Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4.

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4. FAMILIA YA KIISLAMU

4.1. Ndoa Katika Uislamu

1. Maana ya Ndoa:

Kilugha: ni mkataba wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kufuata utaratibu uliowekwa na jamii.
Kisheria: ni mkataba wa hiari wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kuzingatia sharti na taratibu za Kiislamu.




2. Umuhimu wa ndoa katika Uislamu

Ni jambo lililokokotezwa sana kwani ni katika Sunnah za Mtume (s.a.w) yenye umuhimu ufuatao;
i. Kuhifadhi jamii na zinaa

- Ndoa hukinga wanandoa na jamii kwa ujumla na zinaa kwa kuhifadhi tupu zao na kukidhi matamanio baina yao.
Rejea Qur’an (5:5), (4:24)



ii. Kuendeleza kizazi cha mwanaadamu kwa utaratibu mzuri

- Lengo la ndoa pia ni kuhifadhi, kutunza na kuendeleza kizazi cha mwanaadamu bila kuzaliana kiholela.
Rejea Qur’an (4:1), (42:11)



iii. Kujenga mapenzi, huruma na ushirikiano katika familia

- Ndoa huleta utulivu katika moyo kati ya wanandoa na kupatikana huruma, mapenzi na ushirikiano baina yao
Rejea Qur’an (30:21), (2:187)




iv. Kukuza uhusiano na udugu katika jamii

- Uhusiano na udugu kati ya wanafamilia walioana huimarika na kuongezeka zaidi kuwa ukoo, kabila, taifa, n.k
Rejea Qur’an (25:54), (49:13)



v. Kukilea kizazi katika maadili

- Ndoa inakusudiwa kuwa kiungo cha kulea na kuelimisha kizazi katika tabia na maadili mema anayoyaridhia Allah (s.w).


vi. Kumuendeleza mwanaadamu kiuchumi

- Ndoa huchochea wanandoa na wanajamii kwa ujumla kujijenga kiuchumi ili kukidhi mahitaji muhimu ya kimaisha na kibinaadamu.
Rejea Qur’an (6:151)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3991

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno

Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.

Soma Zaidi...
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika

Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.

Soma Zaidi...
Waislamu wanaolazimika kufunga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...