image

Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.

Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

(d) Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji



Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.w). Kina cha Uovu wa tendo hili la kuwasingizia uzinifu watu watwahirifu kinadhihirishwa na adhabu kali inayotolewa dhidi ya wazushi hawa:


“Na wale wanaowasingizia wanawake watahirifu (kuwa wamezini), kisha hawaleti mashahidi wanne, basi wapigeni mijeledi, (bakora) thamanini, na msiwakubalie ushahidi wao tena, na hao ndio mafasiki." (24:4)



"Bila shaka wale wanaowasingizia wanawake waliotakasika wasiojua (maovu), Waislamu; (wenye kuwasingizia watu hawa) wamelaaniwa katika dunia na akhera; nao watapata adhabu kubwa."



“Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao, kwa yale waliyokuwa wakiyafanya."
“Siku hiyo Mwenyezi Mungu Atawapa sawasawa malipo yao ya haki, na watajua kwamba Mwenyezi Mungu ndiye (Mwenye kulipa kwa) haki iliyo dhahiri."
(24:23-2 5)



Pia aya ifuatayo inakemea kwa ujumla juu ya tabia mbaya ya kuwasingizia (kuwazulia) watu wema kuwa wamefanya uovu, ili tu kuwadhalilisha na kuwaaibisha mbele ya jamii:


“Kwa yakini wale wannnaopenda uenee uovu kwa wale walioamini, watapata adhabu iumizayo katika dunia na akhera; na Mwenyezi Mungu ndiye Anayejua; na nyinyi hamjui." (24:19)



Jambo la kuwasingizia uovu watu wema ni ovu mno mbele ya Allah (s.w) kwa sababu ndiyo silaha wanayotumia wanafiki na washirika wao katika kudhoofisha Uislamu kwa kuwakatisha tamaa wanaharakati na kuisambaratisha jamii ya Waislamu kwa ujumla. Katika historia ya Uislamu, wakati wa Mtume (s.a.w) silaha hii waliitumia wanafiki wakiongozwa na mkubwa wao Abdulllah bin Ubayy, walipomsingizia Bi Aisha (r.a), mkewe Mtume (s.a.w), kuwa amezini na Swafan bin Mu'attal Sulami, miongoni mwa maswahaba wema aliyeshiriki katika vita vya Badr. Allah (s.w) aliwatakasa waja wake hawa na uzushi wa wanafiki kwa kushusha Sura hii hasa katika aya zifuatazo:


Hakika wale walioleta uwongo huo (wa kumsingizia Bibi Aisha - mkewe Mtume -kuwa amezini) ni kundi miongoni mwenu, (ni jamaa zenu). Msifikiri ni shari kwenu, bali hiyo ni heri kwenu. Kila mtu katika wao atapata aliyoyachuma katika madhambi hayo. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao, atapata adhabu kubwa (zaidi)
Mbona mliposikia (habari) hii, wanaume Waislamu na wanawake Waislamu hawakuwadhania wenzao mema, na kusema "huu ni uzushi dhahiri?"



Mbona hawakuleta mashahidi wanne? Na walipokosa kuleta mashahidi, basi hao mbele ya Mwenyezi Mungu ni waongo.
Na kama isingalikuwa juu yenu fadhila ya Mwenyezi Mungu na rehema Yake katika dunia na akhera, bila shaka ingalikupateni adhabu kubwa kwa sababu ya yale mliyoyashughulikia.



Mlipoupokea (uwongo huo mkawa mnautangaza) kwa ndimi zenu na mkasema kwa vinywa vyenu msiyoyajua, na mlifikiri ni jambo dogo, kumbe mbele ya Mwenyezi Mungu ni kubwa. Na mbona, mliposikia, hamkusema: "Haitujazii kuzungumza haya: Utakatifu ni Wako (Mola wetu!) Huu ni uwongo mkubwa." Mwenyezi Mungu Anakunasihini msirudie kabisa kufanya mfano wa haya, ikiwa nyinyi ni Waislamu kweli. Na Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya (zake); na Mwenyezi Mungu ndiye Ajuaye, Mwenye hikima.' (24:11-1 8)



Kutokana na aya hizi tunajifunza yafuatayo:


(i) Waumini watakaposikia habari za uzushi dhidi ya watu wema,wasizikubali bali wadai ushahidi ulio wazi unaothibitisha tuhuma hizo.
(ii)Wazushi wakishindwa kuleta ushahidi, wachukuliwe moja kwa moja kuwa ni waongo na Waislamu wote wawe dhidi yao na kuwepo adhabu inayostahiki.
(iii)Ni marufuku kwa waumini kudaka na kutangaza mambo ya uzushi dhidi ya watu wema ambayo hawana hakika nayo. Katika kusisitiza hili Allah anatuasa:
“Enyi mlioamini! Kama fasiki, (asiyekuwa wa kutegemewa) akikujieni na habari (yoyote ile msimkubalie tu) bali pelelezeni (kwanza), msije mkawadhuru watu kwa ujahili na mkawa wenye kujuta juu ya yale mliyoyatenda. ”(49:6)
(iv)Waislamu wanahimizwa wajenge tabia ya kuwa na dhana njema juu ya waumini wenzao kuwa haiwezekani kwa muumini kufanya tendo hilo chafu.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 203


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...

Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.
Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini. Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. Soma Zaidi...

Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.
Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu. Soma Zaidi...

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad
Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah
Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo Soma Zaidi...

“Allah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakaye”
Soma Zaidi...

NGUZO ZA IMANI
Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s. Soma Zaidi...

Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali
Wakatibmeingibe Allah anapotaka kuwasiliana na wanadamu hutuma Malaika wake. Soma Zaidi...

Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi
Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi. Soma Zaidi...

ENYI WAJA WANGU NIMEIKATAZA NAFSI YANGU DHULMA
Soma Zaidi...