Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

(g) Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa


Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.
"Wala usifuate usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo vyote vitaulizwa." (17:36).



Kila mtu wa kawaida hana budi kutumia kipaji chake cha akili (moyo) na milango ya fahamu (macho, masikio, n.k.) katika kuchukua uamuzi sahihi na kufuata utaratibu wa maisha anaoridhia Allah (s.w). Na hasa kazi ya akili na kipaji cha elimu alichotunukiwa binaadamu, ni kumuwezesha kujitambua, kumtambua Mola wake na kumuabudu inavyostahiki.



Mtu atakayeishi kwa kufuata mambo kinyume na utaratibu anaoridhia Allah, ambao ni Uislamu, hatapaswa kumlaumu yeyote isipokuwa nafsi yake kwa matokeo mabaya yatakayomfika katika maisha ya dunia na akhera. Allah (s.w) anatutanabahisha juu ya hili katika aya zifuatazo:



(Wakumbushe wakati) waliofuatwa watakapowakataa wale waliowafuata, na hali ya kuwa wamekwisha kuiona adhabu, na yatakatika mafungamano yao. Na watasema wale waliofuata, "Laiti tungeweza kurudi (duniani) tukawakataa kama wanavyotukataa. "Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu atakavyowaonyesha vitendo vyao kuwa majuto yao; wala hawatakuwa wenye kutoka Motoni." (2:166-167)


Na wakasema wale waliokufuru: "Hat utaiamini Qur-an hii kabisa, wala Vile (vitabu) vilivyokuwa kabla yake." Na ungewaona madhalimu watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, wakirudishiana maneno wao kwa wao, (ungeona mambo)! Wale wanyonge watawaambia wale waliojiona wakubwa: "Kama si nyinyi bila shaka tungekuwa Waislamu." Waseme wale waliojiona wakubwa kuwaambia wale wanyonge: "Oh!Sisi tulikuzuilieni uwongofu baada ya kukufikieni? (Siyo) Bali nyinyi wenyewe mlikuwa waovu. " Na wale wanyonge waseme kuwambia wale waliojiona wakubwa: "Bali (mlikuwa mkifanya), vitimbi (hila) usiku na mchana (vya kutuzuilia tusiamini); mlipotuamuru tumkufuru Mwenyezi Mungu na tumfanyie washirika." Nao wataficha majuto watakapoiona adhabu; na Tutaweka makongwa shingoni mwa wale waliokufuru; kwani wanalipwa mengine ila yale waliyokuwa wakiyatenda?" (34:31-33)


"Na (wakumbushe) watakapobishana katika Moto huo - wakati madhaifu watakapowaambia wale waliojitukuza: "Kwa yakini sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, mnaweza kutuondolea sehemu kidogo ya Moto?" Waseme wale waliokuwa wakijitukuza: "Sisi sote tumo humu; Mwenyezi Mungu amekwishahukumu baina ya viumbe; (na tumekwishastahiki Moto, hatuna la kufanya." Na wale waliomo Motoni watawaambia walinzi wa Jahanamu; "Muombeni Mola wenu atupunguzie (alau) siku moja ya adhabu." (Walinzi) wawaambie: "Je, hawakuwa wakikujieni Mitume wenu kwa hoja zilizowazi?" Waseme: "Kwa nini? (Wakitujia lakini tuliasi)" Wawaambie: "Basi ombeni; na madua ya makafiri hayawi ila ni ya kupotea bure." (40:47-50)





                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 740

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat

"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.

Soma Zaidi...
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.

Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...
Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?

Soma Zaidi...