-an(20:14), (73:1-10), (74:1-7).
(x) Miujiza ni katika dalili za kuwepo Allah(s.w).
(xi) Katika harakati za kusimamisha Uislamu katika jamii tunatakiwa tusimvamie tu kila mtu na kumuingiza kwenye harakati, bali tuanze na ndugu, jamaa na rafiki wa karibu ambao tunajua fika tabia na mwenendo wao. Nabii Musa (a.s) aliomba ndugu yake Harun awe msaidizi wake si kwa kuwa alikuwa ndugu yake tu, bali alimfahamu fika kwa ucha Mungu wake.
(xii)Muumini mwanaharakati hahongeki kwa fadhila atakazofanyiwa na madhalimu ili arudi nyuma katika kusimamisha uadilifu. Musa(a.s) alilelewa katika nyumba ya mfalme,lakini hakuacha kudhihirisha kwa matendo udhalimu wa Firaun na serikali yake ikawa ndio sababu ya kuhukumiwa kifo.
(xiii)Ni kawaida ya matwaghuti kufanya propaganda dhidi ya wanaharakati na kuwapachika majina mabaya. Firaun na serikali yake alimpakazia Nabii Musa(a.s) uwendawazimu na uchawi.
(xiv)Hapana yeyote wa kumchelea katika kutekeleza amri ya Allah(s.w) ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Musa na Harun(a.s) walimkabili Firaun na wakuu wake wa Dola waliozungukwa na majeshi na kuwafikishia ujumbe wa Allah(s.w).
(xv)Hapana yeyote mwenye uwezo wa kutweza au kutengua maamuzi ya nafsi ya mwanaadamu.Wachawi walipobainikiwa na Haki na wakasilimu, Firaun hakuweza kuwaritadisha pamoja na adhabu kali aliyoitoa dhidi yao – Qir-an (26:49-51).
(xvi)Toba inayokubalika ni ile inayoletwa haraka kabla ya kufikwa na mauti – Qur-an (4:18).
(xvii)Kuishi nje ya shahada na kutarajia kufa ndani ya shahada ni muhali. Allah(s.w) ametuamrisha tuishi na shahada na tujitahidi kubakia nayo mpaka kufa kwetu– Qur-an (3:102).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1203
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Simulizi za Hadithi Audio
HISTORIA YA MTUME ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)
Zakaria(a. Soma Zaidi...
Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...
Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...
Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...
Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...
Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...
Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Hud(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa kuonesha upweke wa Allah(s. Soma Zaidi...
Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa
Soma Zaidi...
Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil
Mtume Isa(a. Soma Zaidi...