picha

Ni haramu kwa Waumini kuwaoa au kuolewa na Wazinifu, Washirikina na Mahabithi

Ni haramu kwa Waumini kuwaoa au kuolewa na Wazinifu, Washirikina na Mahabithi

Ni haramu kwa Waumini kuwaoa au kuolewa na Wazinifu, Washirikina na Mahabithi


Mwanamume mzinifu hafungamani ila na mwanamke mzinifu au mwanamke mshirikina; na mwanamke mzinifu hafungamani naye ila mwanamume mzinifu au mshirikina; na hayo yameharamishwa kwa waumini" (24:3)


Wanawake habithi (wabaya) ni wa wanaume habithi na wanaume habithi ni wa wanawake habithi; na wanawake wema ni wa wanaume wema na waume wema ni wa wanawake wema ….. " (24:26)



Aya hizi zinatuweka wazi kuwa ili kujenga jamii iliyoinukia kimaadili, waumini hawanabudi kuwa macho katika uchumba. Waumini wahakikishe kuwa katika ndoa ya kwanza binti muolewaji ni bikra na kijana muoaji ni bikra vile vile. Kadhalika katika ndoa ya pili, waumini wasiidhinishe ndoa mpaka wawe na uhakika pasina tone la shaka, kuwa waoanaji wawili ni watwaharifu na wacha-Mungu. Mwanamume mzinifu ni mshirikina kwa mujibu wa Qur'an kwa kuwa ameyafanya matamanio ya nafsi yake kuwa Mungu badala ya Allah (s.w)


"Je, umemuona yule aliyefanya matamanio (ya nafsi) yake (kila anachokipenda), kuwa Mungu wake? Basi je, utaweza kuwa mlinzi wake (ukamhifadhi na hayo, na hali ya kuwa hataki)? (25:43)


Kukiukwa kwa maagizo ya Allah (s.w), katika aya hizi (24:3, 26), imekuwa ni sababu kubwa ya mtafaruku katika familia nyingi za Waislamu na jamii kwa ujumla. Familia za waumini zitaishi kwa furaha na amani endapo ujumbe wa aya hizi utafuatwa vilivyo tangu mapema katika kuanzisha familia hizi.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1907

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 web hosting    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tawhiid

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)

(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...