Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.
6.3.Kusimamisha Swala.
Kisheria: Ni maombi maalum kwa Allah (s.w) kwa kutekeleza nguzo na masharti maalumu kupitia mafundisho ya Mtume (s.a.w).
Maana ya Kuswali.
- Ni kufanya (kutekeleza) matendo ya swala kama vile; kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, kusoma dhikiri, n.k.
- Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo na sharti zote za swala, kuwa na unyenyekevu (khushui) na kudumu nayo maishani.
Rejea Qur’an (107:4-5), (23:1-2), (23:9), (70:23) na (19:31).
Ni mambo ya lazima kuchungwa na kutekelezwa na muislam kabla hajaanza kuswali
Maana ya Twahara
Kilugha: - Ni utakaso au
- Ni usafi wa nje unaohusiana mwili na nguo na wa ndani unaohusiana na nafsi
Kisheria: - Ni usafi wa roho, mwili na nguo.
- Ni kujitakasa kwa kujieepusha na kila aina ya najisi na hadath (uchafu).
Rejea Qur’an (2:222), (9:108)
- Mtu aliyetakasika ni yule aliyejitwaharisha na kila aina ya najisi na hadath katika mwili, nguo na nafsi kutokana na shirki, kibri, ukafiri, dharau, n.k.
- Najisi maana yake ni uchafu.
- Baadhi ya vitu vilivyonajisi ni:
Tunajitwaharisha kutokana na najisi na hadathi kwa kutumia;
- Ni yale yanayofaa kujitwaharishia.
Makundi ya maji safi.
1.Maji Mutlaq (maji ya asili)
- Ni maji yanayofaa kujitwaharishia yaliyo katika asili yake katika rangi, ladha na harufu. Mfano; maji ya kisima, chem chem, mito, maziwa, n.k.
2.Maji mengi.
- Ni maji yaliyokusanywa au yaliyokusanyika yenye ujazo wa kuanzia ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’
- Maji mengi hayaharibiki kwa kujitwarishia ndani au kuingiwa na najisi ila yakibadilika rangi, harufu au ladha yake.
3.Maji machache.
- Ni maji yenye ujazo chini ya ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’.
Mfano: maji ya vidimbwi, ndoo, mtungi, n.k.
- Maji haya huharibika na kutofaa kujitwaharishia iwapo;
4.Maji makombo.
- Ni maji yaliyonyewa na binaadamu au mnyama (asiye najisi) na kubakishwa. Maji haya yanafaa kujitwaharishia pia.
5.Udongo Safi.
- Ni ule ulioepukana na najisi (uchafu) na uko katika asili yake usiochanganyikana na majivu, vumbi la mkaa au mbao, unga, n.k.
Rejea Hadith EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 69-72.
- Ni najisi inayotokana na mbwa na nguruwe.
- Imeitwa hivyo kutokana na uzito wa kujitwaharisha kwayo.
- Namna ya kutwaharisha paliponajisika ni kuosha mara saba osho (kosho) mojawapo kwa kutumia mchanga (udongo) safi.
2.Najisi ndogo.
- Ni aina zote za najisi isipokuwa ya mbwa na nguruwe.
- Namna ya kujitwaharisha /kutwaharisha penye najisi ni kuosha kwa maji safi mpaka patakate kwa kuondoka harufu na rangi ya najisi.
3.Najisi hafifu.
- Ni mkojo wa mtoto mchanga wa kiume ambaye hajaanza kula chakula isipokuwa kunyonya maziwa ya mama tu.
- Imetwa hivyo kutokana na uhafifu wa kujitwaharisha kwayo.
- Namna ya kujitwaharisha ni kumwagia maji safi paliponajisika bila ya kusugua.
- Ni uchafu wa kihali (kinafsi) usiomruhusu mtu kuswali au kutufu Ka’abah.
1.Hadath ndogo
- Ni hali ya kutokuwa na udhu.
- Hali hii huondoka kwa kutia udhu kamili kwa kuzingatia masharti na nguzo za udhu kama ifuatavyo;
Rejea Qur’an (5:6).
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 73-74.
2 .Hadathi ya kati na kati (Janaba).
- Ni hali ya mtu kupatwa na Janaba kwa kufanya tendo la jimai (tendo la ndoa) au kutokwa na manii kwa kuota au namna nyingineyo.
Rejea Qur’an (4:43) na (5:6)
Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Wenye hedhi na wenye Janaba hawatasoma chochote kutoka kwenye Qur’an” (Tirmidh)
3.Hadathi Kubwa
- Ni hali ya kupatwa hedhi (damu ya mwezi) au nifasi (damu ya uzazi) kwa wanawake tu.
- Kujitwaharisha kutokana na Janaba na hedhi au nifasi ni kuoga kwa maji safi kwa kutekeleza masharti na nguzo za kuoga josho la wajibu kama ifuatavyo;
- Masharti ya kuoga ni sawa na yale ya udhu.
- Nguzo za kuoga ni mbili;
- Ni kitendo cha kujitwaharisha kwa kutumia mchanga au udongo safi.
Rejea Qur’an (5:6)
- Ili tayammamu ikubalike lazima yazingatiwe masharti yafuatayo;
2.Sitara
- Ni sharti la pili la kusimamisha swala ambalo muislamu anatakiwa azingatie kabla kuanza kuswali.
Rejea Qur’an (7:31) na (24:31)
- Uchi wa mwanamume ni sehemu baina ya kitovu na magoti kisheria.
- Katika hali ya kawaida muislamu anatakiwa kujisitiri na kujipamba kikamilifu wakati wa kuswali ila muda wa dharura tu.
- Mwili wote wa mwanamke ni uchi, hivyo stara yake ni kujifunika mwili mzima isipokuwa uso na viganja vya mikono muda wa swala na wakati wote.
3.Kuchunga wakati
- Hili ni sharti la tatu la kusimamisha swala.
- Ibada ya swala za faradh kwa waislamu ni imepangiwa wakati maalumu.
Rejea Qur’an (4:103), (2:187), n.k.
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 87-93.
- Swala za faradh ni tano;
4.Kuelekea Qibla
- Hili ni sharti la nne la kusimamisha swala.
- Maana ya Qibla
Kilugha: Ni kukabili uelekeo au upande.
Kisheria: Ni uelekeo mahali ilipo nyumba tukufu ya Al-Ka’abah, Makkah - Saudia Arabia.
Rejea Qur’an (2:115), (2:149-150).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Mwandhishi Tarehe 2022/01/13/Thursday - 04:43:09 pm Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1725
Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 Kitau cha Fiqh
👉3 kitabu cha Simulizi
👉4 Madrasa kiganjani
Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara Soma Zaidi...
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali. Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
ijuwe maawe maan ya kusimamisha swala
Soma Zaidi...
Haki ya Serikali kuzuia Dhulma
Soma Zaidi...
NAMNA YA KUSWALI SEHEMU YA KWANZA
Mtume (s. Soma Zaidi...
Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Umuhimu wa uchumi katika uislamu
2. Soma Zaidi...
Sheria Katika Uislamu
4. Soma Zaidi...
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada
Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s. Soma Zaidi...