swala ya tarawehe na namna ya kuiswali, rakaa zake na suna zake.

swala ya tarawehe na namna ya kuiswali, rakaa zake na suna zake.

5.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

swala ya tarawehe na namna ya kuiswali, rakaa zake na suna zake.

5. Swala ya Tarawehe
Swala ya Tarawehe ni miongoni mwa Sunnah zilizokokotezwa. Swala hii huswaliwa katika mwezi wa Ramadhan tu wakati wowote kati ya kipindi baada ya swala ya Isha na kuingia kwa swala ya Alfajiri. Umuhimu wa swala hii umedhihiri katika Hadithi ifuatayo:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akisisitiza swala ya usiku katika mwezi wa kufunga (Ramadhani), bila ya kuifaradhisha kwao. Alikuwa akisema: Atakaye swali katika usiku wa mwezi wa kufunga, akiwa na imani na akitarajia malipo (kutoka kwa Allah (s.w), dhambi zake zilizotangulia husamehewa. (Muslim)



Mtume (s.a.w) alikuwa akiswali Tarawehe katika sehemu ya pili ya usiku (katika wakati ule ule wa Tahajjud). Mtume (s.a.w) aliswali Tarawehe pamoja na masahaba katika jamaa siku tatu, kisha akaacha na akawa anaswalia nyumbani kwake kama tunavyofahamishwa katika Hadithi ifuatayo:



‘Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) alikwenda msikitini usiku na akaswalisha Tarawehe na watu wakaswali naye. Asubuhi watu wakasimuliana habari hiyo. Mtume (s.a.w) siku ya pili alikwenda kuswalisha watu wakajaa msikitini. Alifanya hivyo hivyo siku ya tatu. Asubuhi siku ya nne watu wakapeana habari na wakajazana zaidi msikitini kwa ajili ya sw ala ya Tarawehe lakini Mtume (s.a.w) hakw enda


kuswalisha. Baadhi ya watu walisema kwa sauti “swalah”, lakini Mtume (s.a.w) hakwenda msikitini mpaka Alfajir. Alipomaliza sw ala ya Alfajir aliwakabili watu na kuwaeleza: “Jambo lenu halikuwa limefichikana kwangu, lakini nilichelea kuwa kama ningaliendelea mfululizo na swala hiyo ya Tarawehe huenda ingalifanywa kuwa ni faradhi kwenu na huenda m ungalishindw a kuitekeleza ”. (Muslim)



Pamoja na Hadithi hii, pia Mtume (s.a.w) aliwasisitiza Waislamu kuswali swala za Sunnah majumbani mwao na kuwahakikishia kuwa kufanya hivyo kuna malipo makubwa zaidi. Swala ya Tarawehe iliendelea kuswaliwa na kila mtu nyumbani kwake katika kipindi chote cha Mtume (s.a.w) na kipindi cha Khalifa wake wa kwanza (Abu Bakar). Khalifa wa pili, Umar bin Khattab, alianzisha tena kuswali swala ya Tarawehe kwa jamaa msikitini kama inavyoendelea mpaka hivi leo.



Idadi ya Rakaa za Swala ya Tarawehe



Kumekuwepo na maelezo tofauti kuhusiana na idadi ya rakaa za Swala ya tarawehe kutoka kwa wanazuoni tofauti. Lakini kutokana na Hadithi iliyosimuliwa na Mama Aysha (r.a) na kupokelewa na Maimamu wa Hadithi, Mtume (s.a.w) hakupata kuswali zaidi ya rakaa 11 katika mwezi wowote ule. Hadithi ya Jabir (r.a) iliyopokelewa na Ibnu Khuzaimah na Ib n Hibban, Mtume ameripotiwa kuswali rakaa nane za tarawehe na rakaa tatu za witri pamoja na Masahaba wake na kisha siku iliyofuatia akawa hakutoka kwenda kusalisha.



Ama kuhusiana na kuswali rakaa ishirini, ni kweli kuwa Khalifa Umar, Uthman na Ali (r.a) waliswali kwa rakaa hizo. Imamu Ibnu Hibban amesema kuwa mwanzoni ilikuwa ni rakaa kumi na moja isipokuwa kisomo (kisimamo) kilikuwa kirefu kiasi cha watu kuchoka. Hivyo baadaye ikaamuliwa kuwa idadi ya rakaa iongezwe na kisomo kipunguzwe na kuwa cha wastani ingawaje jambo hili halikuingiza Swala ya Witri, kutoka hapo kwenye rakaa 20 ilifika kwa badhi ya wengine akiwemo Imamu Malik hadi rakaa 36 ikiwa kisomo kimezidi kufupishwa. Iliyo sunnah ni kuswali tarawehe kwa rakaa 11-8 za kisimamo cha usiku cha kawaida na rakaa 3 za witri. Kwa kuwa mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa Qur-an inahimizwa sana kuwa Waislamu wahitimishe Qur-an yote alau kwa kusoma juzuu moja kila siku. Tarawehe ni swala sawa na swala nyingine hivyo kusihi kwake kunafungamana na kupatikana khushui, masharti na nguzo zote za swala. Ama hizi tarawehe zinazoswaliwa katika misikiti mingi mbazo Imamu hupata sifa kwa kuswali mbio mbio pasipo na mazingatio wala utulivu ni kinyume kabisa na utaratibu wa swala. Watu wengi ambao huharakisha kumaliza swala ya tarawehe kwa kiasi cha kutokamilisha nguzo za swala hawapati malipo yoyote kutokana na swala zao. Bali kwa kuwa watu hawa wanaifanyia swala mchezo hapana cha kutarajia zaidi ya adhabu kali waliyoahidiwa na Allah (s.w):


“Basi adhabu itawathibitikia wanao swali, ambao wanapuuza swala zao”. (107:4-5)




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 6128

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Ijuwe swala ya Tawbah na jinsi ya kuiswali
Ijuwe swala ya Tawbah na jinsi ya kuiswali

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya sinnah ya tawba.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...
Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika

Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.

Soma Zaidi...
Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)
Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya swala
Ni nini maana ya swala

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.

Soma Zaidi...