Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Kwa tabia zake njema Yusufu(a.

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)


Kwa tabia zake njema Yusufu(a.s) alipendwa sana na baba yake. Ndugu zake Yusufu(a.s) wakajawa chuki na husuda wakijadiliana kuwa;


...............Hakika Yusufu na nduguye wanapendwa sana na baba kuliko sisi, hali sisi ni kundi lenye nguvu. Hakika baba yetu yumo katika upotofu ulio wazi.(12:8)



Wakapanga njama za kumhujumu Yusufu (a.s) kwa kumuua ili mapenzi ya baba yao yawageukie wao. Wakapanga na kuazimia kuwa:



Muueni Yusufu au mtupeni nchi za mbali ili uso wa baba yenu ukuelekeeni na baada ya haya mtakuwa watu wema. (12:9)



Hatimaye wakakubaliana kumtumbukiza kisimani badala kumwua,wazo hili lilitolewa na mmoja wao ambaye angalau aliogopa kubeba dhima ya kufanya dhambi kubwa ya kuiua nafsi pasina haki. Akasema;



Msimuue Yusufu lakini mtupeni Yusufu katika(jiwe la ndani) ya kisima kirefu, watamuokota baadhi ya wasafiri, kama ninyi mnataka kufanya kitu.(12:10)



Yusufu anatumbukizwa kisimani

Kutumbukizwa Yusufu(a.s) Kisimani Pamoja na kuwa na dhamira ile mbaya ya kutaka kufanya kosa la kuua mtu asiyekuwa na hatia , wakaongeza kosa lingine la kusema uwongo. Wakasema:


........Ewe baba yetu, mbona hutuamini juu ya Yusufu, hakika sisi ni wenye kumtakia mema. Mruhusu kesho pamoja nasi atakula kwa furaha na kucheza; hakika sisi tutamlinda (12:11-12)



Ingawa mzee Ya’aquub(a.s) alionesha wasiwasi,lakini hatimaye aliwaruhusu waandamane naye. Walimtumbukiza Yusufu(a.s) kisimani kama walivyo dhamiria na wakaichukua kanzu yake na kuipakaza damu za uwongo, kisha wakamuongopea baba yao:



Ewe baba yetu! Hakika sisi tulikwenda kushindana mbio na tukamuacha Yusufu penye vyombo vyetu, basi mbwa mwitu akamla; lakini hutatuamini ingawa tunasema kweli (12:17)

Ya‘aquub(a.s.) alikuwa na mategemeo makubwa ya kupata mrithi bora atakayeendeleza kazi yake. Hata hivyo hatumwoni mzee Ya’aquub akikata tamaa kwa kufadhaika au kukufuru. Yeye akawajibu;

......



“..............Nafsi zenu zimekushawishini jambo. Basi (langu mimi ni) subira njema; na Mwenyezi Mungu ndiye aombwaye msaada kwa haya mnayoyasema” (12:18).

Hii ndio tabia ya Muislamu. Kurejea na kumtegemea zaidi Allah(s.w) afikwapo na msiba.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1180

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh 08

KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...
Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri

Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji.

Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina

Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.

Soma Zaidi...