Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Malezi ya Mtoto Mchanga baada ya Talaka
Mtoto mchanga hataachanishwa na mama yake mpaka awe na umri wa miaka miwili - umri wa kuacha kunyonya. Matumizi ya mama na mtoto katika kipindi hiki cha kunyonya mtoto yatakuwa juu ya mume japo mkewe aliyemtaliki atakuwa kwa wazazi wake au penginepo nje ya nyumbani kwake. Lakini mume na mke walioachana, wakiridhiana wanaweza kumwachisha kunyonya kabla ya miaka miwili au wanaweza kumkodisha mwanamke mwingine amnyonyeshe. Hukumu hii ya malezi ya mtoto baada ya mume na mke kuachana inabainishwa vyema katika Qur-an:
Na wanawake waliozaa wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili; kwa anayetaka kukamilisha kunyonyesha; na ni juu ya baba (yake) chakula chao (hao watoto na mama) na nguo zao kwa sheria. Wala haikalflshwi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya wasaa wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake, wala baba (asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake).
Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa (kabla ya miaka miwili), kwa kuridhiana na kushauriana, basi sio kosa juu yao. Na kama mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha (wengine wasiokuwa mama zao) basi haitakuwa dhambi juu yenu kama mkitoa (kuwapa hao wanyonyeshaji) mlichowaahidi kwa sharia. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyatenda. (2:233)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.
Soma Zaidi...Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi
Soma Zaidi...Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.
Soma Zaidi...Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.
Soma Zaidi...