image

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku


Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini. Hii ni kwa sababu:



1.Imani ya kweli juu ya Malaika humuepusha Muumini na kumshirikisha Allah (s.w) na viumbe vyake, hasa vile visivyoonekana, miongoni mwa hivyo ni Malaika na Majini.



2.Muislamu anaamini kuwa Malaika ni viumbe watukufu ambao wametakasika na dhambi na kila aina ya uchafu, lakini binaadamu amepewa daraja ya juu zaidi pindi atakapotimiza wajibu wake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa duniani. Imani hii humpelekea mtu kujitahidi upeo wa uwezo wake kuishi maisha yanayolingana na cheo hiki kikubwa, cheo ambacho Malaika walikitamani (Rejea Qur-an, 2:30)..



3.Muislam anaamini kuwa kila wakati na kila alipo yu pamoja na Malaika watukufu. Imani hii peke yake inatosha kumfanya mtu abadili tabia yake. Hii ni kwa sababu binaadamu ameumbwa na haya, kwa hiyo huhuzunika akifanya mambo maovu mbele ya watu na hasa mbele ya watu anaowaheshimu.


4.Muislamu anaamini kuwa Malaika hao sio tu kuwa wapo naye daima bali wanahudhurisha mbele ya Allah (s.w) kila anachokitenda. Imani hii ikithibiti moyoni humfanya Muislam ajitahidi kufanya mambo mema na ajitahidi kuepuka maovu.



5.Muislamu anajua kuwa Malaika sio tu hupendezwa na mema, bali pia humuombea mtu huyo anayefanya mema, maghfira kwa Allah (s.w) jambo ambalo humzidishia Muislamu hima ya kutenda mema daima na kujiepusha na maovu hata akiwa peke yake.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 522


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Nguzo za Imani kwa mujibu wa mafunzo ya kiislami.
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu nguzo sita za imani katika Uislamu. Soma Zaidi...

KUAMINI MALAIKA WA ALLAH (S.W.)
Soma Zaidi...

Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri
Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera. Soma Zaidi...

Lengo la kuletwa mitume
Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:โ€œKwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere.. Soma Zaidi...

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...

Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote
Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu) Soma Zaidi...

Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu
Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ? Soma Zaidi...

Dalili (Alama) za Qiyama
Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Muโ€™uminuun (23:1-11)
Soma Zaidi...

Ni Ipi Elimu yenye manufaa
Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu. Soma Zaidi...