image

Maswali juu ya nguzo za Imani

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 2.

  1. “Mungu hayupo kwa sababu milango ya fahamu haitambui”. Hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa Mungu Muumba. Onesha madai yao na madhaifu ya kila dai.
  2. Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.

 

  1. (a)  Orodhesha nyanja tano zinazoonesha kuwepo Mwenyezi Mungu.

(b)  kwa kutumia historia ya maisha ya mwanaadamu, Onesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.

  1. “Na katika nafsi zenu (kuna ishara) je, hamziyakinishi”? (51:21).

Kutokana na aya hii eleza ni kwa vipi nafsi (dhati) ya mwanaadamu inaonyesha uwepo wa Mwenyezi Mungu.

 

  1. Maisha ya Mitume ni uthibitisho tosha juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).

Thibitisha kauli hii.

  1. Bainisha athari ya maisha ya kila siku ya muumini wa kweli aliyemuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. (a)  Nini maana ya shirki.

(b)  Nini maana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku.

(c)  Taja makundi ya shirki.

 

8.   (a) “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” (31:13).

         Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.

      (b) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku?

    9.   (a)  Orodhesha sifa za Malaika unazozifahamu.

          (b)  Ni yapi majukumu ya Malaika?

          (c)    Ni upi umuhimu na maana ya kuamini Malaika katiaka maisha yetu ya kila siku?

    10. (a)  Bainisha Vitabu vilivyotajwa ndani ya Qur’an na Mitume walioteremshiwa kwayo.

          (b)  Kwa nini ni Kitabu cha Qur’an pekee ndio chenye sifa ya kuongoza maisha sahihi?

      (c)  Onesha dosari ya Vitabu vilivyotangulia kutoaminika kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanaadamu.

 

11.  ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’

          Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tano kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.

    12.  Ni lipi lengo la kuteremshwa Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w)?





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1619


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu? Soma Zaidi...

Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu
Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu. Soma Zaidi...

NGUZO ZA IMANI
Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s. Soma Zaidi...

1.0 NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)
1. Soma Zaidi...

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.
Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Kujiepusha na Shirk
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s. Soma Zaidi...

Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.
Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu. Soma Zaidi...

Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)
Soma Zaidi...

Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia
Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s. Soma Zaidi...

Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu
Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...