Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4. FAMILIA YA KIISLAMU

4.1. Ndoa Katika Uislamu

1. Maana ya Ndoa:

Kilugha: ni mkataba wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kufuata utaratibu uliowekwa na jamii.
Kisheria: ni mkataba wa hiari wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kuzingatia sharti na taratibu za Kiislamu.




2. Umuhimu wa ndoa katika Uislamu

Ni jambo lililokokotezwa sana kwani ni katika Sunnah za Mtume (s.a.w) yenye umuhimu ufuatao;
i. Kuhifadhi jamii na zinaa

- Ndoa hukinga wanandoa na jamii kwa ujumla na zinaa kwa kuhifadhi tupu zao na kukidhi matamanio baina yao.
Rejea Qur’an (5:5), (4:24)



ii. Kuendeleza kizazi cha mwanaadamu kwa utaratibu mzuri

- Lengo la ndoa pia ni kuhifadhi, kutunza na kuendeleza kizazi cha mwanaadamu bila kuzaliana kiholela.
Rejea Qur’an (4:1), (42:11)



iii. Kujenga mapenzi, huruma na ushirikiano katika familia

- Ndoa huleta utulivu katika moyo kati ya wanandoa na kupatikana huruma, mapenzi na ushirikiano baina yao
Rejea Qur’an (30:21), (2:187)




iv. Kukuza uhusiano na udugu katika jamii

- Uhusiano na udugu kati ya wanafamilia walioana huimarika na kuongezeka zaidi kuwa ukoo, kabila, taifa, n.k
Rejea Qur’an (25:54), (49:13)



v. Kukilea kizazi katika maadili

- Ndoa inakusudiwa kuwa kiungo cha kulea na kuelimisha kizazi katika tabia na maadili mema anayoyaridhia Allah (s.w).


vi. Kumuendeleza mwanaadamu kiuchumi

- Ndoa huchochea wanandoa na wanajamii kwa ujumla kujijenga kiuchumi ili kukidhi mahitaji muhimu ya kimaisha na kibinaadamu.
Rejea Qur’an (6:151)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2813

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.
Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.

Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika.

Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu:Shahada
Nguzo za uislamu:Shahada

Nguzo za uislamu: Shahada (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kutoa vilivyo vizuri
Kutoa vilivyo vizuri

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani
Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi

Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.

Soma Zaidi...