JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.

Soma wazo hili: 

Unatakiwa kutengeneza program ya chemsha bongo,  ambapo program itauliza swali kisha mtu atatoajibu ndani ya sekunde 10 endapo hajaweka jibu ataambiwa muda umekwisha

 

Sasa hapo ndipo tutahitani function ya ku set muda. Kufanya hivi kwa kutumia javascript tutatumia function unayoitaka setTimeout(). Jambo la kuzingatia ni kuwa muda hapa unahesabiwa kwa kutumia millsecond. sekunde 1 ni sawa na millsecond 1000. Hivyo ukitaka code zi fanye kazi baada ya dakika 5 hapo utaweka 5000. Sasa wacha tuone jinsi ambavyo tutaweza kuandika function yetu hii.

 

Kwanza  utaweka function yako setTimeout()  unaweza kuiweka ndani ya variable. Mfano var time = settimeout()

Pili ndani ya hiyo function utaweka statement zalo ukitengenisha na alama ya coma yaani (,) mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)},) 

 

Tatu utaweka muda unaotaka baada ya hiyo koma. Mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)}, 5000).

 

Angalia mfano wa hapo chini

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>

<form>

 <label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>

 <input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">

</form>

 

<script>

 var myTimeout = setTimeout(function (){ document.write("Muda umekwisha")}, 5000)

</script>

</body>


 

Sasa endapo hujajaza jibu na muda ukiisha Utaletewa ujumbe huo. 

 

Pia code hizo hapo unaweza kuzigeuza na kuziadika katika mtindo wa kuweka ku call function ndani ya setTimeout(). Matokeo ya code hizo hapo chini ni sawa na matokeo ya code hizo hapo juu.

 

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>

<form>

 <label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>

 <input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">

</form>

 

<script>

 function quiz (){ document.write("Muda umekwisha")}

 var myTimeout = setTimeout(quiz, 5000)

</script>

</body>

 

setInterval

Sasa ikitokea unahitaji ku excute code kila baada ya muda fulani hapa utatumia setinterval. Somo la hapo juu tumezungumzia ku excute code baada ya muda fuani, lakini hapa ni kila baada ya muda fulani. 

 

Mfano:

Umetakiwa kuweka program ya kuesabu muda yaani sekunde. Kisha uweke kwenye program ya kuuliza swali. Hivyo itakuwa ukihesabu zikitimia sekunde flani in stop.

 

Kufanya hivi tutatumia function ya setinterval. kwa mfano hapo tutaset program ya kuhesabu kila baada ya millsecond 1000 maana kila baada ya dakika 1.

 

Kanuni za kuandika setInterval ni sawa na zile za kuandika setTimeout. Kikubwa cha kuzingatio ni kuwa timeInterval itakuwa inaendelea ku excute kila baada ya huo muda ulioweka bila ya kikomo mpaka pale utakapo fanya i stop.

 

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<p id="showTime"></p>

<script>

 var hesabu = 0;

 var muda = setInterval(function (){

   hesabu += 1;

   document.getElementById("showTime").innerHTML = hesabu;

 }, 1000);

</script>

</body>

 

Unaweza kuweka timeinterval zaidi ya moja kwenye code, pia unaweza kucanganya na setTimeout zaidi ya moja kweye ukurasa mmoja. Sasa kama nilivyo kueleza kuwa code zitaendelea ku excute kila baada ya muda fulani, mpaka utakapo sitisha kufanya hivyo.


 

Jinsi ya kusitisha timeInterval() na setTimeout():

ili kuweza kusitisha settimeout() tutatumia method hii clearTimeout() na ukitaka kusitisha setinterval() tutatumia method hii clearInterval()

 

Mfano 1: kusitisa setinterval

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<id="showTime"></p>

<button onclick="sitisha()">Sitisha Muda</button>

<script>

 var hesabu 0;

 var muda setInterval(function (){

   hesabu += 1...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 504

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

Soma Zaidi...
Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css

Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 18: Jinsi ya kutumia switch case kwenye javascript

Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript

Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...