image

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)

Pamoja na Isa(a.

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)


Pamoja na Isa(a.s) kufundisha tawhiid kwa kauli na vitendo; baada ya kuondoka kwake, mafundisho yake yalipotoshwa. Sura ya 222 ambayo ni ya mwisho katika Injili ya Barnabas inaeleza kama ifuatavyo juu ya kilichotokea baada ya Yesu kuondoka:



“Baada ya kuondoka kwa Yesu, wanafunzi wakatawanyika katika sehemu mbali mbali za Israeli na za ulimwengu. Na haki inayochukiwa na shetani, ilibughudhiwa, kama ambavyo daima inabughudhiwa na batili. Watu kadhaa waovu kwa kusingizia kuwa walikuwa wanafunzi (wa Yesu), wakahubiri kuwa Yesu alikufa na kufufuka. Na wengine wakahubiri,kwamba Yesu ni mwana wa Mungu, miogoni mwao Paulo. Lakina sisi kama nilivyoandika, tunaohubiri kwa wale wamchao Mwenyezi Mungu, tunahubiri ili waokoke siku ya mwisho na Hukumu ya Mwenyezi Mungu, Amin.”




Mafundisho ya Nabii Isa(a.s) yalipotoshwa katika maeneo yafuatayo:

(i) Imani ya Utatu


Imani ya Mungu mmoja aliyofundisha Nabii Isa (a.s) iligeuzwa na kufanywa imani ya Utatu. Mungu mmoja akagawanywa katika sehemu tatu; Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu. Hata mafundisho ya Biblia yenyewe yapo kinyume na imani hii. Rejea vifungu vifuatavyo:



“Yesu akamwambia, kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliyemwema ila mmoja ndiye Mungu.” (Marko 10:18)
“Yesu akamwambia, Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie. Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, Mungu wangu naye ni Mungu wenu.” (Yohana 20:17)

“Kwa Sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena nitakayosema.” (Yohana 10:49)



“Mungu akanena maneno haya yote akasema: Mimi Bwana Mungu wako niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi (Kutoka 20:1-3)

‘Sikiliza Ee Israeli, BWANA, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.” (Kumbukumbu la Taurat) (6:4)

Ama katika Qur-an imani hiyo inakanushwa kabisa na aya zifuatazo:


Kwa hakika wamekufuru wale waliosema: “Mwenyezi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu; (yeye ndiye wa tatu wao).” Na kama hawataacha hayo wayasemayo, kwa yakini itawakamata – wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao – adhabu iumizayo.(5:73)


(ii) Imani ya Uungu wa Yesu
Kuhusu imani juu ya Uungu wa Isa(a.s) na mama yake Qur’an inasema:

Kwa yakini wamekwisha kufuru wale waliosema: “Mwenyezi Mungu ni Masihi bin Maryamu.” Sema: “Ni nani atakayemiliki (kuzuilia) chochote mbele ya Mwenyezi Mungu kama yeye angetaka kumwangamiza Masihi mtoto wa Maryam, na mama yake na vyote vilivyomo katika ardhi na Ufalme wa mbinguni na ardhi na vilivyomo kati yake ni vya Mwenyezi Mungu (tu peke yake). Muumba apendavyo, na Mwenyezi Mungu ni muweza juu ya kila kitu. (5:17).



Masihi bin Maryamu si chochote ila ni Mtume . (Na) bila shaka Mitume wengi wamepita kabla yake. Na mamake ni mwanamke mkweli, (na) wote wawili walikuwa wakila chakula Tazama jinsi tunavyowabainishia Aya, kisha tazama jinsi wanavyogeuzwa (kuacha haki). (5:75)





(iii) Imani ya Uwana wa Mungu wa Nabii Isa(a.s)

Kuhusu itikadi ya Wakristo ya Yesu kuwa mwana wa Mungu, Qur’an inatufahamisha:

Na Mayahudi wanasema: “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;” na Wakristo wanasema: “Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu..” haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya wale walio kufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! (9:30).

Hakuwa (Nabii Issa) ila ni mja tuliyemneeemesha na tukamfanya mithali (nzuri) kwa wana wa Israili. (43:59).



(iv) Imani ya kusulubiwa Yesu Msalabani
Imani ya kufa na kufufuka Nabii Isa(a.s) ni imani ya msingi katika dini ya Ukristo. Imani hii imesimama juu ya dhana zifuatazo:
- Dhambi ya asili.
- Haja ya kuwa na Mpatanishi.
- Kafara ya damu (kifo), kwa ajili ya dhambi.



