DUA YA 1 - 10

1.

DUA YA 1 - 10


1.Dhikri ya kuleta wakati wa kuamka kutoka usingizini Mtume (s.a.w) alipoamka kutoka usingizini alikuwa akisema: Al-hamdulillahilladhy ahyaanaa ba'adamaa amaatanaa wailayhi nnushuuru" โ€œSifa zote njema anastahiki Allah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na ni kwake tu ufufuo." Mtume (s.a.w) amesema: "atakaye amka usiku kisha akasema: Laailahaillallaahu wah-dahu laa shariika lahu, lahulmulku walahul-hamdu wahuwa a'laa kulli shay-in qadiiru, โ€œHapana Mola ila Allah, Mpweke asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema, ni muweza juu ya kila kitu; Kisha akasema "Rabbigh-fir-ly" โ€œEe, Mola nisamehe" Basi atasamehewa. Na kama atasimama akaenda kutawadha kisha akaswali basi swala yake itakubaliwa."

2.Dhikri ya kuleta wakati wa kuvaa nguo Al-hamdulillaahi lladhy kasaany hadha (thawba) warazaqaniihi min ghairi hawlin minny walaaquwwat" "Sifa zote njema ni za Allah ambaye amenivisha nguo hii na kuniruzuku pasina uwezo wala nguvu kutoka kwangu."

3.Dua ya Kuvua Nguo "Bismillah" "Kwa jina la Allah (nina vua)."

4.Dua ya Kuingilia Chooni Muislamu akiingia chooni atangulize mguu wa kushoto na kusema: (Bismillah) โ€œAllahumma inni a'uudhubika minal-khubuth wal-khabaaithi" (Kwa jina na Allah). Ee, Allah najikinga kwako na maovu yote na wafanya maovu"

5.Dua ya Kutoka Chooni Muislamu akitoka chooni hutanguliza mguu wa kulia na kusema: โ€œGhuf-raanaka" โ€œNakuomba msamaha (Ee Allah)

6.Dhikri wakati wa kutoka Nyumbani Bismillahi tawakkal-tu 'alallaahi walaahawla walaaquwwata illaabillaahi Kwa jina la Allah, ninajitegemeza kwa Allah, na hapana uwezo wala nguvu ila vyote vinatokana na Allah"

7.Dhikri wakati wa kurejea nyumbani Bismillahi walaj-naa, wabismillaah kharaj-naa wa'alaa Rabanaa tawakkal-naa. โ€œKwa jina la Allah tunaingia na kwa jina la Allah tunatoka, na kwa Mola wetu tunategemea."

8.8.Dua ya Kuingia Msikitini Tukiingia msikitini tunatanguliza mguu wa kulia na kusema: โ€œA'udhubillaahil-'adhiim wabiwajhi-hil-kariim. 'Wasul-Twaanihil-qadiimi minash-shaytwaanir rajiim Bismillaah wasw-swallatu wassalaam aโ€™laa rasuulillah , Allaahummaf-tahaly ab-waaba rah-matika". โ€œNajikinga kwa Allah aliye mtukufu, na kwa uso wake mtukufu, na kwa utawala wake wa kale, kutokana na sheitwani aliyeepushwa na rehema za Allah,Kwa jina la Allah na Rehma na Amani ziwafikie Mtume wa Allah Ee! Allah nifungulie milango ya rehema zako."

9.9.Dua ya kutoka Msikitini Tukitoka msikitini tunatanguliza mguu wa kushoto na kusema: โ€œBismillahir wasw-swalaatu was-salaamu 'alaa rasuulillaahi, Allaahumma inny as-aluka min fadh-lika, Allaahumma A'iswimniy, minash-shaytwaanir-rajiimi." โ€œKwa jina la Allah na rehema na amani zimfikie Mtume wa Allah; Ee! Allah,nakuomba katika fadhila zako, Ee! Allah nilinde kutokana na shetani aliyeepushwa na rehema zako (aliye laaniwa)."

10.Dhikri za Kuleta Asubuhi na Jioni โ€œAllahumma 'aafiniy fiy badaniy,Allahumma 'aafiniy fiy sam-'iy. Allahumma 'aafiniy fiy baswariy,Laailaha illaa anta. (Mara tatu) Ee! Allah nipe afya ya mwili wangu,Ee! Allah nipe afya ya usikivu wangu (masikio yangu),Ee! Allah nipe afya ya uoni wangu (macho yangu). Hapana Mola ila wewe (mara tatu).


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1773

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Soma Zaidi...
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽู†ูŽู‘ ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ู…ูŽู†ู’ ูƒูŽุงู†ูŽ ูŠูุคู’ู…ูู†ู ุจูุงูŽู„ู„ูŽู‘ู‡ู ูˆูŽุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ู...

Soma Zaidi...
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

ุนูŽู†ู’ ุนูู…ูŽุฑูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽูŠู’ุถู‹ุง ู‚ูŽุงู„ูŽ: " ุจูŽูŠู’ู†ูŽู…ูŽุง ู†ูŽุญู’ู†ู ุฌูู„ููˆุณูŒ ุนูู†ู’ุฏูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุฐูŽุงุชูŽ ูŠูŽูˆู’ู…ูุŒ ุฅุฐู’ ?...

Soma Zaidi...
Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...