Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Kumkafini (Kumvisha Sanda) Maiti.
- Ni sunnah kutumia nguo nyeupe.
‘Ibn Abbas amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:
“Vaeni nguo nyeupe, kwa sababu hili ni vazi lenu lililo bora kuliko yote, na wakafinini maiti wenu kwa nguo (nyeupe)”
(Abu Daud, Tirmidh na Ibn Majah)
- Pia sanda isiwe nguo ya gharama.
‘Ali (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Msigharamie sana nguo za sanda, kwani inakwenda kuozeana (kaburini)”
(Abu Daud)
- Hajji akifa akiwa katika vazi la Ihram (Hija), vazi hilo ndio litakuwa sanda yake.
‘Abdullah bin Abbas amesimulia kuwa mtu mmoja alikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) ngamia wake alimkanyaga, wakati akiwa anahiji mpaka akafa, Mtume wa Allah akasema:
“Muosheni na maji na majani ya mkunazi na mumkafini kwa hayo mashuka yake mawili, msimpake manukato na msimfunike kichwa chake …….”
(Bukhari na Muslim )
- Ukubwa wa sanda unategemeana na ukubwa wa maiti.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii
Soma Zaidi...