Himizo la kuwasamehe waliotukosea

“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).

Himizo la kuwasamehe waliotukosea

(e) Himizo la kuwasamehe waliotukosea


“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni? Na Allah ni msamehevu, mrehemevu. ”(24:22)



Tukirejea historia, Bi 'Aisha (r.a) amesema kuwa baada ya kuteremshwa aya za (24:11-21) zilizomtakasa na uzushi wa wanafiki, baba yake, Abu Bakr (r.a) aliapa kuwa hatamsaidia tena kwa mali Mistah bin Uthatha, miongoni mwa watu waliokuwa mstari wa mbele katika kueneza uzushi dhidi ya Bi 'Aisha (r.a).


Katika kufanya kitendo cha kueneza uzushi, Mistah hakuonyesha kabisa kujali mahusiano wala ihsani ambazo Abu Bakar (r.a) daima alikuwa anamfanyia yeye na familia yake. Hili lilimkasirisha sana Abu Bakar mpaka kumfikisha kwenye kuchukua kiapo cha kusitisha msaada wake kwa Mistah. Baada ya kushushwa aya hii, Abu Bakar aliomba msamaha kwa Allah (s.w) na akaanza tena kumsaidia Mistah kwa moyo mkunjufu zaidi kuliko hata hapo awali.



Kwa mujibu wa 'Abdullah bin 'Abbas (r.a), waumini wengine miongoni mwa maswahaba pia waliapa kuwa hawatawasaidia tena wale wote walioshiriki katika kusambaza masingizio dhidi ya Bi 'Aisha (r.a). Lakini baada ya kuteremshwa aya hii, wote walivibatilisha viapo vyao, na uhasama wote uliosababishwa na hayo 'masingizio' ukaisha.
Kwa mujibu wa aya hii na maelezo haya ya kihistoria tunajifunza kuwa:



(i) Katika maadili mema, hatuna budi kuendelea kuwafanyia wema wale waliotukosea, maadamu hatudhuriki tukiendelea kuwafanyia hivyo. Hekima ya kufanya hivyo Allah (s.w) anaibainisha katika aya zifuatazo:


"Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha ubaya (unaofanyiwa) kwa wema, tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, anakuwa kama jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu" Lakini jambo hili hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (Mbele ya Allah (s.w))." (41:34-35)


(ii) Hatuna budi kuwa wepesi kuwasamehe wale walio tukosea ili iwe sababu na sisi kusamehewa makosa yetu na Allah (s.w)"
Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni?……" (24:22)




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 613

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?

Soma Zaidi...
Makundi ya dini za wanaadamu

Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.

Soma Zaidi...
Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Nafasi ya akili katika kumtambua Allah

Kwa kutumia akili yako unaweza kumtambua Allah bila ya shaka yeyote ile. Postbhii itakufundisha nafasi ya akilonkatika kutambuwa uwepo na Uwezo wa Allah.

Soma Zaidi...