Kumkafini (kumvisha sanda maiti)
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Kumkafini (Kumvisha Sanda) Maiti.
- Mazingatio juu ya Sanda.
- Ni sunnah kutumia nguo nyeupe.
‘Ibn Abbas amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:
“Vaeni nguo nyeupe, kwa sababu hili ni vazi lenu lililo bora kuliko yote, na wakafinini maiti wenu kwa nguo (nyeupe)”
(Abu Daud, Tirmidh na Ibn Majah)
- Pia sanda isiwe nguo ya gharama.
‘Ali (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Msigharamie sana nguo za sanda, kwani inakwenda kuozeana (kaburini)”
(Abu Daud)
- Hajji akifa akiwa katika vazi la Ihram (Hija), vazi hilo ndio litakuwa sanda yake.
‘Abdullah bin Abbas amesimulia kuwa mtu mmoja alikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) ngamia wake alimkanyaga, wakati akiwa anahiji mpaka akafa, Mtume wa Allah akasema:
“Muosheni na maji na majani ya mkunazi na mumkafini kwa hayo mashuka yake mawili, msimpake manukato na msimfunike kichwa chake …….”
(Bukhari na Muslim )
- Ukubwa wa sanda unategemeana na ukubwa wa maiti.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 ai web app 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Mafunzo ya swala
Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?
Soma Zaidi...Mifano na namna ya kurithisha
Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.
Soma Zaidi...Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...