Navigation Menu



image

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

(g) Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa


Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.
"Wala usifuate usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo vyote vitaulizwa." (17:36).



Kila mtu wa kawaida hana budi kutumia kipaji chake cha akili (moyo) na milango ya fahamu (macho, masikio, n.k.) katika kuchukua uamuzi sahihi na kufuata utaratibu wa maisha anaoridhia Allah (s.w). Na hasa kazi ya akili na kipaji cha elimu alichotunukiwa binaadamu, ni kumuwezesha kujitambua, kumtambua Mola wake na kumuabudu inavyostahiki.



Mtu atakayeishi kwa kufuata mambo kinyume na utaratibu anaoridhia Allah, ambao ni Uislamu, hatapaswa kumlaumu yeyote isipokuwa nafsi yake kwa matokeo mabaya yatakayomfika katika maisha ya dunia na akhera. Allah (s.w) anatutanabahisha juu ya hili katika aya zifuatazo:



(Wakumbushe wakati) waliofuatwa watakapowakataa wale waliowafuata, na hali ya kuwa wamekwisha kuiona adhabu, na yatakatika mafungamano yao. Na watasema wale waliofuata, "Laiti tungeweza kurudi (duniani) tukawakataa kama wanavyotukataa. "Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu atakavyowaonyesha vitendo vyao kuwa majuto yao; wala hawatakuwa wenye kutoka Motoni." (2:166-167)


Na wakasema wale waliokufuru: "Hat utaiamini Qur-an hii kabisa, wala Vile (vitabu) vilivyokuwa kabla yake." Na ungewaona madhalimu watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, wakirudishiana maneno wao kwa wao, (ungeona mambo)! Wale wanyonge watawaambia wale waliojiona wakubwa: "Kama si nyinyi bila shaka tungekuwa Waislamu." Waseme wale waliojiona wakubwa kuwaambia wale wanyonge: "Oh!Sisi tulikuzuilieni uwongofu baada ya kukufikieni? (Siyo) Bali nyinyi wenyewe mlikuwa waovu. " Na wale wanyonge waseme kuwambia wale waliojiona wakubwa: "Bali (mlikuwa mkifanya), vitimbi (hila) usiku na mchana (vya kutuzuilia tusiamini); mlipotuamuru tumkufuru Mwenyezi Mungu na tumfanyie washirika." Nao wataficha majuto watakapoiona adhabu; na Tutaweka makongwa shingoni mwa wale waliokufuru; kwani wanalipwa mengine ila yale waliyokuwa wakiyatenda?" (34:31-33)


"Na (wakumbushe) watakapobishana katika Moto huo - wakati madhaifu watakapowaambia wale waliojitukuza: "Kwa yakini sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, mnaweza kutuondolea sehemu kidogo ya Moto?" Waseme wale waliokuwa wakijitukuza: "Sisi sote tumo humu; Mwenyezi Mungu amekwishahukumu baina ya viumbe; (na tumekwishastahiki Moto, hatuna la kufanya." Na wale waliomo Motoni watawaambia walinzi wa Jahanamu; "Muombeni Mola wenu atupunguzie (alau) siku moja ya adhabu." (Walinzi) wawaambie: "Je, hawakuwa wakikujieni Mitume wenu kwa hoja zilizowazi?" Waseme: "Kwa nini? (Wakitujia lakini tuliasi)" Wawaambie: "Basi ombeni; na madua ya makafiri hayawi ila ni ya kupotea bure." (40:47-50)





                   







           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 534


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad
Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Soma Zaidi...

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s. Soma Zaidi...

SIFA ZA WAUMINI
Soma Zaidi...

Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.
Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini. Soma Zaidi...

ENYI WAJA WANGU NIMEIKATAZA NAFSI YANGU DHULMA
Soma Zaidi...

Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6). Soma Zaidi...

(b)Umbile la Mwanaadamu ni la kidini
Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini. Soma Zaidi...

Sababu za kutokubalika kwa vitabu vilivyotumwa kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu zama hizi
Soma Zaidi...

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Maana ya Kumuamini Allah (s.w) katika Utendaji wa kila siku
Soma Zaidi...

mitume
Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...