picha

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

(g) Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa


Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.
"Wala usifuate usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo vyote vitaulizwa." (17:36).



Kila mtu wa kawaida hana budi kutumia kipaji chake cha akili (moyo) na milango ya fahamu (macho, masikio, n.k.) katika kuchukua uamuzi sahihi na kufuata utaratibu wa maisha anaoridhia Allah (s.w). Na hasa kazi ya akili na kipaji cha elimu alichotunukiwa binaadamu, ni kumuwezesha kujitambua, kumtambua Mola wake na kumuabudu inavyostahiki.



Mtu atakayeishi kwa kufuata mambo kinyume na utaratibu anaoridhia Allah, ambao ni Uislamu, hatapaswa kumlaumu yeyote isipokuwa nafsi yake kwa matokeo mabaya yatakayomfika katika maisha ya dunia na akhera. Allah (s.w) anatutanabahisha juu ya hili katika aya zifuatazo:



(Wakumbushe wakati) waliofuatwa watakapowakataa wale waliowafuata, na hali ya kuwa wamekwisha kuiona adhabu, na yatakatika mafungamano yao. Na watasema wale waliofuata, "Laiti tungeweza kurudi (duniani) tukawakataa kama wanavyotukataa. "Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu atakavyowaonyesha vitendo vyao kuwa majuto yao; wala hawatakuwa wenye kutoka Motoni." (2:166-167)


Na wakasema wale waliokufuru: "Hat utaiamini Qur-an hii kabisa, wala Vile (vitabu) vilivyokuwa kabla yake." Na ungewaona madhalimu watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, wakirudishiana maneno wao kwa wao, (ungeona mambo)! Wale wanyonge watawaambia wale waliojiona wakubwa: "Kama si nyinyi bila shaka tungekuwa Waislamu." Waseme wale waliojiona wakubwa kuwaambia wale wanyonge: "Oh!Sisi tulikuzuilieni uwongofu baada ya kukufikieni? (Siyo) Bali nyinyi wenyewe mlikuwa waovu. " Na wale wanyonge waseme kuwambia wale waliojiona wakubwa: "Bali (mlikuwa mkifanya), vitimbi (hila) usiku na mchana (vya kutuzuilia tusiamini); mlipotuamuru tumkufuru Mwenyezi Mungu na tumfanyie washirika." Nao wataficha majuto watakapoiona adhabu; na Tutaweka makongwa shingoni mwa wale waliokufuru; kwani wanalipwa mengine ila yale waliyokuwa wakiyatenda?" (34:31-33)


"Na (wakumbushe) watakapobishana katika Moto huo - wakati madhaifu watakapowaambia wale waliojitukuza: "Kwa yakini sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, mnaweza kutuondolea sehemu kidogo ya Moto?" Waseme wale waliokuwa wakijitukuza: "Sisi sote tumo humu; Mwenyezi Mungu amekwishahukumu baina ya viumbe; (na tumekwishastahiki Moto, hatuna la kufanya." Na wale waliomo Motoni watawaambia walinzi wa Jahanamu; "Muombeni Mola wenu atupunguzie (alau) siku moja ya adhabu." (Walinzi) wawaambie: "Je, hawakuwa wakikujieni Mitume wenu kwa hoja zilizowazi?" Waseme: "Kwa nini? (Wakitujia lakini tuliasi)" Wawaambie: "Basi ombeni; na madua ya makafiri hayawi ila ni ya kupotea bure." (40:47-50)





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1164

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 web hosting    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali

Wakatibmeingibe Allah anapotaka kuwasiliana na wanadamu hutuma Malaika wake.

Soma Zaidi...
Lengo la kuletwa mitume

Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere..

Soma Zaidi...
Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi

Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.

Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Soma Zaidi...