Kusimamisha swala.

Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.

 

6.3.Kusimamisha Swala.

 Kisheria: Ni maombi maalum kwa Allah (s.w) kwa kutekeleza nguzo na masharti maalumu kupitia mafundisho ya Mtume (s.a.w).

Maana ya Kuswali.

-     Ni kufanya (kutekeleza) matendo ya swala kama vile; kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, kusoma dhikiri, n.k.

-     Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo na sharti zote za swala, kuwa na unyenyekevu (khushui) na kudumu nayo maishani.

      Rejea Qur’an (107:4-5), (23:1-2), (23:9), (70:23) na (19:31).

Ni mambo ya lazima kuchungwa na kutekelezwa na muislam kabla hajaanza kuswali

  1. Twahara.
  2. Sitara
  3. Kuchunga Wakati.
  4. Kuelekea Qibla.
  1. Twahara.

Maana ya Twahara

Kilugha: - Ni utakaso au

-  Ni usafi wa nje unaohusiana mwili na nguo na wa ndani unaohusiana   na nafsi

 

Kisheria: - Ni usafi wa roho, mwili na nguo. 

-  Ni kujitakasa kwa kujieepusha na kila aina ya najisi na hadath (uchafu).

                                         Rejea Qur’an (2:222), (9:108)

                      

      -     Mtu aliyetakasika ni yule aliyejitwaharisha na kila aina ya najisi na hadath katika mwili, nguo na nafsi kutokana na shirki, kibri, ukafiri, dharau, n.k.

 

-  Najisi maana yake ni uchafu.

-  Baadhi ya vitu vilivyonajisi ni:

  1. Haja ndogo na kubwa ya binaadamu au mnyama.
  2. Damu             
  3. Usaha             
  4. Matapishi
  5. Pombe aina zote           
  6. Mzoga wowote isipokuwa wa binaadamu, samaki na nzige na jamii yake.    
  7. Maziwa ya mnyama asiyeliwa mfano: punda wa nyumbani, farasi, n.k.     
  8. Kiungo cha mnyama kilichokatwa na hali yuko hai, mfano; mkia wa kondoo, n.k. 
  9. Mbwa na nguruwe na kila kinachotokana nao.

 

 

Tunajitwaharisha kutokana na najisi na hadathi kwa kutumia;

 

  1. Maji safi.

-    Ni yale yanayofaa kujitwaharishia.

Makundi ya maji safi.

1.Maji Mutlaq (maji ya asili)

-  Ni maji yanayofaa kujitwaharishia yaliyo katika asili yake katika rangi, ladha na harufu. Mfano; maji ya kisima, chem chem, mito, maziwa, n.k.

 

2.Maji mengi.

-  Ni maji yaliyokusanywa au yaliyokusanyika yenye ujazo wa kuanzia ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’

 

-  Maji mengi hayaharibiki kwa kujitwarishia ndani au kuingiwa na najisi ila yakibadilika rangi, harufu au ladha yake.

 

3.Maji machache.

-     Ni maji yenye ujazo chini ya ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’.

Mfano: maji ya vidimbwi, ndoo, mtungi, n.k.

 

-     Maji haya huharibika na kutofaa kujitwaharishia iwapo;

 

4.Maji makombo.

-     Ni maji yaliyonyewa na binaadamu au mnyama (asiye najisi) na kubakishwa. Maji haya yanafaa kujitwaharishia pia.

 

5.Udongo Safi.

-    Ni ule ulioepukana na najisi (uchafu) na uko katika asili yake usiochanganyikana na majivu, vumbi la mkaa au mbao, unga, n.k.

 

Rejea Hadith EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 69-72.

 

  1. Najisi kubwa.

-     Ni najisi inayotokana na mbwa na nguruwe.

-     Imeitwa hivyo kutokana na uzito wa kujitwaharisha kwayo.

-     Namna ya kutwaharisha paliponajisika ni kuosha mara saba osho (kosho) mojawapo kwa kutumia mchanga (udongo) safi.

 

2.Najisi ndogo.

-    Ni aina zote za najisi isipokuwa ya mbwa na nguruwe.

-     Namna ya kujitwaharisha /kutwaharisha penye najisi ni kuosha kwa maji safi mpaka patakate kwa kuondoka harufu na rangi ya najisi.

 

3.Najisi hafifu.

-     Ni mkojo wa mtoto mchanga wa kiume ambaye hajaanza kula chakula isipokuwa kunyonya maziwa ya mama tu.

-     Imetwa hivyo kutokana na uhafifu wa kujitwaharisha kwayo.

