picha

Siku ya idi al-fitir na namna ya kusherekea idi

Siku ya idi al-fitir na namna ya kusherekea idi

Yaliyo Sunnah kuyafanya Siku ya Idd



Ni sunnah siku ya Idd kukoga, kuvalia nguo nzuri kuliko zote ulizo nazo na kupaka uturi (manukato) kwa wanaume. Pia ni sunnah siku ya Idd kupika vyakula na kuandaa vinywaji vizuri zaidi kuliko siku za kawaida. kwa wafugaji na wale wenye wasaa, ni sunah kumchinja mnyama aliye bora zaidi kuliko wengine katika mifugo yake kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:



Amehadithia Hasan Asibbit (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) ametuamrisha katika Idd m bili kuvaa vizuri zaidi kadri tuw ezavyo, tupake uturi bora zaidi kuliko wote tulionao, na tuchinje wanyama wenye thamani zaidi kuliko wote tu lion a o. (A l-Ha kim).



Ni sunnah vile vile kuwakaribisha ndugu, marafiki, majirani, maskini, yatima na wengine wasiojiweza. Ni sunnah kuwatembelea ndugu, marafiki, majirani na wagonjwa. Ni sunnah vile vile kupeana zawadi.



Tahadhari Katika Siku ya Idd
Waislamu hawana budi kukumbuka kuwa sherehe za Kiislamu, makusudio yake na muundo wake, ni tofauti kabisa na sherehe zisizokuwa za Kiislamu. Sherehe za Kiislamu ni kilele cha kuonyesha shukrani zetu kwa Allah (s.w) kwa kutujaalia na kutuwezesha kutimiza wajibu wetu kwake katika kutekeleza ibada kubwa na nzito kama vile kufunga Ramadhani na kukamilisha Ibada ya Hija. Hivyo, sherehe hizi ni lazima ziambatane na kumshukuru, kumtukuza, kumtaja na kumkumbuka sana Allah (s.w).



Tunafahamu kuwa katika sherehe zisizokuwa za Kiislamu au zisizosherehekewa kwa mtazamo wa Kiislamu, ndio wakati ambao Allah (s.w) husahauliwa kuliko nyakati zote na ndio wakati ambao shetani hukumbukwa na kuadhimishwa kuliko nyakati zote. Kwa maana nyingine katika sherehe hizi watu hujiingiza kwa furaha na kicheko katika kumuasi Allah (s.w). Kutokana na uzoefu wetu sherehe hizi zimeambatana na ulevi, ngoma na mziki, mchanganyiko wa wanaume na wanawake, uzinifu na mengineyo kama haya.



Waislamu wanatahadharishwa sana wajiepushe na sherehe za namna hii, kwani zitawafanya wawe ni wenye kukufuru badala ya kuwa wenye kumshukuru Allah (s.w), kwa mafanikio hayo wanayo yasherehekea. Katika sherehe hizi za Idd Muislamu anatakiwa achukue hadhari kubwa katika kuchunga mipaka ya sherehe, kwani kumuasi Allah (s.w) katika siku ya Idd ni kosa kubwa sana mbele ya Allah kuliko kumuasi Allah (s.w) wakati mwingine, Mtume (s.a.w) amesema:
“Kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Idd ni sawa na kumuasi Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama ”.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2061

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Zoezi la 6 kusimamisha swala

Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...
Namna ya kurithisgha hatuwa kwa hatuwa.

Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.

Soma Zaidi...