Maswali juu ya nguzo za Imani
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Zoezi la 2.
- “Mungu hayupo kwa sababu milango ya fahamu haitambui”. Hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa Mungu Muumba. Onesha madai yao na madhaifu ya kila dai.
- Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.
- (a) Orodhesha nyanja tano zinazoonesha kuwepo Mwenyezi Mungu.
(b) kwa kutumia historia ya maisha ya mwanaadamu, Onesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.
- “Na katika nafsi zenu (kuna ishara) je, hamziyakinishi”? (51:21).
Kutokana na aya hii eleza ni kwa vipi nafsi (dhati) ya mwanaadamu inaonyesha uwepo wa Mwenyezi Mungu.
- Maisha ya Mitume ni uthibitisho tosha juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w).
Thibitisha kauli hii.
- Bainisha athari ya maisha ya kila siku ya muumini wa kweli aliyemuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
- (a) Nini maana ya shirki.
(b) Nini maana ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku.
(c) Taja makundi ya shirki.
8. (a) “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” (31:13).
Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.
(b) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku?
9. (a) Orodhesha sifa za Malaika unazozifahamu.
(b) Ni yapi majukumu ya Malaika?
(c) Ni upi umuhimu na maana ya kuamini Malaika katiaka maisha yetu ya kila siku?
10. (a) Bainisha Vitabu vilivyotajwa ndani ya Qur’an na Mitume walioteremshiwa kwayo.
(b) Kwa nini ni Kitabu cha Qur’an pekee ndio chenye sifa ya kuongoza maisha sahihi?
(c) Onesha dosari ya Vitabu vilivyotangulia kutoaminika kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanaadamu.
11. ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’
Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tano kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.
12. Ni lipi lengo la kuteremshwa Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w)?
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
(b)Umbile la Mwanaadamu ni la kidini
Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini.
Soma Zaidi...Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.
Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.
Soma Zaidi...