picha

Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.

Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.

Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.

(a) Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.



Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.w) amelikataza si tu kulitenda, bali hata kulikurubia.
“Wala msikaribie zinaa. Hakika hiyo ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa) ". (1 7:32)



Watakao kiuka amri hii ya Allah (s.w), jamii ya Waislamu inalazimika kuwaadhibu wawili hao kwa adhabu iliyo sawa sawa kama inavyo bainishwa katika aya (24:2)



"Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamume, mpigeni kila mmoja katika wao mijeledi (bakora) mia. Wala isiwashike kwa ajili yao huruma katika (kupitisha) hukumu hii ya Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi mnamuamini. Na lishuhudie adhabu yao (hii) kundi la waumini" (24:2)



Adhabu hii ni kwa wale ambao hawajaoa au hawajaolewa. Adhabu ya wazinifu ambao wameoa au kuolewa ni kurujumiwa (kupigwa kwa mawe) mpaka wafe kama tunavyojifunza katika Hadithi.



“Omar (r.a) amesimulia: "Hakika Allah (s.w) alimtuma Muhammad kwa haki, alimshushia kitabu (Qur'an). Katika aya alizoshusha Allah (s.w) palikuwa na aya ya kupiga mawe (wazinifu) mpaka wafe. Mtume wa Allah alihukumu kupigwa mawe (wazinifu) mpaka kufa na baada yake pia tuliwahukumu (Wazinifu) kupigwa mawe mpaka kufa. Na hukumu ya kupigwa mawe mpaka kufa katika kitabu cha Allah ni jambo la haki dhidi ya wanaume na wanawake waliozini wakiwa wameoa/wameolewa baada ya ushahidi kukamilika au baada ya kupata ujauzito au baada ya kukiri kufanya kitendo hicho" (Bukhari na Muslimu)


Jabir (r.a) ameeleza kuwa mtu alizini na mwanamke. Mtume (s.a.w) akapitisha hukumu dhidi yake na akachapwa viboko stahiki (100). Baadaye Mtume (s.a.w) alifahamishwa kuwa mtu yule alikuwa ameoa. Hivyo, Mtume (s.a.w) alipitisha hukumu stahiki dhidi yake na akapigwa mawe mpaka kufa" (Abu Daud)



Zinaa ni tendo la jimai lililofanywa baina ya mume na mke nje ya ndoa. Katika Uislamu na katika maadili mema ya kibinaadamu hapana ndoa inayokubalika baina ya jinsia moja, yaani ndoa ya mume kwa mume (ubasha) au mke kwa mke (usagaji). Pamoja na uovu wa zinaa, jimai baina ya jinsia moja, yaani Ubasha na Usagaji ni uovu uliokithiri. Watu waovu katika kaumu ya Nabii Lut (s.a) ikiwa ni pamoja na mkewe, waliangamizwa kutokana na kuzama kwao katika kutenda ovu hili.



“Na (wakumbushe) Luti alipowaambia watu wake: "Je, mnafanya uchafu, na hali mnaona?"
"Mnawaingilia wanaume kwa matamanio mabaya badala ya wanawake? Hakika nyinyi ni watu mfanyao ujinga kabisa." (27:54-55)



Pamoja na nasaha walizopewa na Mtume wao, Lut (a.s), watu hawa hawakutaka kubabili tabia yao chafu.
Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: “Wafukuzeni wafuasi wa Luti katika mji wenu, hao ni watu wanaojitakasa, (basi wasikae na sisi wachafu)." (2 7:56)



Wakasema: “Kama usipoacha, ee Luti (kutukataza haya), bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaofukuzwa (katika nchi hii)." (26:167)



Hukumu ya Allah (s.w) kwa watu hawa walionywa wasionyeke ilikuwa ni kuwaadhibu hapa hapa duniani na huko akhera wakiwa wanangojewa na adhabu kali.


Basi ilipofika amri yetu, tuliifanya ; juu yake kuwa chini yake, na tukawateremshia mvua ya changarawe za udongo mgumu (wa Motoni uliokamatana).
(Changarawe) zilizotiwa alama kwa Mola wako (kila moja kuwa ya mtu fulani). Na (adhabu) hii haiko mbali na madhalimu (wengine kama hawa watu wa umma huu wanaofanya machafu haya). (11:82-83)



Mtume (s.a.w) amelikemea vikali na kulitolea hukumu ya kifo tendo la kaumu Lut (ubasha) kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Hakika jambo ovu la kutisha ninalokhofia umat wangu, ni tendo la kaumu Lut." (Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah)
Akramah kutoka kwa Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yeyote yule mtakayemshika kwa kosa la kufanya kitendo cha kaumu Lut, muueni yeye na yule aliyefanyiwa kitendo hicho." (Tirmidh, Ibn Majah)



Pamoja na ukubwa wa uovu wa matendo haya ya Ubasha na Usagaji, uliobainishwa wazi katika Qur'an na Hadith Sahihi za Mtume (s.a.w), leo hii duniani kuna nchi zilizo halalisha ndoa za jinsia moja na kutoa uhuru kamili wa kufanya matendo ya zinaa, ubasha na usagaji. Hiki ndio kiwango cha kuporomoka kwa maadili duniani hivi leo. Lakusikitisha zaidi, ni kwamba nchi zilizoporomoka kimaadili kiasi hicho, ndizo zinazojikweza kwa ustaarabu na uungwana na nchi nyingine zikiwemo za Waislamu kuzifanya viigizo.



Maovu haya ya uzinzi na ubasha yametolewa hukumu kali kiasi hicho cha kuchapwa mijeledi 100 mbele ya hadhara au kuuawa ili kuiokoa jamii ya binaadamu na madhara makubwa yanayosababishwa na maovu haya.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2349

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 ai web app    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...
Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jeraha kwenye ngozi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k

Soma Zaidi...
Maswali juu ya nguzo za Imani

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Himizo la kuwasamehe waliotukosea

“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...