Maswali juu ya nguzo za Imani


image


Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


Zoezi la 2.

  1. “Mungu hayupo kwa sababu milango ya fahamu haitambui”. Hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa Mungu Muumba. Onesha madai yao na madhaifu ya kila dai.
  2. Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.

 

  1. (a)  Orodhesha nyanja tano zinazoonesha kuwepo Mwenyezi Mungu.

(b)  kwa kutumia historia ya maisha ya mwanaadamu, Onesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.

  1. “Na katika nafsi zenu (kuna ishara) je, hamziyakinishi”? (51:21).

Kutokana na aya hii eleza ni kwa vipi nafsi (dhati) ya mwanaadamu inaonyesha uwepo wa Mwenyezi Mungu.

 

  1. Maisha ya Mitume ni uthibitisho tosha juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).

Thibitisha kauli hii.

  1. Bainisha athari ya maisha ya kila siku ya muumini wa kweli aliyemuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. (a)  Nini maana ya shirki.

(b)  Nini maana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku.

(c)  Taja makundi ya shirki.

 

8.   (a) “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” (31:13).

         Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.

      (b) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku?

    9.   (a)  Orodhesha sifa za Malaika unazozifahamu.

          (b)  Ni yapi majukumu ya Malaika?

          (c)    Ni upi umuhimu na maana ya kuamini Malaika katiaka maisha yetu ya kila siku?

    10. (a)  Bainisha Vitabu vilivyotajwa ndani ya Qur’an na Mitume walioteremshiwa kwayo.

          (b)  Kwa nini ni Kitabu cha Qur’an pekee ndio chenye sifa ya kuongoza maisha sahihi?

      (c)  Onesha dosari ya Vitabu vilivyotangulia kutoaminika kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanaadamu.

 

11.  ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’

          Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tano kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.

    12.  Ni lipi lengo la kuteremshwa Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w)?



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Nafasi ya Elimu katika uislamu
Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu? Soma Zaidi...

image Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu) Soma Zaidi...

image Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu
Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Matendo ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Madhumuni ya dola ya uislamu
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Faida (matunda) ya kusimamisha swala katika jamii
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...