4.
4.1. Ndoa Katika Uislamu
1. Maana ya Ndoa:
Kilugha: ni mkataba wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kufuata utaratibu uliowekwa na jamii.
Kisheria: ni mkataba wa hiari wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kuzingatia sharti na taratibu za Kiislamu.
2. Umuhimu wa ndoa katika Uislamu
Ni jambo lililokokotezwa sana kwani ni katika Sunnah za Mtume (s.a.w) yenye umuhimu ufuatao;
i. Kuhifadhi jamii na zinaa
- Ndoa hukinga wanandoa na jamii kwa ujumla na zinaa kwa kuhifadhi tupu zao na kukidhi matamanio baina yao.
Rejea Qurโan (5:5), (4:24)
ii. Kuendeleza kizazi cha mwanaadamu kwa utaratibu mzuri
- Lengo la ndoa pia ni kuhifadhi, kutunza na kuendeleza kizazi cha mwanaadamu bila kuzaliana kiholela.
Rejea Qurโan (4:1), (42:11)
iii. Kujenga mapenzi, huruma na ushirikiano katika familia
- Ndoa huleta utulivu katika moyo kati ya wanandoa na kupatikana huruma, mapenzi na ushirikiano baina yao
Rejea Qurโan (30:21), (2:187)
iv. Kukuza uhusiano na udugu katika jamii
- Uhusiano na udugu kati ya wanafamilia walioana huimarika na kuongezeka zaidi kuwa ukoo, kabila, taifa, n.k
Rejea Qurโan (25:54), (49:13)
v. Kukilea kizazi katika maadili
- Ndoa inakusudiwa kuwa kiungo cha kulea na kuelimisha kizazi katika tabia na maadili mema anayoyaridhia Allah (s.w).
vi. Kumuendeleza mwanaadamu kiuchumi
- Ndoa huchochea wanandoa na wanajamii kwa ujumla kujijenga kiuchumi ili kukidhi mahitaji muhimu ya kimaisha na kibinaadamu.
Rejea Qurโan (6:151)
Umeionaje Makala hii.. ?
Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.
Soma Zaidi...Je inapoonekana sehemu moja tufunge duania nzima ama tufunge kwa kuangalia mwandamo katika maenro tunayoishi.
Soma Zaidi...- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.
Soma Zaidi...Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.
Soma Zaidi...Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...