Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika


image


Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa.


Mali yenye kuchangiwa mtaji kwa hisa

Mtu akishaamua kuuza hisa (share) kwa watu wengine kwa ajili ya mali fulani katika sheria ya Kiislamu anapoteza umilikaji wa mali wa mtu mmoja. Kuuza hisa kwa wengine kwa maana nyingine ni kukaribisha watu wengine kushiriki katika umilikaji wa mali ile. Nafasi ya mtu katika kumiliki mali hiyo itategemea idadi ya hisa alizonazo katika mali ile. Wenye hisa inabidi washirikiane katika faida na hasara pamoja na gharama za uendeshaji.

 

Faida anazopata atakayekuwa mwenye kumiliki mali
Zipo faida kadhaa ambazo atakayekuwa mwenye kumiliki mali huzipata kwa kufuata ushirika katika biashara, mtaji na faida (Shared Equity and rental) badala ya kupata mikopo ya biashara yenye riba. Faida kubwa atakayopata ni fadhila za Allah (s.w.) kwa kule kuepuka kwake kutoa riba kwa mkopo atakaopata. Tunajifunza katika Hadithi za Mtume (s.a.w.) kuwa laana ya Allah (s.w.) huwafikia wote wanaohusika na riba (mtoaji, mpokeaji, shahidi). Hata hivyo kuna faida nyingine ambazo anaweza kuzipata:

 


(i) Atakayekuwa mwenye kumiliki mali kwa kutochukuwa mkopo wenye masharti ya riba hujiepusha kabisa na hatari ya kunyang’anywa mali yake (aliyoweka rahani) akishindwa kutimiza masharti yake.

 


(ii)Fedha ambayo angeitoa kama riba kwa ajili ya mkopo atabaki nayo na kutumia kwa shughuli nyingine kuendeshea maisha yake.

 


(iii)Atakuwa na uhakika wa kupata sehemu halali ya faida inayotokana na mali hiyo (kama ipo). Kadhalika kama ikitokea hasara haitamlazimu kubeba mzigo wote wa hasara kwani ushirika katika biashara huhusisha vile vile umuhimu wa kugawana hasara itokeapo.

 


Faida kwa wenye kununua hisa
Mwenye kununua hisa huchangia katika mtaji. Naye huepuka ghadhabu za Allah (s.w.) za utoaji mkopo kwa riba. Zaidi ya haya hupata faida zifuatazo:

 


(i) Hupata sehemu ya faida itokanayo na mali hiyo kulingana na mchango wake kwenye biashara (idadi ya hisa alizonazo).

 

(ii) Huwa na sauti kwenye mali kwani naye pia ni mwenye kumiliki mali ile mpaka atakapouza hisa zake. Isitoshe hutoa kiwango kidogo kujipatia haki ya kumiliki ukilinganisha na mtaji mzima.

 


Kwa ujumla jamii nzima itanufaika kwa kuacha mfumo wa mikopo kwa riba na kuhimiza watu kufanya ushirika katika biashara. Ilivyo waliokopeshana kwa riba hawawi katika uhusiano mzuri kiroho. Aliyekopeshwa ilimbidi kufanya hivyo kutokana na shida aliyokuwa nayo. Kutoa kwake riba anakufanya kwa kuwa anafahamu hatari za kutofanya hivyo (kupoteza mali yake) ingawa kitendo hicho kinamuuma sana rohoni. Hivyo urafiki kati ya mkopeshaji na mkopeshwaji huwa ni wa kinafiki. Jambo hili ni wazi sana katika jamii ya dunia ya sasa. Hebu fikiria athari za mikopo hii kwa nchi masikini duniani. Ni mara nyingi nchi masikini zimekuwa zikipiga kelele aidha kupunguziwa au kufutiwa kabisa baadhi ya madeni yao. Sehemu kubwa ya madeni hayo ni limbikizo la riba la miaka mingi.

 


Hivyo Uislamu unapiga vita riba kutokana na madhara yake kibinafsi, kitaifa na kimataifa. Aidha Uislamu unahimiza ushirikiano katika biashara kama ufumbuzi wa tatizo la riba.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

image Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

image Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu
Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu. Soma Zaidi...

image Hadathi ya kati na kati
Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati. Soma Zaidi...

image Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali. Soma Zaidi...

image Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma
Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma. Soma Zaidi...

image Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

image Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga. Soma Zaidi...

image Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu
Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo Soma Zaidi...

image Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala. Soma Zaidi...