 

-     Namna ya kujitwaharisha ni kumwagia maji safi paliponajisika bila ya kusugua.

-     Ni uchafu wa kihali (kinafsi) usiomruhusu mtu kuswali au kutufu Ka’abah.

 

 

1.Hadath ndogo

-    Ni hali ya kutokuwa na udhu.

-     Hali hii huondoka kwa kutia udhu kamili kwa kuzingatia masharti na nguzo za udhu kama ifuatavyo;

 

  1. Kuwa na maji safi na ya kutosha kuweza kutiririka kwenye viungo vya udhu na sio kupakazwa.
  2. Kutokuwa na kitu kilichogandamana na kinachozuia maji kupenya kwenye ngozi katika viungo vya udhu kama ulimbo, lami, rangi, n.k.
  3. Kutokuwa na vumbi au uchafu wowote unaoweza kubadili rangi na ladha ya maji unapotia udhu.
  4. Kuondoa kila aina yoyete ya najisi juu ya viungo vya udhu kabla ya kuanza kutawadha.
  5. Kutokuwa (kukata) kucha ndefu.

 

  1. Kutia nia moyoni kuwa unatwadha.
  2. Kuosha uso kikamilifu.
  3. Kuosha mikono miwili mpaka vifundoni.
  4. Kupaka maji kichwani.
  5. Kuosha miguu miwili mpaka vifundoni (kongo mbili).
  6. Kufuata utaratibu huu (i – v) kwa mfuatano.

Rejea Qur’an (5:6).

 

  1. Kupiga mswaki kabla ya kuanza kutawadha.
  2. Kuanza kutawadha kwa kuosha viganja vya mikono kwa kusema “Bismillaah
  3. Kusukutua na kupandisha maji puani.
  4. Kupaka maji shingoni wakati wa kupaka kichwani.
  5. Kuosha masikio mara tu baada ya kupuka maji kichwani.
  6. Kuosha kila kiungo cha udhu mara tatu.
  7. Kuanza kuosha viungo vya kulia kisha kushoto.
  8. Kuelekea Qibla na kuomba dua baada ya kutawadha.

Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 73-74.

 

  1. Kuswali.
  2. Kutufu (kuizunguka) Ka’abah.

 

  1. Kutokwa na kitu chochote katika utupu wa mbele au nyuma kama vile; upepo, maji maji, haja ndogo au kubwa, n.k.
  2. Kutokwa na fahamu kwa kulala au kusinzia bila kukaa kwa kumakinisha makalio ardhini.
  3. Kushika au kugusa sehemu za siri kwa kiganja cha mkono bila kizuizi chochote.
  4. Kugusana na mwanamke na kutokwa maji maji kwenye utupu kwa matamanio, vinginevyo udhu hautenguki.

 

2 .Hadathi ya kati na kati (Janaba).

-    Ni hali ya mtu kupatwa na Janaba kwa kufanya tendo la jimai (tendo la ndoa) au kutokwa na manii kwa kuota au namna nyingineyo.

 

Rejea Qur’an (4:43) na (5:6)

  1. Kuswali.
  2. Kutufu Ka’abah
  3. Kukaa msikitini
  4. Kuisoma Qur’an hata kimoyo moyo.

 

Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

“Wenye hedhi na wenye Janaba hawatasoma chochote kutoka kwenye Qur’an” (Tirmidh)

 

3.Hadathi Kubwa

-    Ni hali ya kupatwa hedhi (damu ya mwezi) au nifasi (damu ya uzazi) kwa wanawake tu.

 

  1. Kuswali au Kutufu Ka’abah
  2. Kukaa msikitini
  3. Kugusa au kubeba msahafu (ila kwa dharura sana)
  4. Kufunga
  5. Kufanya tendo la ndoa (jimai)
  6. Kutalikiwa (kupewa talaka)

 

-     Kujitwaharisha kutokana na Janaba na hedhi au nifasi ni kuoga kwa maji safi kwa kutekeleza masharti na nguzo za kuoga josho la wajibu kama ifuatavyo;

-    Masharti ya kuoga ni sawa na yale ya udhu.

-    Nguzo za kuoga ni mbili;

  1. Kutia nia moyoni kuwa unaoga
  2. Kueneza maji mwili mzima.

-     Ni kitendo cha kujitwaharisha kwa kutumia mchanga au udongo safi.

 

  1. Ugonjwa usioruhusu kutumia maji.
  2. Kuwa safarini na kukosa maji.
  3. Kuwa katika mazingira ya kizuizi (yasiyorusu) kutumia maji.
  4. Kukosekana maji.

