Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma wazo hili:
Unatakiwa kutengeneza program ya chemsha bongo, ambapo program itauliza swali kisha mtu atatoajibu ndani ya sekunde 10 endapo hajaweka jibu ataambiwa muda umekwisha.
Sasa hapo ndipo tutahitani function ya ku set muda. Kufanya hivi kwa kutumia javascript tutatumia function unayoitaka setTimeout(). Jambo la kuzingatia ni kuwa muda hapa unahesabiwa kwa kutumia millsecond. sekunde 1 ni sawa na millsecond 1000. Hivyo ukitaka code zi fanye kazi baada ya dakika 5 hapo utaweka 5000. Sasa wacha tuone jinsi ambavyo tutaweza kuandika function yetu hii.
Kwanza utaweka function yako setTimeout() unaweza kuiweka ndani ya variable. Mfano var time = settimeout()
Pili ndani ya hiyo function utaweka statement zalo ukitengenisha na alama ya coma yaani (,) mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)},)
Tatu utaweka muda unaotaka baada ya hiyo koma. Mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)}, 5000).
Angalia mfano wa hapo chini
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
var myTimeout = setTimeout(function (){ document.write("Muda umekwisha")}, 5000)
</script>
</body>
Sasa endapo hujajaza jibu na muda ukiisha Utaletewa ujumbe huo.
Pia code hizo hapo unaweza kuzigeuza na kuziadika katika mtindo wa kuweka ku call function ndani ya setTimeout(). Matokeo ya code hizo hapo chini ni sawa na matokeo ya code hizo hapo juu.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
function quiz (){ document.write("Muda umekwisha")}
var myTimeout = setTimeout(quiz, 5000)
</script>
</body>
setInterval
Sasa ikitokea unahitaji ku excute code kila baada ya muda fulani hapa utatumia setinterval. Somo la hapo juu tumezungumzia ku excute code baada ya muda fuani, lakini hapa ni kila baada ya muda fulani.
Mfano:
Umetakiwa kuweka program ya kuesabu muda yaani sekunde. Kisha uweke kwenye program ya kuuliza swali. Hivyo itakuwa ukihesabu zikitimia sekunde flani in stop.
Kufanya hivi tutatumia function ya seti...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutaenda kujifunza namna ya kuhifadhi taarifa za mtumiaji endapo mtandao utakuwa haupo ()
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.
Soma Zaidi...Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka.
Soma Zaidi...