Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:
Il-hamu.
- Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.
Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.
- Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.
- Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.
Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).
Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.
- Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.
Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).
Ndoto za kweli (ndoto za mitume).
- Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.
- Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).
Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).
Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).
- Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.
- Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).
Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowNguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...