Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.
6.3.Kusimamisha Swala.
Kisheria: Ni maombi maalum kwa Allah (s.w) kwa kutekeleza nguzo na masharti maalumu kupitia mafundisho ya Mtume (s.a.w).
Maana ya Kuswali.
- Ni kufanya (kutekeleza) matendo ya swala kama vile; kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, kusoma dhikiri, n.k.
- Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo na sharti zote za swala, kuwa na unyenyekevu (khushui) na kudumu nayo maishani.
Rejea Qur’an (107:4-5), (23:1-2), (23:9), (70:23) na (19:31).
Ni mambo ya lazima kuchungwa na kutekelezwa na muislam kabla hajaanza kuswali
Maana ya Twahara
Kilugha: - Ni utakaso au
- Ni usafi wa nje unaohusiana mwili na nguo na wa ndani unaohusiana na nafsi
Kisheria: - Ni usafi wa roho, mwili na nguo.
- Ni kujitakasa kwa kujieepusha na kila aina ya najisi na hadath (uchafu).
Rejea Qur’an (2:222), (9:108)
- Mtu aliyetakasika ni yule aliyejitwaharisha na kila aina ya najisi na hadath katika mwili, nguo na nafsi kutokana na shirki, kibri, ukafiri, dharau, n.k.
- Najisi maana yake ni uchafu.
- Baadhi ya vitu vilivyonajisi ni:
Tunajitwaharisha kutokana na najisi na hadathi kwa kutumia;
- Ni yale yanayofaa kujitwaharishia.
Makundi ya maji safi.
1.Maji Mutlaq (maji ya asili)
- Ni maji yanayofaa kujitwaharishia yaliyo katika asili yake katika rangi, ladha na harufu. Mfano; maji ya kisima, chem chem, mito, maziwa, n.k.
2.Maji mengi.
- Ni maji yaliyokusanywa au yaliyokusanyika yenye ujazo wa kuanzia ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’
- Maji mengi hayaharibiki kwa kujitwarishia ndani au kuingiwa na najisi ila yakibadilika rangi, harufu au ladha yake.
3.Maji machache.
- Ni maji yenye ujazo chini ya ndoo 12 au lita 240 au ‘Qulatain’.
Mfano: maji ya vidimbwi, ndoo, mtungi, n.k.
- Maji haya huharibika na kutofaa kujitwaharishia iwapo;
4.Maji makombo.
- Ni maji yaliyonyewa na binaadamu au mnyama (asiye najisi) na kubakishwa. Maji haya yanafaa kujitwaharishia pia.
5.Udongo Safi.
- Ni ule ulioepukana na najisi (uchafu) na uko katika asili yake usiochanganyikana na majivu, vumbi la mkaa au mbao, unga, n.k.
Rejea Hadith EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 69-72.
- Ni najisi inayotokana na mbwa na nguruwe.
- Imeitwa hivyo kutokana na uzito wa kujitwaharisha kwayo.
- Namna ya kutwaharisha paliponajisika ni kuosha mara saba osho (kosho) mojawapo kwa kutumia mchanga (udongo) safi.
2.Najisi ndogo.
- Ni aina zote za najisi isipokuwa ya mbwa na nguruwe.
- Namna ya kujitwaharisha /kutwaharisha penye najisi ni kuosha kwa maji safi mpaka patakate kwa kuondoka harufu na rangi ya najisi.
3.Najisi hafifu.
- Ni mkojo wa mtoto mchanga wa kiume ambaye hajaanza kula chakula isipokuwa kunyonya maziwa ya mama tu.
- Imetwa hivyo kutokana na uhafifu wa kujitwaharisha kwayo.
- Namna ya kujitwaharisha ni kumwagia maji safi paliponajisika bila ya kusugua.
- Ni uchafu wa kihali (kinafsi) usiomruhusu mtu kuswali au kutufu Ka’abah.
1.Hadath ndogo
- Ni hali ya kutokuwa na udhu.
- Hali hii huondoka kwa kutia udhu kamili kwa kuzingatia masharti na nguzo za udhu kama ifuatavyo;
Rejea Qur’an (5:6).
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 73-74.
2 .Hadathi ya kati na kati (Janaba).
- Ni hali ya mtu kupatwa na Janaba kwa kufanya tendo la jimai (tendo la ndoa) au kutokwa na manii kwa kuota au namna nyingineyo.
Rejea Qur’an (4:43) na (5:6)
Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Wenye hedhi na wenye Janaba hawatasoma chochote kutoka kwenye Qur’an” (Tirmidh)
3.Hadathi Kubwa
- Ni hali ya kupatwa hedhi (damu ya mwezi) au nifasi (damu ya uzazi) kwa wanawake tu.
- Kujitwaharisha kutokana na Janaba na hedhi au nifasi ni kuoga kwa maji safi kwa kutekeleza masharti na nguzo za kuoga josho la wajibu kama ifuatavyo;
- Masharti ya kuoga ni sawa na yale ya udhu.
- Nguzo za kuoga ni mbili;
- Ni kitendo cha kujitwaharisha kwa kutumia mchanga au udongo safi.
Rejea Qur’an (5:6)
- Ili tayammamu ikubalike lazima yazingatiwe masharti yafuatayo;
2.Sitara
- Ni sharti la pili la kusimamisha swala ambalo muislamu anatakiwa azingatie kabla kuanza kuswali.
Rejea Qur’an (7:31) na (24:31)
- Uchi wa mwanamume ni sehemu baina ya kitovu na magoti kisheria.
- Katika hali ya kawaida muislamu anatakiwa kujisitiri na kujipamba kikamilifu wakati wa kuswali ila muda wa dharura tu.
- Mwili wote wa mwanamke ni uchi, hivyo stara yake ni kujifunika mwili mzima isipokuwa uso na viganja vya mikono muda wa swala na wakati wote.
3.Kuchunga wakati
- Hili ni sharti la tatu la kusimamisha swala.
- Ibada ya swala za faradh kwa waislamu ni imepangiwa wakati maalumu.
Rejea Qur’an (4:103), (2:187), n.k.
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 87-93.
- Swala za faradh ni tano;
4.Kuelekea Qibla
- Hili ni sharti la nne la kusimamisha swala.
- Maana ya Qibla
Kilugha: Ni kukabili uelekeo au upande.
Kisheria: Ni uelekeo mahali ilipo nyumba tukufu ya Al-Ka’abah, Makkah - Saudia Arabia.
Rejea Qur’an (2:115), (2:149-150).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...