Maswali juu ya nguzo za Imani
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Zoezi la 2.
- “Mungu hayupo kwa sababu milango ya fahamu haitambui”. Hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa Mungu Muumba. Onesha madai yao na madhaifu ya kila dai.
- Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.
- (a) Orodhesha nyanja tano zinazoonesha kuwepo Mwenyezi Mungu.
(b) kwa kutumia historia ya maisha ya mwanaadamu, Onesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.
- “Na katika nafsi zenu (kuna ishara) je, hamziyakinishi”? (51:21).
Kutokana na aya hii eleza ni kwa vipi nafsi (dhati) ya mwanaadamu inaonyesha uwepo wa Mwenyezi Mungu.
- Maisha ya Mitume ni uthibitisho tosha juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).
Thibitisha kauli hii.
- Bainisha athari ya maisha ya kila siku ya muumini wa kweli aliyemuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
- (a) Nini maana ya shirki.
(b) Nini maana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku.
(c) Taja makundi ya shirki.
8. (a) “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” (31:13).
Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.
(b) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku?
9. (a) Orodhesha sifa za Malaika unazozifahamu.
(b) Ni yapi majukumu ya Malaika?
(c) Ni upi umuhimu na maana ya kuamini Malaika katiaka maisha yetu ya kila siku?
10. (a) Bainisha Vitabu vilivyotajwa ndani ya Qur’an na Mitume walioteremshiwa kwayo.
(b) Kwa nini ni Kitabu cha Qur’an pekee ndio chenye sifa ya kuongoza maisha sahihi?
(c) Onesha dosari ya Vitabu vilivyotangulia kutoaminika kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanaadamu.
11. ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’
Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tano kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.
12. Ni lipi lengo la kuteremshwa Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w)?
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 web hosting 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.
Soma Zaidi...Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah
Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.
Soma Zaidi...