Navigation Menu



Namna ya kulipa swaumu ya ramadhani na ni nani anatakiwa alipe

Namna ya kulipa swaumu ya ramadhani na ni nani anatakiwa alipe

Kulipia Ramadhani



Mtu anapodaiwa siku alizo kula katika mchana wa mwezi wa Ramadhani,au siku ambazo swaumu yake ilibatilika, si lazima azilipe mara tu baada ya Ramadhani, japo ni bora mtu kumaliza deni lake haraka. Tunafahamishwa katika Hadith kuwa Bibi β€˜Aysha (r.a) alikuwa akilipia Ramadhani katika mwezi wa Shaaban:



Aysha (r.a) ameeleza: β€œNilikuwa na madeni ya swaumu ya Ramadhani. Sikuweza kulipa kadha ila katika mwezi wa Shaaban. (Bukhari na Muslim).



Hali kadhalika si lazima mtu kulipa mfululizo siku zote anazodaiwa, bali anaweza kuzilipa kidogo kidogo kutokana na Hadith ifuatayo:



Ibn Umar (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema juu ya kulipa Ramadhani: (Mtu) akitaka na afarikishe; na akitaka na afululize. (Daru Qu tni).



Kama mtu amechelewa kulipa siku anazodaiwa mpaka Ramadhani nyingine ikaingia, basi kwanza ataifunga hiyo Ramadhani iliyomuingilia. Baadaye ndipo alipe hiyo deni yake wala halipi fidia; iwe kuchelewa huko ni kwa udhuru ama si kwa udhuru. Lakini ni vizuri zaidi kulipa siku anazodaiwa kabla ya kuingia Ramadhani nyingine.




                   


           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 945


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Jinsi ya kumuosha maiti wa kiislami mwanaume au mwanamke
Post hii inakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kumuosha maiti wa kiislamu Soma Zaidi...

Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...

Njia haramu za uchumi
Soma Zaidi...

Funga ya ramadhan na nyinginezo
Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Umuhimu wa uchumi katika uislamu
2. Soma Zaidi...

Taratibu za ndoa ya kiislamu, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

namna ya kuswali
11. Soma Zaidi...

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu
Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Soma Zaidi...