Kubatilika kwa Hija
Hija itabatilika iwapo Haji ataacha kutekeleza moja wapo ya matendo yafuatayo:
(i) Ihram au nia ya Hija na kuwa katika hali ya Ihram ikiwa ni pamoja na vazi lake kwa wanaume na kuchunga masharti ya Ihram. Mtu akivunja masharti ya Ihram Hija haibatiliki lakini analazimika kufidia kwa kuchinja mnyama au kulisha maskini au kufunga. Ila kufanya tendo la ndoa ndani ya Ihram hubatilisha Hija kabisa.
Sa’i kati ya Safaa na Marwa.
(ii) Kuhudhuria katika uwanja wa Arafat siku ya mwezi 9 Dhul- Hija kati ya kuchomoza jua la mwezi 9 dhul-Hija na alfajir ya mwezi10 Dhul-Hija.
(iii) Tawaful Ifadha (Tawafu ya Nguzo).
Lengo la Hija
Kama tulivyojifunza katika masomo yaliyopita, lengo la ujumla la kuamrishwa kusimamisha nguzo tano za Uislamu, Shahada, kusimamisha Swala, Kutoa Zaka, Kufunga Ramadhani na Kuhiji Makka - ni kumuandaa mja aweze kuishi kulingana na lengo la kuumbwa kwake na kuletwa hapa duniani. Lengo la kuumbwa mwanaadamu limebainishwa katika Qur-an kuwa ni kumwabudu Allah(s.w.) katika kila kipengele cha maisha yake (Rejea Qur’an 51:56).
Ibada ya Hijja ni kilele au ni Chuo Kikuu cha kukamilisha maandalizi ya kumfikisha Muumini katika lengo la kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha na kumuwezesha Muumini kuisimamisha dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa juu ya dini zote.
Namna Hija inavyomuandaa Muumini kuwa Khalifa waAllah katika jamii
Katika sehemu hii tutaangalia falsafa ya kila kitendo cha Ibada ya Hija kuanzia maandalizi ya safari mpaka mwisho wa safari na kuonesha namna ya kila kitendo cha Hijja kinavyomuandaa mja kuwa mcha-Mungu aliyetayari kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa hali na mali.
Umeionaje Makala hii.. ?
Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Funga inavyomuandaa mtu kuwa mcha-Mungu.
Soma Zaidi...Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili.
Soma Zaidi...Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir
Soma Zaidi...