Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma wazo hili:
Unatakiwa kutengeneza program ya chemsha bongo, ambapo program itauliza swali kisha mtu atatoajibu ndani ya sekunde 10 endapo hajaweka jibu ataambiwa muda umekwisha.
Sasa hapo ndipo tutahitani function ya ku set muda. Kufanya hivi kwa kutumia javascript tutatumia function unayoitaka setTimeout(). Jambo la kuzingatia ni kuwa muda hapa unahesabiwa kwa kutumia millsecond. sekunde 1 ni sawa na millsecond 1000. Hivyo ukitaka code zi fanye kazi baada ya dakika 5 hapo utaweka 5000. Sasa wacha tuone jinsi ambavyo tutaweza kuandika function yetu hii.
Kwanza utaweka function yako setTimeout() unaweza kuiweka ndani ya variable. Mfano var time = settimeout()
Pili ndani ya hiyo function utaweka statement zalo ukitengenisha na alama ya coma yaani (,) mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)},)
Tatu utaweka muda unaotaka baada ya hiyo koma. Mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)}, 5000).
Angalia mfano wa hapo chini
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
var myTimeout = setTimeout(function (){ document.write("Muda umekwisha")}, 5000)
</script>
</body>
Sasa endapo hujajaza jibu na muda ukiisha Utaletewa ujumbe huo.
Pia code hizo hapo unaweza kuzigeuza na kuziadika katika mtindo wa kuweka ku call function ndani ya setTimeout(). Matokeo ya code hizo hapo chini ni sawa na matokeo ya code hizo hapo juu.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>
<form>
<label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>
<input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">
</form>
<script>
function quiz (){ document.write("Muda umekwisha")}
var myTimeout = setTimeout(quiz, 5000)
</script>
</body>
setInterval
Sasa ikitokea unahitaji ku excute code kila baada ya muda fulani hapa utatumia setinterval. Somo la hapo juu tumezungumzia ku excute code baada ya muda fuani, lakini hapa ni kila baada ya muda fulani.
Mfano:
Umetakiwa kuweka program ya kuesabu muda yaani sekunde. Kisha uweke kwenye program ya kuuliza swali. Hivyo itakuwa ukihesabu zikitimia sekunde flani in stop.
Kufanya hivi tutatumia function ya setinterval. kwa mfano hapo tutaset program ya kuhesabu kila baada ya millsecond 1000 maana kila baada ya dakika 1.
Kanuni za kuandika setInterval ni sawa na zile za kuandika setTimeout. Kikubwa cha kuzingatio ni kuwa timeInterval itakuwa inaendelea ku excute kila baada ya huo muda ulioweka bila ya kikomo mpaka pale utakapo fanya i stop.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<p id="showTime"></p>
<script>
var hesabu = 0;
var muda = setInterval(function (){
hesabu += 1;
document.getElementById("showTime").innerHTML = hesabu;
}, 1000);
</script>
</body>
Unaweza kuweka timeinterval zaidi ya moja kwenye code, pia unaweza kucanganya na setTimeout zaidi ya moja kweye ukurasa mmoja. Sasa kama nilivyo kueleza kuwa code zitaendelea ku excute kila baada ya muda fulani, mpaka utakapo sitisha kufanya hivyo.
Jinsi ya kusitisha timeInterval() na setTimeout():
ili kuweza kusitisha settimeout() tutatumia method hii clearTimeout() na ukitaka kusitisha setinterval() tutatumia method hii clearInterval()
Mfano 1: kusitisa setinterval
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
</html>
<body>
<p id="showTime"></p>
<button onclick="sitisha()">Sitisha Muda</button>
<script>
var hesabu = 0;
var muda = setInterval(function (){
hesabu += 1;
">...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...Ksomo hili litakwenda kukufundisha kuhusu object kwenye javascript, kazi zake na sheria zake katika kuiandika.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form.
Soma Zaidi...