(h) Kujiepusha na maringo na majivuno



Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri. Kwa mujibu wa Hadith sahihi kibri ni katika madhambi makubwa"



"Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ambaye moyoni mwake mna punje ya kibri hataingia peponi." Sahaba mmoja akauliza: "Je, kama mtu anapenda nguo nzuri na viatu?" Mtume (s. a.w) akasema, "Allah (s.w) ni mzuri na anapenda vizuri. Kibri ni kukataa ukweli na kupuuza watu." (Muslim)
Il i kuepukana na maringo na kibri Al l ah(s.w) anatutanabahisha:



"… Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa mlima." (1 7:3 7)



"Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu, akakuhuisheni; kisha atakufisheni; kisha atakuhuisheni (tena); kisha kwake mtarejeshwa." (2:28)



Aliye bora mbele ya wengine ni yule aliyewazidi katika kumcha Mwenyezi Mungu - Rejea Qur-an (49:13)