image

MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA

Historia ya harakati za Mtume(s.

MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA

MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA

Historia ya harakati za Mtume(s.a.w) za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii yake zimegawanyika katika vipindi viwili – kipindi cha Makka na kipindi cha Madinah. Kipindi cha Makka kilichukua muda wa miaka kumi na tatu(13) kuanzia pale Mtume(s.a.w) alipoanza kupokea wahayi wa kwanza wa Qur’an mpaka alipoondoka kuhamia Madinah. Kipindi cha Madinah kilianza pale alipopokelewa Madinah na Answar mpaka mwisho wa uhai wake. Kipindi hiki kilichukua muda wa miaka kumi (10).



Mazingira ya Makka na Madinah yalikuwa tofauti. Hivyo hata mbinu za kuhuisha na kusimamisha Uislamu zilitofautiana. Pia hata mbinu za wapinzani wa Uislamu zilitofautiana.

Kuanza Kulingania kwa Siri

Baada ya Mtume(s.a.w) kupewa amri ya “simama uonye (watu)” aliamua kuanza kulingania kwa siri. Bila ya kutangaza hadharani kuwa yeye sasa ni Mtume wa Allah(s.w), alianza kumuendea mtu mmoja mmoja katika wale waliokuwa karibu naye kifamilia na kirafiki. Mtume(s.a.w) alianza kuutangaza Utume wake



kwa mkewe Khadija na watoto kisha kwa wale waliokuwa chini ya ulezi wake, ndugu yake, Ally bin Abu-Talib na huru wake, Zaid bin Harith. Baada ya hapo Mtume(s.a.w) aliwaendea rafiki na jamaa zake wa karibu na kuwafikishia ujumbe wa Utume. Miongoni mwa rafiki zake waliokuwa karibu ni Abubakar(r.a). Rafiki zake nao waliufikisha ujumbe wa Uislamu kwa familia zao na rafiki zao wa karibu kiasi kwamba ujumbe ulitambaa chini kwa chini mpaka ukaingia takriban katika kila nyumba ya wakazi wa Makka.



Katika kipindi hiki cha kufikisha ujumbe kwa siri, kilicho dumu kwa miaka mitatu, Mtume(s.a.w) alikuwa akikutana na Waislamu kwa siri katika nyumba ya Bwana Arqam bin Abi Arqam iliyojulikana kwa jina maarufu, “Darul-Arqam”.



Mtume(s.a.w) alikuwa anakutana na waumini Darul-Arqam ili kuwafundisha Uislamu na kuwapa waumini maelekezo ya namna ya kuutekeleza katika maisha ya kibinafsi na ya kijamii. Alikuwa akiwasomea aya za Qur-an alizokuwa anashushiwa kila mara na kuwaelekeza namna ya kuzitekeleza katika maisha yao ya kila siku. Kila Muislamu wakati ule aliujua Uislamu na kuutekeleza vilivyo katika maisha yake ya kila siku. Kwa mujibu wa Hadith, iliyo simuliwa na Ibn Masu’ud(r.a), kila Muislamu aliisoma Qur-an kwa lengo la kuifanya mwongozo wa maisha yake ya kila siku.



Wengi waliosilimu katika kipindi hiki cha awali walikuwa watumwa, maskini, vijana na wale wasiokuwa maarufu katika jamii. Kilichowafanya hawa watu wa mwanzo kusilimu haraka haraka bila ya kusita, ni ule ukaribu wao na Muhammad(s.a.w) ambao uliwawezesha kuifahamu vyema tabia yake tukufu. Walimfahamu kuwa alikuwa mwaminifu mno na hawakuwahi kamwe kumsikia akisema uwongo. Kwa ukweli wake na uaminifu uliopea, walimuita “As-Sadiq Al-Amin” (Mkweli Mwaminifu) hata kabla ya kutangaza ujumbe wa Uislamu. Pia, hata kabla ya kuanza kutangaza ujumbe wa Utume wake, alikuwa mpole na mwenye kuwahurumia mno wanyonge hasa watumwa na maskini. Hivyo, alipowatangazia hao rafiki zake na jamaa zake wa karibu kuwa yeye ni Mtume wa Allah, wote waliitikia wito wake wakasilimu isipokuwa wale waliokuwa na matatizo yao ya ubinafsi kama ami yake, Abu-Lahab.


Mafunzo:

Kutokana na Mtume(s.a.w) kuanza kulingania ujumbe wa Uislamu kwa siri, tunajifunza yafuatayo:

Kwanza, baada ya kuukiri Uislamu na kuutekeleza kimatendo, hatunabudi kuufikisha Uislamu huo kwa familia zetu, rafiki na jamaa zetu wa karibu. Hawa watakuwa wepesi kutusikiliza na kutufuata kwa kuwa wanatufahamu vyema. Tabia njema ni nyenzo muhimu sana.



Pili, ni muhimu kuwa wasiri na waangalifu katika hatua za mwanzo mwanzo za kuuhuisha Uislamu katika jamii ili maadui zetu wasije kutuzima kabla ujumbe haujasambaa kwa watu wengi. Baada ya miaka mitatu ya Mtume(s.a.w) kutangaza ujumbe kwa siri, takriban katika kila familia ya wakazi wa Makka palikuwa na mtu aliyesilimu.Jambo hili liliwaudhi na kuwahuzunisha sana wakuu wa jamii ya Kiquraish.



Tatu, kuujua Uislamu vilivyo kwa kila Muislamu ni jambo muhimu sana. Hata katika kipindi hiki cha kutangaza ujumbe kwa siri, Mtume(s.a.w) hakuacha kuwakusanya Waislamu kisiri siri katika kituo cha Darul-Arqam kuwafundisha Uislamu na kuwapa maelekezo ya utekelezaji wake katika maisha ya kila siku. Uislamu hautoweza kusimama katika jamii iwapo wanaojiita Waislamu watakuwa wameridhika kuishi kwa kufuata upepo kama bendera. Waislamu wa kufuata mkumbo (norminal Muslims) mara nyingi hutumiwa na maadui na kuupiga vita Uislamu na Waislamu bila kujitambua. Aidha, Waislamu wa mkumbo mara nyingi huwa rahisi kukumbwa na propoganda za maadui wa Uislamu. Vile vile Waislamu wa aina hii ni rahisi kuathiriwa na mila na desturi za makafiri.



                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 621


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)
Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza. Soma Zaidi...

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a. Soma Zaidi...

Kisa cha Israa na Miraji na kufaradhishwa swala tano
Safari ya Mi'rajKatika mwaka wa 12 B. Soma Zaidi...

Sababu za makafiri wa kiqureish kuupinga ujumbe wa uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋 Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 03
Soma Zaidi...

Vipengele vya mkataba wa Hudaibiya na faida zake katika Ukombozi (ufunguzi) wa mji wa Makkah
Soma Zaidi...

Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil
Mtume Isa(a. Soma Zaidi...

tarekh 02
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Kifo cha Khalia Uthman kilivyotokea
Soma Zaidi...

Historia ya vita vya Muta
hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISMAIL
Soma Zaidi...