Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea

Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea

Iddil -Fitri



Iddil-Fitri ni siku kuu ya Kiislamu ya kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Ramadhani. Mwezi wa Ramadhani ambao ndani yake imefaradhishwa funga ambayo imeambatanishwa na matendo mbali mbali ya sunnah, umekusudiwa uwe mwezi wa mafunzo na mazoezi ya kumfanya mja awe mchaji Mungu katika kiwango kinachostahiki kwa kipindi chote cha mwaka mzima.


Iddil-Fitri ndicho kilele cha mafunzo haya ambapo Waislamu wanafurahia na kumshukuru Allah (s.w) kwa kumaliza salama mafunzo haya muhimu na wakati huo huo humuomba Allah (s.w) ayafanye mafunzo hayo yawe yenye kuwafikisha kwenye lengo lililokusudiwa. Hivyo, moja kwa moja inadhihiri kuwa Iddil-Fitri haisherehekewi kwa mavazi mazuri na kwa vyakula na vinywaji vizuri tu, bali kilele cha sherehe hii kinafikiwa kwa kuswali swala ya Iddil-Fitri na kumtukuza na kumuhimidi Allah (s.w) sana kwa Takbira.



Swala ya Iddil-Fitri



Swala ya Idd mbili - Iddil-Fitri na Iddil-Hajj (kilele cha ibada ya Hija) ni sunnah zilizokokotezwa. Swala ya Idd inaswaliwa kwa rakaa mbili na kufuatiwa na Khutuba mbili kama zile zinazosomwa kabla ya swala ya Ijumaa. Swala ya idd ina Takbira 12,takbira 7 hutolewa katika rakaa ya kwanza kabla ya kusoma suratul-Faatiha na takbira 5 huletwa katika rakaa ya pili. vile vile kabla ya kusoma suratul-Faatiha.Mahali pa kuswalia Idd ni bora pawe uwanjani ili Waislamu wakusanyike pamoja kutoka sehemu mbali mbali za mji. Mtume (s.a.w) alikuwa akifanya hivyo. Ni sunnah kula chochote kabla ya kuswali Iddil-Fitri kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifu atazo:



Anas (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah hakw enda kusw ali Iddil- Fitri mpaka alipokula Tende katika idadi ya witri. (Bukhari).
Buraydah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa hatoki kwa swala ya Iddil-Fitri mpaka awe amekula (Kitu) na hakuwa anakula katika s iku ya kuchinja (Iddil-Haj) mpaka asw ali (Dirim i).



Ni sunnah kuleta takbira mara kwa mara kuanzia pale mwezi wa Shawwal unapoandama mpaka baada ya swala ya Iddil-fitri. Takbira


Tafsiri ya Takbira:
Allah Mkubwa, Allah Mkubwa, Allah Mkubwa hapana mola ila Allah Allah Mkubwa, Allah Mkubwa na shukurani zote ni za Allah. Allah Mkubwa aliyetukuka, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi, na namtakasa asubuhi na jioni. Hapana Mola ila Allah. Wala hatumuabudu yeyote ila Yeye peke yake, tunamtakasa yeye na dini yake hata kama w atachukia makafiri.Hapana mola ila Allah peke yake. Ameisadikisha (ameitimiza) ahadi yake na akamnusuru mja (Mtume s.a.w) wake, na akalitukuza jeshi lake, akalipa ushindi kundi lake. Hapana mola ila Allah. Allah Mkubwa. Ewe Allah, teremsha rehma zako juu ya Muhammad, na Maswahaba wake Muhammad, na waliomnusuru Muhammad, na Wakeze Muhammad, na kizazi chake Muhammad, na uwape salama na amani kwa wingi.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2300

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Matendo ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi

Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.

Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...
Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu

Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.

Soma Zaidi...
Swala ya jamaa na taratibu zake

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake.

Soma Zaidi...