Rejea Qur’an (5:6)

 

-  Ili tayammamu ikubalike lazima yazingatiwe masharti yafuatayo;

  1. Ipatikane dharura ya kutoruhusu kutumia maji katika kujitwaharisha.
  2. Pawe na hitajio la kutayammamu kama vile; kuswali, kutufu, n.k.
  3. Tayammamu ifanyike baada ya kutimia muda wa swala, kutufu, n.k.
  4. Pawepo na udongo safi, uliotwaharika, mkavu na wenye vumbi vumbi.

 

 

  1. Nia (kukusudia udongo safi)
  2. Kupaka uso
  3. Kupaka mikono
  4. Kufuata utaratibu huu (i-iii) kwa mfuatano

 

  1. Kufikwa na kila lenye kutengua udhu wa kawaida
  2. Kupatikana maji kabla ya kuswali au kutufu

 

2.Sitara

-     Ni sharti la pili la kusimamisha swala ambalo muislamu anatakiwa azingatie kabla kuanza kuswali.

      Rejea Qur’an (7:31) na (24:31)

 

-    Uchi wa mwanamume ni sehemu baina ya kitovu na magoti kisheria.

-     Katika hali ya kawaida muislamu anatakiwa kujisitiri na kujipamba kikamilifu wakati wa kuswali ila muda wa dharura tu.

-     Mwili wote wa mwanamke ni uchi, hivyo stara yake ni kujifunika mwili mzima isipokuwa uso na viganja vya mikono muda wa swala na wakati wote.

           

  1. Vazi la mwanamke lazima lifunike mwili mzima isipokuwa uso na viganja vya mikono.
  2. Vazi lazima lisibane na kuweza kuonesha ramani (viungo) ya mwili wa mwanamke.
  3. Vazi lazima liwe zito kiasi cha kutoweza kuonesha rangi ya ngozi au umbo la mwanamke.
  4. Vazi la mwanamke lisiwe la kuvutia sana kuweza kusababisha ushawishi kwa wanaume.
  5. Vazi la mwanamke lisiwe la kifahari sana la kuleta majivuno, kibri, kujiona, n.k.
  6. Vazi la mwanamke wa kiislamu lisifanane na vazi la mwanamume.

 

 

3.Kuchunga wakati

-     Hili ni sharti la tatu la kusimamisha swala.

-     Ibada ya swala za faradh kwa waislamu ni imepangiwa wakati maalumu.       

Rejea Qur’an (4:103), (2:187), n.k.

Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 87-93.

 

-     Swala za faradh ni tano;

  1. Adhuhuri – Ina rakaa 4, huingia baada ya kupinduka jua kuelekea magharibi.
  2. Alasir – Ina rakaa 4, huingia baada ya kuisha muda wa adhuhuri.
  3. Magh’rib – Ina rakaa 3, huanza mara baada ya kuzama jua.
  4. Ishaa – Ina rakaa 4, huanza baada ya kuingiza kiza halisi hadi alfajir.
  5. Alfajir – Ina rakaa 2, huanza mwisho wa usiku hadi kabla ya kuchomoza jua.

 

  1. Kuswali Sunnah baada ya swala ya Alfajir mpaka jua litakapochomoza.
  2. Wakati jua linachomoza.
  3. Wakati jua lipo katikati utosini
  4. Kuswali Sunnah baada ya swala ya Alasir
  5. Wakati wa kuzama jua

 

 

4.Kuelekea Qibla

-     Hili ni sharti la nne la kusimamisha swala.

-     Maana ya Qibla

Kilugha: Ni kukabili uelekeo au upande.

Kisheria: Ni uelekeo mahali ilipo nyumba tukufu ya Al-Ka’abah, Makkah - Saudia Arabia.

                       Rejea Qur’an (2:115), (2:149-150).

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/13/Thursday - 04:43:09 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1674


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hatua za kinga za ugumba na Utasa.
Ugumba ni 'ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa' kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba. Soma Zaidi...

Uhakiki wa hadithi za mtume
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mtume Muhammad alelewa na mama yake mzazi akiwa na umri wa miaka 4.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 8. Hapa utajifunza malezi ya Mtume kutokakwa Halimavkuja kwa mama yake. Soma Zaidi...

Mgawanyo wa Elimu Usiokubalika katika uislamu.
Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu. Soma Zaidi...

Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi. Soma Zaidi...

Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kumuamini mwenyezi Mungu..
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt Soma Zaidi...

Uchambuzi wa hadithi za mtume
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...