Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:
Il-hamu.
- Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.
Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.
- Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.
- Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.
Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).
Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.
- Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.
Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).
Ndoto za kweli (ndoto za mitume).
- Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.
- Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).
Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).
Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).
- Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.
- Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).
Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).
Umeionaje Makala hii.. ?
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.
Soma Zaidi...Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini.
Soma Zaidi...Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.
Soma Zaidi...Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.
Soma Zaidi...Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.
Soma Zaidi...Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.
Soma Zaidi...