Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Mambo anayofanyiwa mtu (maiti) mara tu baada ya kufa.

Baada ya mtu kufa inatuwajibikia tuseme: “Innalillah wainnailaihraaji’una”. Qur’an (2:156). Kisha kumfanyia maiti mambo yafuatayo:

 

  1. Kwa taratibu kurudishia mdomo wake usiwe wazi kwa kufunga kwa    kitambaa kutoka kidevuni na kuzungushia kichwani.

 

  1. Kufunga macho ya marehemu na huku ukisema; 

Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah, Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake ya baadaye. Na jaalia anayokutanayo yawe bora kuliko aliyoyaacha.”

 

  1. Lainisha viungo vyake (miguu na mikono) kwa kukunja na kukunjua taratibu.

       -    Kama kuna ugumu maji ya uvuguvugu au mafuta yanaweza kutumika    kulaisha na kunyoosha viungo hivyo.

      -    Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na kulazwa uso   ukielekezwa Qibla kwenye mkeka au kitanda kisicho na godoro.  

 

  1. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo na kisha kufunikwa kwa shuka kubwa

-    Ni vyema afunwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu kizito ili tumbo lisifutuke.

 

  1. Marashi na ubani vitumike kwa wingi ili kuzima harufu ya uvundo wa maiti.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views: 2455

Share On:

Share follows: 1 | Unique share links followed: 1
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 ai web app     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kuua nafsi bila ya Haki

Kuua nafsi bila ya Haki, ni kuiua nafsi isiyo na kosa linalostahiki hukumu ya kifo.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu?

Soma Zaidi...
Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.

Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.

Soma Zaidi...