Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Kumkafini (Kumvisha Sanda) Maiti.
- Ni sunnah kutumia nguo nyeupe.
‘Ibn Abbas amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:
“Vaeni nguo nyeupe, kwa sababu hili ni vazi lenu lililo bora kuliko yote, na wakafinini maiti wenu kwa nguo (nyeupe)”
(Abu Daud, Tirmidh na Ibn Majah)
- Pia sanda isiwe nguo ya gharama.
‘Ali (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Msigharamie sana nguo za sanda, kwani inakwenda kuozeana (kaburini)”
(Abu Daud)
- Hajji akifa akiwa katika vazi la Ihram (Hija), vazi hilo ndio litakuwa sanda yake.
‘Abdullah bin Abbas amesimulia kuwa mtu mmoja alikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) ngamia wake alimkanyaga, wakati akiwa anahiji mpaka akafa, Mtume wa Allah akasema:
“Muosheni na maji na majani ya mkunazi na mumkafini kwa hayo mashuka yake mawili, msimpake manukato na msimfunike kichwa chake …….”
(Bukhari na Muslim )
- Ukubwa wa sanda unategemeana na ukubwa wa maiti.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo
Soma Zaidi...Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.
Soma Zaidi...Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.
Soma Zaidi...