picha

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:

Il-hamu.

- Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.

 

 

 

Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.

- Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.

 

 

 

- Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.

 

    Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).

 

 

 

Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.

- Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.

 

    Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).

 

 

 

Ndoto za kweli (ndoto za mitume).

- Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.

 

 

 

- Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).

 

    Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).

 

 

 

Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).

- Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.

 

 

 

- Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).

 

    Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2774

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo Ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...