Haya ndio yanayobatilisha Hija
Kubatilika kwa Hija
Hija itabatilika iwapo Haji ataacha kutekeleza moja wapo ya matendo yafuatayo:
(i) Ihram au nia ya Hija na kuwa katika hali ya Ihram ikiwa ni pamoja na vazi lake kwa wanaume na kuchunga masharti ya Ihram. Mtu akivunja masharti ya Ihram Hija haibatiliki lakini analazimika kufidia kwa kuchinja mnyama au kulisha maskini au kufunga. Ila kufanya tendo la ndoa ndani ya Ihram hubatilisha Hija kabisa.
Saβi kati ya Safaa na Marwa.
(ii) Kuhudhuria katika uwanja wa Arafat siku ya mwezi 9 Dhul- Hija kati ya kuchomoza jua la mwezi 9 dhul-Hija na alfajir ya mwezi10 Dhul-Hija.
(iii) Tawaful Ifadha (Tawafu ya Nguzo).
Lengo la Hija
Kama tulivyojifunza katika masomo yaliyopita, lengo la ujumla la kuamrishwa kusimamisha nguzo tano za Uislamu, Shahada, kusimamisha Swala, Kutoa Zaka, Kufunga Ramadhani na Kuhiji Makka - ni kumuandaa mja aweze kuishi kulingana na lengo la kuumbwa kwake na kuletwa hapa duniani. Lengo la kuumbwa mwanaadamu limebainishwa katika Qur-an kuwa ni kumwabudu Allah(s.w.) katika kila kipengele cha maisha yake (Rejea Qurβan 51:56).
Ibada ya Hijja ni kilele au ni Chuo Kikuu cha kukamilisha maandalizi ya kumfikisha Muumini katika lengo la kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) katika kila kipengele cha maisha na kumuwezesha Muumini kuisimamisha dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa juu ya dini zote.
Namna Hija inavyomuandaa Muumini kuwa Khalifa waAllah katika jamii
Katika sehemu hii tutaangalia falsafa ya kila kitendo cha Ibada ya Hija kuanzia maandalizi ya safari mpaka mwisho wa safari na kuonesha namna ya kila kitendo cha Hijja kinavyomuandaa mja kuwa mcha-Mungu aliyetayari kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa hali na mali.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Kitabu cha Afya π3 ai web app π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 web hosting π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Makosa Yanayofanywa Wakati wa Swala
Swala ni nguzo ya pili ya Uislamu baada ya Shahada na ni ibada ya kwanza ambayo mja atahisabiwa nayo Siku ya Kiyama. Kwa sababu ya umuhimu wake mkubwa, Muislamu anatakiwa kuiswali kwa usahihi kulingana na mafundisho ya Mtume Muhammad (Swalla Allahu Alayhi Wasallam). Hata hivyo, watu wengi hufanya makosa mbalimbali wakati wa swala, mengine kwa kutokujua na mengine kutokana na uzembe. Makosa haya yanaweza kupunguza thawabu za swala au hata kuifanya swala kuwa batili. Katika makala hii tutajifunza makosa ya kawaida yanayofanywa wakati wa swala, madhara yake, na namna ya kuyarekebisha.
Soma Zaidi...Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na ubinaadamu wao.
Soma Zaidi...Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga.
Soma Zaidi...