JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma wazo hili:
Unatakiwa kutengeneza program ya chemsha bongo, ambapo program itauliza swali kisha mtu atatoajibu ndani ya sekunde 10 endapo hajaweka jibu ataambiwa muda umekwisha.
Sasa hapo ndipo tutahitani function ya ku set muda. Kufanya hivi kwa kutumia javascript tutatumia function unayoitaka setTimeout(). Jambo la kuzingatia ni kuwa muda hapa unahesabiwa kwa kutumia millsecond. sekunde 1 ni sawa na millsecond 1000. Hivyo ukitaka code zi fanye kazi baada ya dakika 5 hapo utaweka 5000. Sasa wacha tuone jinsi ambavyo tutaweza kuandika function yetu hii.
Kwanza utaweka function yako setTimeout() unaweza kuiweka ndani ya variable. Mfano var time = settimeout()
Pili ndani ya hiyo function utaweka statement zalo ukitengenisha na alama ya coma yaani (,) mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)},)
Tatu utaweka muda unaotaka baada ya hiyo koma. Mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)}, 5000).
Angalia mfano wa hapo chini
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
var myTimeout = setTimeout(function (){ document.write("Muda umekwisha")}, 5000)
</script>
</body>
Sasa endapo hujajaza jibu na muda ukiisha Utaletewa ujumbe huo.
Pia code hizo hapo unaweza kuzigeuza na kuziadika katika mtindo wa kuweka ku call function ndani ya setTimeout(). Matokeo ya code hizo hapo chini ni sawa na matokeo ya code hizo hapo juu.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
function quiz (){ document.write("Muda umekwisha")}
var myTimeout = setTimeout(quiz, 5000)
</script>
</body>
setInterval
Sasa ikitokea unahitaji ku excute code kila baada ya muda fulani hapa utatumia setinterval. Somo la hapo juu tumezungumzia ku excute code baada ya muda fuani, lakini hapa ni kila baada ya muda fulani.
Mfano:
Umetakiwa kuweka program ya kuesabu muda yaani sekunde. Kisha uweke kwenye program ya kuuliza swali. Hivyo itakuwa ukihesabu zikitimia sekunde flani in stop.
Kufanya hivi tutatumia function ya seti...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 ai web app 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript
Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.
Soma Zaidi...