Wakristo wanaamini kuwa baada ya Adam(a.s) kumkosea Mola wake; kizazi chake chote kilirithi dhambi. Kwa hiyo kila anayezaliwa anazaliwa na dhambi. Ili salama ipatikane kwa mwanaadamu ni lazima apatikane asiye na dhambi awe mpatanishi kati ya Mungu na mwanaadamu. Mtume Isa (Yesu) anadhaniwa ndiye asiye na dhambi na mpatanishi. Lakini ili dhambi za wanadamu zioshwe imekuwa lazima damu ya Yesu imwagike. Kwa hiyo kufa Yesu msalabani ilikuwa hitajio la lazima ili wanaadamu waokolewe na dhambi. Imani hii inasonga mbele na kudai kuwa Mkristo wa leo amepunguziwa kazi. Hana haja ya kufuata sheria. Lililo wajibu juu yake ni kuamini tu kuwa yesu ni Mtoto wa Mungu na alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zake.



Lakini kuhusu dhana ya dhambi ya asili Qur-an inatufunza kuwa Nabii Adam alitubu na Mola wake akapokea toba yake.



Kisha Adam akapokea maneno (ya maombi) kwa Mola wake, (akaomba), na Mola wake Akapokea toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kupokea toba (kwa wenye kutubia) na mwingi wa kurehemu (2:37)

Ama kuhusu mtu kutolewa kafara kwa ajili ya dhambi za mtu mwingine, Biblia ina haya ya kusema:

“Lakini watoto wao hakuwaua, ila alifanya sawa sawa na alivyo amuru, akisema, mababa wasife kwa makosa ya wana, wala wana wasife kwa makosa ya mababa; lakini kila mtu atakufa kwa dhambi yake mwenyewe. (2 mambo ya nyakati 25:4)

Mababa wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya baba zao; kila mtu na auawe kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.” (Kumb, … 4:16).

“Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi, Bali kila mtu atakufa kwa Sababu ya uovu wake mwenye; kila mtu alaye zabibu kali meno yake yatakuwa ganzi.” (Yeremia: 31:29-30).


Nabii Isa(a.s) Siku ya Kiyama


Siku ya kiyama itakuwa nzito sana kwa wale waliokuwa wakiamini na kutangaza kuwa Nabii Isa(a.s) ni Mungu, na kumuabudia kinyume cha alivyofundisha. Allah(s.w) atamuuliza Nabii Isa(a.s)




Na(Kumbukeni)Mwenyezi Mungu atakaposema:“Ewe Isa bin Maryam! Je wewe uliwaambia watu ‘Nifanyeni mimi na mama yangu miungu badala ya Mwenyezi Mungu?’. Aseme: “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika. Hainistahiki mimi kusema ambayo si haki yangu. Kama ningelisema bila shaka ungelijua; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyo nafsini mwako; hakika wewe ndiwe ujuaye mambo ya ghaibu. (5:116)



Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamrisha; ya kwamba
‘Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu’. Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao; na uliponikamilishia muda wangu, Wewe ukawa mchungaji juu yao, na Wewe shahidi juu ya kila kitu. Ikiwa utawaadhibu, basi bila shaka hao ni waja wako; na ukiwasamehe basi kwa hakika wewe ndiwe mwenye nguvu na Mwenye hikima.(5:117-118)





Mwenyezi Mungu atasema: “Hii ndiyo siku ambayo wakweli utawafaa ukweli wao”. Wao watapata Bustani zipitazo mito mbele yake. humo watakaa milele. Mwenyezi Mungu amewawia radhi; nao wawe radhi naye. Huko ndiko kufaulu kukubwa(5:119)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 503


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

MAMA YAKE MTUME MUHAMMAD (S.A.W) ANAMLEA MTUME MUHAMAD AKIWA NA UMRI WA MIAKA MINNE (4)
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...

Khalifa ‘Umar bin Abdul Aziz
Soma Zaidi...

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KATIKA HARAKATI ZA KULINGANIA DINI
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Darsa za sira (maisha ya mtume jaribio la 01
Soma Zaidi...

tarekh 06
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Madhumuni ya dola ya uislamu
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s. Soma Zaidi...

tarekh 08
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)
Soma Zaidi...