picha

Maswali juu ya nguzo za Imani

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 2.

  1. “Mungu hayupo kwa sababu milango ya fahamu haitambui”. Hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa Mungu Muumba. Onesha madai yao na madhaifu ya kila dai.
  2. Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.

 

  1. (a)  Orodhesha nyanja tano zinazoonesha kuwepo Mwenyezi Mungu.

(b)  kwa kutumia historia ya maisha ya mwanaadamu, Onesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.

  1. “Na katika nafsi zenu (kuna ishara) je, hamziyakinishi”? (51:21).

Kutokana na aya hii eleza ni kwa vipi nafsi (dhati) ya mwanaadamu inaonyesha uwepo wa Mwenyezi Mungu.

 

  1. Maisha ya Mitume ni uthibitisho tosha juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).

Thibitisha kauli hii.

  1. Bainisha athari ya maisha ya kila siku ya muumini wa kweli aliyemuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. (a)  Nini maana ya shirki.

(b)  Nini maana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku.

(c)  Taja makundi ya shirki.

 

8.   (a) “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” (31:13).

         Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.

      (b) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku?

    9.   (a)  Orodhesha sifa za Malaika unazozifahamu.

          (b)  Ni yapi majukumu ya Malaika?

          (c)    Ni upi umuhimu na maana ya kuamini Malaika katiaka maisha yetu ya kila siku?

    10. (a)  Bainisha Vitabu vilivyotajwa ndani ya Qur’an na Mitume walioteremshiwa kwayo.

          (b)  Kwa nini ni Kitabu cha Qur’an pekee ndio chenye sifa ya kuongoza maisha sahihi?

      (c)  Onesha dosari ya Vitabu vilivyotangulia kutoaminika kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanaadamu.

 

11.  ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’

          Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tano kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.

    12.  Ni lipi lengo la kuteremshwa Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w)?

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/15/Saturday - 08:03:07 am Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2700

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah

Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah

Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).

Soma Zaidi...
Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Soma Zaidi...
Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake

Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
SHIRK

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya dini

Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu katika mtazamo wa Uislamu

Katika Uislamu elimu imegawanyika katika Elimu ya muongozo na elimu ya mazingira.

Soma Zaidi...