Kukaa itiqaf na sheria zake hasa katika mwezi wa ramadhani

Kukaa itiqaf na sheria zake hasa katika mwezi wa ramadhani

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kukaa itiqaf na sheria zake hasa katika mwezi wa ramadhani

Kukaa Itiqaf



Kukaa Itiqaf katika kumi la mwisho la Ramadhani ni sunna iliyokokotezwa. Ki-lugha “Itqaf” ina maana ya kukaa mahali. katika sheria ya Kiislamu “Itiqaf” ni kukaa msikitini kwa ajili tu ya kumkumbuka na kumtukuza Allah (s.w) na kufanya ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an na kufanya amali yoyote njema ambayo inaruhusiwa kufanyika msikitini nje ya shughuli za kawaida za kutafuta rizki. Kwa hiyo mahali pa kukalia “Itiqaf” ni msikitini kama ilivyotajwa katika Qur-an:



“... Wala msichanganyike nao, na hali mmekaa Itiqaf misikitini .... ” (2:187).



Misikiti inayokaliwa Itiqaf iwe ni ile inayoswaliwa jamaa na Ijumaa ili pasiwe na haja ya kutoka kwa swala za jamaa au kwa swala ya Ijumaa. Wanawake wanaruhusiwa kufanyia Itiqaf zao majumbani mwao katika sehemu zao za kusalia lakini baada ya kupata ruhusa kutoka kwa waume zao. Kwa muda wote mtu atapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kutokatoka msikitini ila kwa dharura kubwa sana kama vile kwenda haja au kwenda kula. Mtu akiwa katika Itiqaf hulazimika kujitenga na shughuli zote za kutafuta maslahi ya maisha na shughuli zote za kijamii kama vile kutembelea wagonjwa, kuhudhuria mazishi, na kadhalika. Mtu anapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kuchanganyika na mkewe.


“ ... Na w ala msichanganyike nao na hali mnakaa Itiqaf msikitini. (2:187).
Kwa ujumla katika muda huu wa kukaa Itiqaf, Mu’takif (Mwenye kukaa Itiqaf) anatakiwa ajihusishe tu na ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an, kuleta tasbihi, tahmid, tahalili, takbir, istighfar na maombi mbali mbali.



Mu’takif anaruhusiwa kuja na matandiko yake msikitini na kuyaweka mahali pa uficho ambapo hayatawakarahisha watu wakati wa swala ya jamaa. Katika miezi mingine isiyokuwa Ramadhani mtu anaweza kukaa itiqaf kwa muda wowote ule, siku moja au masaa machache. Ni vyema mtu anapokuwa hana shughuli muhimu, anuie kukaa Itiqaf msikitini badala ya kujiingiza kwenye shughuli zisizo muhimu au shughuli za upuuzi zenye kumuingiza katika dhambi na kumpotezea muda ambao ni rasilimali pekee ya maisha yake. Katika mwezi wa Ramadhani Itiqaf imekokotezwa sana katika kumi la mwisho ili kumuwezesha Muumini kuudiriki usiku wa Lailatul-Qadr - akiwa katika hali ya kumkumbuka Allah (s.w). Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika kumi hili la mwisho kama tunavyojifunza katika hadith zifu atazo:



Ames imulia Abdullah bin Umar (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za mw ezi wa Ram adhani. (Bukhari na Muslim).



Aysha (r.a.) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za Ramadhani mpaka alipotawafu (Allah alipo mchukua).Kisha wakeze waliendelea kukaa Itiqaf baada yake. (Bukhari na Muslim).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1560

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki

Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako.

Soma Zaidi...
Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki za raia katika dola ya kiislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mifumo ya benki ya kiislamu.
Mifumo ya benki ya kiislamu.

Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha

Soma Zaidi...