picha

Himizo la kuwasamehe waliotukosea

“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).

Himizo la kuwasamehe waliotukosea

(e) Himizo la kuwasamehe waliotukosea


“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni? Na Allah ni msamehevu, mrehemevu. ”(24:22)



Tukirejea historia, Bi 'Aisha (r.a) amesema kuwa baada ya kuteremshwa aya za (24:11-21) zilizomtakasa na uzushi wa wanafiki, baba yake, Abu Bakr (r.a) aliapa kuwa hatamsaidia tena kwa mali Mistah bin Uthatha, miongoni mwa watu waliokuwa mstari wa mbele katika kueneza uzushi dhidi ya Bi 'Aisha (r.a).


Katika kufanya kitendo cha kueneza uzushi, Mistah hakuonyesha kabisa kujali mahusiano wala ihsani ambazo Abu Bakar (r.a) daima alikuwa anamfanyia yeye na familia yake. Hili lilimkasirisha sana Abu Bakar mpaka kumfikisha kwenye kuchukua kiapo cha kusitisha msaada wake kwa Mistah. Baada ya kushushwa aya hii, Abu Bakar aliomba msamaha kwa Allah (s.w) na akaanza tena kumsaidia Mistah kwa moyo mkunjufu zaidi kuliko hata hapo awali.



Kwa mujibu wa 'Abdullah bin 'Abbas (r.a), waumini wengine miongoni mwa maswahaba pia waliapa kuwa hawatawasaidia tena wale wote walioshiriki katika kusambaza masingizio dhidi ya Bi 'Aisha (r.a). Lakini baada ya kuteremshwa aya hii, wote walivibatilisha viapo vyao, na uhasama wote uliosababishwa na hayo 'masingizio' ukaisha.
Kwa mujibu wa aya hii na maelezo haya ya kihistoria tunajifunza kuwa:



(i) Katika maadili mema, hatuna budi kuendelea kuwafanyia wema wale waliotukosea, maadamu hatudhuriki tukiendelea kuwafanyia hivyo. Hekima ya kufanya hivyo Allah (s.w) anaibainisha katika aya zifuatazo:


"Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha ubaya (unaofanyiwa) kwa wema, tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, anakuwa kama jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu" Lakini jambo hili hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (Mbele ya Allah (s.w))." (41:34-35)


(ii) Hatuna budi kuwa wepesi kuwasamehe wale walio tukosea ili iwe sababu na sisi kusamehewa makosa yetu na Allah (s.w)"
Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni?……" (24:22)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1288

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 ai web app    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuamini siku ya mwisho

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...
Kwanini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini?

Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...