Haya ndio yanayobatilisha Hija

Haya ndio yanayobatilisha Hija

Kubatilika kwa Hija
Hija itabatilika iwapo Haji ataacha kutekeleza moja wapo ya matendo yafuatayo:



(i) Ihram au nia ya Hija na kuwa katika hali ya Ihram ikiwa ni pamoja na vazi lake kwa wanaume na kuchunga masharti ya Ihram. Mtu akivunja masharti ya Ihram Hija haibatiliki lakini analazimika kufidia kwa kuchinja mnyama au kulisha maskini au kufunga. Ila kufanya tendo la ndoa ndani ya Ihram hubatilisha Hija kabisa.
Sa’i kati ya Safaa na Marwa.



(ii) Kuhudhuria katika uwanja wa Arafat siku ya mwezi 9 Dhul- Hija kati ya kuchomoza jua la mwezi 9 dhul-Hija na alfajir ya mwezi10 Dhul-Hija.



(iii) Tawaful Ifadha (Tawafu ya Nguzo).


Lengo la Hija
Kama tulivyojifunza katika masomo yaliyopita, lengo la ujumla la kuamrishwa kusimamisha nguzo tano za Uislamu, Shahada, kusimamisha Swala, Kutoa Zaka, Kufunga Ramadhani na Kuhiji Makka - ni kumuandaa mja aweze kuishi kulingana na lengo la kuumbwa kwake na kuletwa hapa duniani. Lengo la kuumbwa mwanaadamu limebainishwa katika Qur-an kuwa ni kumwabudu Allah(s.w.) katika kila kipengele cha maisha yake (Rejea Qur’an 51:56).



Ibada ya Hijja ni kilele au ni Chuo Kikuu cha kukamilisha maandalizi ya kumfikisha Muumini katika lengo la kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha na kumuwezesha Muumini kuisimamisha dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa juu ya dini zote.



Namna Hija inavyomuandaa Muumini kuwa Khalifa waAllah katika jamii
Katika sehemu hii tutaangalia falsafa ya kila kitendo cha Ibada ya Hija kuanzia maandalizi ya safari mpaka mwisho wa safari na kuonesha namna ya kila kitendo cha Hijja kinavyomuandaa mja kuwa mcha-Mungu aliyetayari kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa hali na mali.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1201

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa

Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoharibu swala yaani yanayobatilisha swala.

Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake

Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Haki za raia katika dola ya kiislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii

(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi.

Soma Zaidi...
Mafungu ya mirathi katika uislamu

Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1.

Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo 17 za swala.

Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.

Soma Zaidi...