Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu


image


Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).


Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:

Il-hamu.

- Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.

 

 

 

Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.

- Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.

 

 

 

- Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.

 

    Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).

 

 

 

Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.

- Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.

 

    Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).

 

 

 

Ndoto za kweli (ndoto za mitume).

- Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.

 

 

 

- Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).

 

    Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).

 

 

 

Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).

- Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.

 

 

 

- Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).

 

    Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).

 

 

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu). Soma Zaidi...