Menu



DUA YA 1 - 10

1.

DUA YA 1 - 10


1.Dhikri ya kuleta wakati wa kuamka kutoka usingizini Mtume (s.a.w) alipoamka kutoka usingizini alikuwa akisema: Al-hamdulillahilladhy ahyaanaa ba'adamaa amaatanaa wailayhi nnushuuru" “Sifa zote njema anastahiki Allah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha na ni kwake tu ufufuo." Mtume (s.a.w) amesema: "atakaye amka usiku kisha akasema: Laailahaillallaahu wah-dahu laa shariika lahu, lahulmulku walahul-hamdu wahuwa a'laa kulli shay-in qadiiru, “Hapana Mola ila Allah, Mpweke asiye na mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema, ni muweza juu ya kila kitu; Kisha akasema "Rabbigh-fir-ly" “Ee, Mola nisamehe" Basi atasamehewa. Na kama atasimama akaenda kutawadha kisha akaswali basi swala yake itakubaliwa."

2.Dhikri ya kuleta wakati wa kuvaa nguo Al-hamdulillaahi lladhy kasaany hadha (thawba) warazaqaniihi min ghairi hawlin minny walaaquwwat" "Sifa zote njema ni za Allah ambaye amenivisha nguo hii na kuniruzuku pasina uwezo wala nguvu kutoka kwangu."

3.Dua ya Kuvua Nguo "Bismillah" "Kwa jina la Allah (nina vua)."

4.Dua ya Kuingilia Chooni Muislamu akiingia chooni atangulize mguu wa kushoto na kusema: (Bismillah) “Allahumma inni a'uudhubika minal-khubuth wal-khabaaithi" (Kwa jina na Allah). Ee, Allah najikinga kwako na maovu yote na wafanya maovu"

5.Dua ya Kutoka Chooni Muislamu akitoka chooni hutanguliza mguu wa kulia na kusema: “Ghuf-raanaka" “Nakuomba msamaha (Ee Allah)

6.Dhikri wakati wa kutoka Nyumbani Bismillahi tawakkal-tu 'alallaahi walaahawla walaaquwwata illaabillaahi Kwa jina la Allah, ninajitegemeza kwa Allah, na hapana uwezo wala nguvu ila vyote vinatokana na Allah"

7.Dhikri wakati wa kurejea nyumbani Bismillahi walaj-naa, wabismillaah kharaj-naa wa'alaa Rabanaa tawakkal-naa. “Kwa jina la Allah tunaingia na kwa jina la Allah tunatoka, na kwa Mola wetu tunategemea."

8.8.Dua ya Kuingia Msikitini Tukiingia msikitini tunatanguliza mguu wa kulia na kusema: “A'udhubillaahil-'adhiim wabiwajhi-hil-kariim. 'Wasul-Twaanihil-qadiimi minash-shaytwaanir rajiim Bismillaah wasw-swallatu wassalaam a’laa rasuulillah , Allaahummaf-tahaly ab-waaba rah-matika". “Najikinga kwa Allah aliye mtukufu, na kwa uso wake mtukufu, na kwa utawala wake wa kale, kutokana na sheitwani aliyeepushwa na rehema za Allah,Kwa jina la Allah na Rehma na Amani ziwafikie Mtume wa Allah Ee! Allah nifungulie milango ya rehema zako."

9.9.Dua ya kutoka Msikitini Tukitoka msikitini tunatanguliza mguu wa kushoto na kusema: “Bismillahir wasw-swalaatu was-salaamu 'alaa rasuulillaahi, Allaahumma inny as-aluka min fadh-lika, Allaahumma A'iswimniy, minash-shaytwaanir-rajiimi." “Kwa jina la Allah na rehema na amani zimfikie Mtume wa Allah; Ee! Allah,nakuomba katika fadhila zako, Ee! Allah nilinde kutokana na shetani aliyeepushwa na rehema zako (aliye laaniwa)."

10.Dhikri za Kuleta Asubuhi na Jioni “Allahumma 'aafiniy fiy badaniy,Allahumma 'aafiniy fiy sam-'iy. Allahumma 'aafiniy fiy baswariy,Laailaha illaa anta. (Mara tatu) Ee! Allah nipe afya ya mwili wangu,Ee! Allah nipe afya ya usikivu wangu (masikio yangu),Ee! Allah nipe afya ya uoni wangu (macho yangu). Hapana Mola ila wewe (mara tatu).


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 981

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa Elimu Usiokubalika katika uislamu.

Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu.

Soma Zaidi...
Maana ya uislamu.

Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Soma Zaidi...