DUA WAKATI WA KURUKUU,KUITIDALI, KUSUJUDI NA NAMNA YA KUSOMA TAHIYATU

DUA WAKATI WA KURUKUU,KUITIDALI, KUSUJUDI NA NAMNA YA KUSOMA TAHIYATU

6.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

DUA WAKATI WA KURUKUU,KUITIDALI, KUSUJUDI NA NAMNA YA KUSOMA TAHIYATU

6. Kurukuu
Baada ya kusoma Suratul-Fatiha na Surah nyingine, au baadhi ya aya katika sura nyingine unasema Allahu-akbar kisha unarukuu (kuinama). Rukuu ni nguzo ya swala pamoja na kujituliza humo. Katika rukuu ni sunnah kumsabihi Allah (s.w) kwa kusema kimya kimya mara tatu au zaidi “Subhana Rabbiyal’Adhiim” “Utukufu ni wako Ee Bwana (Mlezi) wangu Uliye mkuu”

7.Kuitidal
Kuitidali ni kusimama wima kutoka kwenye rukuu, ni sunnah kusema wakati wa kunyanyuka maneno haya:“sami’a llahu liman hamidahu” Mwenyezi Mungu anamsikia kila mwenye kumhimidi. Na baada ya kusimama sawa ni sunnah kusema “rabbanaa walakal-hamdu”ewe mola wetu sifa zote za ukamilifu ni zako. Pia ni sunnah kusema maneno haya “rabbanaa walakal-hamdu mil-as-samaawati wamil-al-ardhi wamil-amashi-ita minshai-in ba’adah” Ewe Mola wetu sifa zote za ukamilifu ni za kwako, kutoka mbinguni, kutoka ardhini na katika vitu vyote vilivyo baina yao (mbingu na ardhi) na kutoka katika vinginevyo unavyo viridhia

8.Kusujudi
Ni nguzo pamoja na kujituliza katika sujudi. Mkusujudi ni kuvituliza chini viungo saba kwa utaratibu wa swala. Vingo hivyo ni , paji a uso, viganya viwili vya mikono, magoti mawili na matumbo ya nyayo za vidole vya miguuni.viungo vyote hivi vinatakiwa vielekee kibla. Paji la uso ni pamoja na pua iguse chini.utasema kwenye sijda “subhaana rabbiyal-a’alaa” utukufu ni wa kwako Mola uliye tukuka.

9.kukaa baina ya sijda mbili
Hiki ni kitako kinachopatikana baada ya kutoka kusujudi. Sifa ya kikao hiki ni kukalia unyayo wa mguu wa kushoto na kuweka mikono miwili juu ya mapaja. Ni sunnah kusema maneno haya: “rabbigh-firliy warhamnii wa’afinii warzuqniy”Ewe Mola wangu nisamehe, na unirehemu, na unipe afya na uniruzuku

10.kikaa tahiyyatu
Katika kukaa Thiyyatu mtume alikuwa akikalia futi la mguu wa kushoto na kusimamisha futi la mguu wa kulia na katika tahiyyatu ya mwisho alikaa chini na kuulaza mguu wa kushoto katika uvungu wa mguu wa kulia na alisimamisha futi la mguu wa kulia, katika vikao vyote hivyo viwili,

Mtume (s.a.w) alivilaza viganja vyake juu ya mapaja karibu na magoti kama tunavyoelezwa katika hadith ifuatayo: Abdullah bin Jubair(r.a) ameeleza kuwa wakati Mtume (s.a.w) alipokaa tahiyyatu, alikuwa akiweka kiganja chake cha mkono wa kulia juu ya paja lake la kulia na kiganja cha mkono wa kushoto juu ya paja la mguu wa kushoto na alikuwa akinyoosha kidole chake cha shahada (wakati wa k u s e m a , “ A s h - h a d u anllaaillaha illallah) na kukiegemeza juu ya kidole gumba na alikuwa akiweka kiganja chake cha mkono wa kushoto juu ya goti lake (la mguu wa kushoto). (Muslim).


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 5021

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah

Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali
Jifunze ni kwa namna gani Malaika waliweza kuwasiliana ana manabii Malimbali

Wakatibmeingibe Allah anapotaka kuwasiliana na wanadamu hutuma Malaika wake.

Soma Zaidi...
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu

Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu katika uislamu? Nini naana ya elimu ya muongizo. Je elimu ya mazingiravmaana yakeni nini. Ni upi utofauti wa elimu ya muongozo na elimu ya mazingira?

Soma Zaidi...