Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.

Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

(d) Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji



Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.w). Kina cha Uovu wa tendo hili la kuwasingizia uzinifu watu watwahirifu kinadhihirishwa na adhabu kali inayotolewa dhidi ya wazushi hawa:


β€œNa wale wanaowasingizia wanawake watahirifu (kuwa wamezini), kisha hawaleti mashahidi wanne, basi wapigeni mijeledi, (bakora) thamanini, na msiwakubalie ushahidi wao tena, na hao ndio mafasiki." (24:4)



"Bila shaka wale wanaowasingizia wanawake waliotakasika wasiojua (maovu), Waislamu; (wenye kuwasingizia watu hawa) wamelaaniwa katika dunia na akhera; nao watapata adhabu kubwa."



β€œSiku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao, kwa yale waliyokuwa wakiyafanya."
β€œSiku hiyo Mwenyezi Mungu Atawapa sawasawa malipo yao ya haki, na watajua kwamba Mwenyezi Mungu ndiye (Mwenye kulipa kwa) haki iliyo dhahiri."
(24:23-2 5)



Pia aya ifuatayo inakemea kwa ujumla juu ya tabia mbaya ya kuwasingizia (kuwazulia) watu wema kuwa wamefanya uovu, ili tu kuwadhalilisha na kuwaaibisha mbele ya jamii:


β€œKwa yakini wale wannnaopenda uenee uovu kwa wale walioamini, watapata adhabu iumizayo katika dunia na akhera; na Mwenyezi Mungu ndiye Anayejua; na nyinyi hamjui." (24:19)



Jambo la kuwasingizia uovu watu wema ni ovu mno mbele ya Allah (s.w) kwa sababu ndiyo silaha wanayotumia wanafiki na washirika wao katika kudhoofisha Uislamu kwa kuwakatisha tamaa wanaharakati na kuisambaratisha jamii ya Waislamu kwa ujumla. Katika historia ya Uislamu, wakati wa Mtume (s.a.w) silaha hii waliitumia wanafiki wakiongozwa na mkubwa wao Abdulllah bin Ubayy, walipomsingizia Bi Aisha (r.a), mkewe Mtume (s.a.w), kuwa amezini na Swafan bin Mu'attal Sulami, miongoni mwa maswahaba wema aliyeshiriki katika vita vya Badr. Allah (s.w) aliwatakasa waja wake hawa na uzushi wa wanafiki kwa kushusha Sura hii hasa katika aya zifuatazo:


Hakika wale walioleta uwongo huo (wa kumsingizia Bibi Aisha - mkewe Mtume -kuwa amezini) ni kundi miongoni mwenu, (ni jamaa zenu). Msifikiri ni shari kwenu, bali hiyo ni heri kwenu. Kila mtu katika wao atapata aliyoyachuma katika madhambi hayo. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao, atapata adhabu kubwa (zaidi)
Mbona mliposikia (habari) hii, wanaume Waislamu na wanawake Waislamu hawakuwadhania wenzao mema, na kusema "huu ni uzushi dhahiri?"



Mbona hawakuleta mashahidi wanne? Na walipokosa kuleta mashahidi, basi hao mbele ya Mwenyezi Mungu ni waongo.
Na kama isingalikuwa juu yenu fadhila ya Mwenyezi Mungu na rehema Yake katika dunia na akhera, bila shaka ingalikupateni adhabu kubwa kwa sababu ya yale mliyoyashughulikia.



Mlipoupokea (uwongo huo mkawa mnautangaza) kwa ndimi zenu na mkasema kwa vinywa vyenu msiyoyajua, na mlifikiri ni jambo dogo, kumbe mbele ya Mwenyezi Mungu ni kubwa. Na mbona, mliposikia, hamkusema: "Haitujazii kuzungumza haya: Utakatifu ni Wako (Mola wetu!) Huu ni uwongo mkubwa." Mwenyezi Mungu Anakunasihini msirudie kabisa kufanya mfano wa haya, ikiwa nyinyi ni Waislamu kweli. Na Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya (zake); na Mwenyezi Mungu ndiye Ajuaye, Mwenye hikima.' (24:11-1 8)



Kutokana na aya hizi tunajifunza yafuatayo:


(i) Waumini watakaposikia habari za uzushi dhidi ya watu wema,wasizikubali bali wadai ushahidi ulio wazi unaothibitisha tuhuma hizo.
(ii)Wazushi wakishindwa kuleta ushahidi, wachukuliwe moja kwa moja kuwa ni waongo na Waislamu wote wawe dhidi yao na kuwepo adhabu inayostahiki.
(iii)Ni marufuku kwa waumini kudaka na kutangaza mambo ya uzushi dhidi ya watu wema ambayo hawana hakika nayo. Katika kusisitiza hili Allah anatuasa:
β€œEnyi mlioamini! Kama fasiki, (asiyekuwa wa kutegemewa) akikujieni na habari (yoyote ile msimkubalie tu) bali pelelezeni (kwanza), msije mkawadhuru watu kwa ujahili na mkawa wenye kujuta juu ya yale mliyoyatenda. ”(49:6)
(iv)Waislamu wanahimizwa wajenge tabia ya kuwa na dhana njema juu ya waumini wenzao kuwa haiwezekani kwa muumini kufanya tendo hilo chafu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 625

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu)

Soma Zaidi...
Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Soma Zaidi...
SHIRK

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali

Wakatibmeingibe Allah anapotaka kuwasiliana na wanadamu hutuma Malaika wake.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...