Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija

Maandalizi ya Safari ya Hija



Maandalizi ya Hija hayaanzii kwenye miezi ya Hija, bali huanzia mbali katika umri wa mtu. Tunafahamu kuwa utekelezaji wa Ibada ya Hija unahitaji kuwa na uwezo wa kifedha (kimali). Hivyo Muislamu wa kweli katika kuchuma na kutumia mali yake, hana budi kuzingatia suala la nguzo ya Zaka na nguzo ya Hija. Muislamu atakapoweka mbele yake wazo la kutoa Zaka na Kuhiji, daima atachunga mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuchuma kwake, kwani anafahamu wazi kuwa mali iliyochumwa kwa njia za haramu haifai kutolea Zaka au Kuhijia. Hebu tuzingatie hadithi ifuatayo:



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Swala haikubaliwi bila ya Twahara, wala Sadaqa haikubaliwi kama inatolewa kutokana na mali iliyochumwa kwa njia za haramu. (Muslim).



Halikadhalika, kutokana na hadithi hii, Hija haitasihi endapo mtu atahiji kwa kutumia mali iliyopatikana kwa njia za haramu. Hivyo, fikra ya kuhiji, humzoesha Muumini kuchunga mipaka ya Mwenyezi Mungu katika uchumi.



Pia fikra ya Hija humzoesha Muumini kutumia mali yake kwenye mambo muhimu tu ili kumuwezesha kuweka akiba kwa ajili ya Hija. Yaani fikra ya kutekeleza nguzo hii, humuepusha na ubadhirifu au utumiaji bila ya haja na bila ya ratiba.



Mtu anayekusudia kuhiji azidishe kutenda wema. Ajizatiti katika kusimamisha swala tano, kutoa Zaka, kufunga Ramadhani, kuwahurumia wanyonge kwa kuwapa misaada wanayohitajia na kusuhubiana vizuri na watu wote kwa ujumla. Amuombe msamaha kila aliyemkosea na amsamehe kila aliyemkosea. Pia mwenye kunuia Hija anatakiwa ajitahidi kujiepusha na maovu na azidishe kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa yote aliyokosea kwa kujua au kutojua na yaliyowazi au yaliyofichikana. Katika Qur-an Mwenyezi Mungu (s.w) anaagiza kwa wanaokusudia kuhiji:


β€œNa anayekusudia kufanya Hija katika miezi hiyo, basi asiseme maneno machafu, wala asifanye vitendo vichafu wala asibishane katika hiyo Hija. Na kheri yoyote mnayoifanya Mw enyezi Mungu anajua …” (2:197)



Utaona mtu mwenye fikra ya kutekeleza ibada ya Hija daima atakuwa mwangalifu katika mwenendo wake wa kila siku. Atajitahidi kutekeleza maamrisho yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kujiepusha na makatazo yake yote atajitahidi kuwatendea wema wanaadamu wenzake na kila mara atakuwa mwenye kujiandaa kuitika mwito wa Mola wake (Labbayka), kama vile mtu anayejiandaa kukutana na Mola wake kwa kifo, muda mfupi ujao.






                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1522

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 web hosting   

Post zinazofanana:

Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu

Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.

Soma Zaidi...
Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu

Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
mambo yanayofungua swaumu

post hii ijakwenda kukufundisha mambo yanayoharibu funga

Soma Zaidi...
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...