image

DUA YA 1 - 10

1.

DUA YA 1 - 10


1.Dhikri ya kuleta wakati wa kuamka kutoka usingizini Mtume (s.a.w) alipoamka kutoka usingizini alikuwa akisema: Al-hamdulillahilladhy ahyaanaa ba'adamaa amaatanaa wailayhi nnushuuru" “Sifa zote njema anastahiki Allah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na ni kwake tu ufufuo." Mtume (s.a.w) amesema: "atakaye amka usiku kisha akasema: Laailahaillallaahu wah-dahu laa shariika lahu, lahulmulku walahul-hamdu wahuwa a'laa kulli shay-in qadiiru, “Hapana Mola ila Allah, Mpweke asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema, ni muweza juu ya kila kitu; Kisha akasema "Rabbigh-fir-ly" “Ee, Mola nisamehe" Basi atasamehewa. Na kama atasimama akaenda kutawadha kisha akaswali basi swala yake itakubaliwa."

2.Dhikri ya kuleta wakati wa kuvaa nguo Al-hamdulillaahi lladhy kasaany hadha (thawba) warazaqaniihi min ghairi hawlin minny walaaquwwat" "Sifa zote njema ni za Allah ambaye amenivisha nguo hii na kuniruzuku pasina uwezo wala nguvu kutoka kwangu."

3.Dua ya Kuvua Nguo "Bismillah" "Kwa jina la Allah (nina vua)."

4.Dua ya Kuingilia Chooni Muislamu akiingia chooni atangulize mguu wa kushoto na kusema: (Bismillah) “Allahumma inni a'uudhubika minal-khubuth wal-khabaaithi" (Kwa jina na Allah). Ee, Allah najikinga kwako na maovu yote na wafanya maovu"

5.Dua ya Kutoka Chooni Muislamu akitoka chooni hutanguliza mguu wa kulia na kusema: “Ghuf-raanaka" “Nakuomba msamaha (Ee Allah)

6.Dhikri wakati wa kutoka Nyumbani Bismillahi tawakkal-tu 'alallaahi walaahawla walaaquwwata illaabillaahi Kwa jina la Allah, ninajitegemeza kwa Allah, na hapana uwezo wala nguvu ila vyote vinatokana na Allah"

7.Dhikri wakati wa kurejea nyumbani Bismillahi walaj-naa, wabismillaah kharaj-naa wa'alaa Rabanaa tawakkal-naa. “Kwa jina la Allah tunaingia na kwa jina la Allah tunatoka, na kwa Mola wetu tunategemea."

8.8.Dua ya Kuingia Msikitini Tukiingia msikitini tunatanguliza mguu wa kulia na kusema: “A'udhubillaahil-'adhiim wabiwajhi-hil-kariim. 'Wasul-Twaanihil-qadiimi minash-shaytwaanir rajiim Bismillaah wasw-swallatu wassalaam a’laa rasuulillah , Allaahummaf-tahaly ab-waaba rah-matika". “Najikinga kwa Allah aliye mtukufu, na kwa uso wake mtukufu, na kwa utawala wake wa kale, kutokana na sheitwani aliyeepushwa na rehema za Allah,Kwa jina la Allah na Rehma na Amani ziwafikie Mtume wa Allah Ee! Allah nifungulie milango ya rehema zako."

9.9.Dua ya kutoka Msikitini Tukitoka msikitini tunatanguliza mguu wa kushoto na kusema: “Bismillahir wasw-swalaatu was-salaamu 'alaa rasuulillaahi, Allaahumma inny as-aluka min fadh-lika, Allaahumma A'iswimniy, minash-shaytwaanir-rajiimi." “Kwa jina la Allah na rehema na amani zimfikie Mtume wa Allah; Ee! Allah,nakuomba katika fadhila zako, Ee! Allah nilinde kutokana na shetani aliyeepushwa na rehema zako (aliye laaniwa)."

10.Dhikri za Kuleta Asubuhi na Jioni “Allahumma 'aafiniy fiy badaniy,Allahumma 'aafiniy fiy sam-'iy. Allahumma 'aafiniy fiy baswariy,Laailaha illaa anta. (Mara tatu) Ee! Allah nipe afya ya mwili wangu,Ee! Allah nipe afya ya usikivu wangu (masikio yangu),Ee! Allah nipe afya ya uoni wangu (macho yangu). Hapana Mola ila wewe (mara tatu).


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 430


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s. Soma Zaidi...

Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini
Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s. Soma Zaidi...

Mambo muhimu anayofanyiwa muislamu kabla ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mazingatio kabla ya kuosha maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nguzo za imani
Zifuatazo Ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah
Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Soma Zaidi...

Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?
Soma Zaidi...

KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi
Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi. Soma Zaidi...

Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah
Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu Soma Zaidi...

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ... Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...