image

Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo yatokanayo na Upinzani wa Maquraish dhidi ya Uislamu (Qur’an).

  1. Upinzani wa Makafiri dhidi ya ujumbe wa Uislamu upo nyakati na muda wote na hautaisha.

 

  1. Hatuna budi kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa kuanzia familia, ndugu na jamaa zetu wa karibu kabla ya wengine ili kupata wasaidizi wa karibu.

 

  1. Waislamu hawana budi kuwa tayari na kutokata tamaa katika kuusimamisha Uislamu bila ya kumchelea yeyote yule.

 

  1. Makafiri siku zote wako tayari kutumia kila mbinu na njia kuhakikisha kuwa wanabaki katika utawala na itikadi za ibada zao ili kuendeleza na kuimarisha maslahi yao kupitia unyonyaji na ukandamizaji.  

 

  1. Mbinu za Makafiri za kutaka kuuhilikisha Uislamu na waislamu zinafanana katika zama zote za historia ya maisha ya mwanaadamu.

 

  1. Mtume (s.a.w) na maswahaba wake waliweza kuhimili vitimbi vya makafiri na hatimaye kuweza kuusimamisha Uislamu katika jamii ni baada ya wao kufuata na kutekeleza kikamilifu mafunzo ya Qur’an (96:1-5), (73:1-10) na (74:1-7).

 

  1. Suala la kuulingania na kuutangaza ujumbe wa Uislamu ni zito, lenye misukosuko na gharama kubwa ya kutoa mali na nafsi (uhai).

 

  1. Siku zote makafiri na maadui wengine wa Uislamu hawakotayari kuona Uislamu unasimama katika jamii na waislamu wanautekeleza vilivyo.

 

  1. Tusitarajie matunda ya kusimama Uislamu kupatikana kwa muda mfupi na kwa urahisi, kwani linahitaji mipango ya muda mrefu na kujitoa muhanga.

 

  1. Wakati wowote Waislamu watakapojizatiti katika kuulingania na kuupigania Uislamu kwa mali na nafsi zao, Allah (s.w) atawapa nusura dhidi ya maadui wao.

Rejea Qur’an (61:8, 10-13).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 993


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad
(i) Suratul- ‘Alaq (96:1-5)“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa ‘alaq. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani
3. Soma Zaidi...

HISTORIANA MAISHA YA MTUME ISA(A.S)
Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

tarekh 3
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YA‘AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

Mikataba ya aqabah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA BANI ISRAIL
Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu
Mtume Yusufu(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUPASULIWA KWA KIFUA AU TUMBO CHA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AKIWA MTOTO KWA BI HALIMA
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...