picha

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Mambo anayofanyiwa mtu (maiti) mara tu baada ya kufa.

Baada ya mtu kufa inatuwajibikia tuseme: “Innalillah wainnailaihraaji’una”. Qur’an (2:156). Kisha kumfanyia maiti mambo yafuatayo:

 

  1. Kwa taratibu kurudishia mdomo wake usiwe wazi kwa kufunga kwa    kitambaa kutoka kidevuni na kuzungushia kichwani.

 

  1. Kufunga macho ya marehemu na huku ukisema; 

Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah, Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake ya baadaye. Na jaalia anayokutanayo yawe bora kuliko aliyoyaacha.”

 

  1. Lainisha viungo vyake (miguu na mikono) kwa kukunja na kukunjua taratibu.

       -    Kama kuna ugumu maji ya uvuguvugu au mafuta yanaweza kutumika    kulaisha na kunyoosha viungo hivyo.

      -    Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na kulazwa uso   ukielekezwa Qibla kwenye mkeka au kitanda kisicho na godoro.  

 

  1. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo na kisha kufunikwa kwa shuka kubwa

-    Ni vyema afunwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu kizito ili tumbo lisifutuke.

 

  1. Marashi na ubani vitumike kwa wingi ili kuzima harufu ya uvundo wa maiti.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2210

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 ai web app     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Makundi ya dini za wanaadamu

Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...