image

JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.

Soma wazo hili: 

Unatakiwa kutengeneza program ya chemsha bongo,  ambapo program itauliza swali kisha mtu atatoajibu ndani ya sekunde 10 endapo hajaweka jibu ataambiwa muda umekwisha

 

Sasa hapo ndipo tutahitani function ya ku set muda. Kufanya hivi kwa kutumia javascript tutatumia function unayoitaka setTimeout(). Jambo la kuzingatia ni kuwa muda hapa unahesabiwa kwa kutumia millsecond. sekunde 1 ni sawa na millsecond 1000. Hivyo ukitaka code zi fanye kazi baada ya dakika 5 hapo utaweka 5000. Sasa wacha tuone jinsi ambavyo tutaweza kuandika function yetu hii.

 

Kwanza  utaweka function yako setTimeout()  unaweza kuiweka ndani ya variable. Mfano var time = settimeout()

Pili ndani ya hiyo function utaweka statement zalo ukitengenisha na alama ya coma yaani (,) mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)},) 

 

Tatu utaweka muda unaotaka baada ya hiyo koma. Mfano var time = settimeout(function() {Document.write(“Muda umekwisha”)}, 5000).

 

Angalia mfano wa hapo chini

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>

<form>

 <label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>

 <input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">

</form>

 

<script>

 var myTimeout = setTimeout(function (){ document.write("Muda umekwisha")}, 5000)

</script>

</body>


 

Sasa endapo hujajaza jibu na muda ukiisha Utaletewa ujumbe huo. 

 

Pia code hizo hapo unaweza kuzigeuza na kuziadika katika mtindo wa kuweka ku call function ndani ya setTimeout(). Matokeo ya code hizo hapo chini ni sawa na matokeo ya code hizo hapo juu.

 

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<h2>Jaza kitendawili hiki</h2>

<form>

 <label>Haba na haba hujaza _______________</label><br><br><br>

 <input type="text" placeholder="Jaza jibu hapa">

</form>

 

<script>

 function quiz (){ document.write("Muda umekwisha")}

 var myTimeout = setTimeout(quiz, 5000)

</script>

</body>

 

setInterval

Sasa ikitokea unahitaji ku excute code kila baada ya muda fulani hapa utatumia setinterval. Somo la hapo juu tumezungumzia ku excute code baada ya muda fuani, lakini hapa ni kila baada ya muda fulani. 

 

Mfano:

Umetakiwa kuweka program ya kuesabu muda yaani sekunde. Kisha uweke kwenye program ya kuuliza swali. Hivyo itakuwa ukihesabu zikitimia sekunde flani in stop.

 

Kufanya hivi tutatumia function ya setinterval. kwa mfano hapo tutaset program ya kuhesabu kila baada ya millsecond 1000 maana kila baada ya dakika 1.

 

Kanuni za kuandika setInterval ni sawa na zile za kuandika setTimeout. Kikubwa cha kuzingatio ni kuwa timeInterval itakuwa inaendelea ku excute kila baada ya huo muda ulioweka bila ya kikomo mpaka pale utakapo fanya i stop.

 

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<p id="showTime"></p>

<script>

 var hesabu = 0;

 var muda = setInterval(function (){

   hesabu += 1;

   document.getElementById("showTime").innerHTML = hesabu;

 }, 1000);

</script>

</body>

 

Unaweza kuweka timeinterval zaidi ya moja kwenye code, pia unaweza kucanganya na setTimeout zaidi ya moja kweye ukurasa mmoja. Sasa kama nilivyo kueleza kuwa code zitaendelea ku excute kila baada ya muda fulani, mpaka utakapo sitisha kufanya hivyo.


 

Jinsi ya kusitisha timeInterval() na setTimeout():

ili kuweza kusitisha settimeout() tutatumia method hii clearTimeout() na ukitaka kusitisha setinterval() tutatumia method hii clearInterval()

 

Mfano 1: kusitisa setinterval

<html>

<head>

 <title>Mafunzo ya javascript</title>

</head>

</html>

<body>

<id="showTime"></p>

<button onclick="sitisha()">Sitisha Muda</button>

<script>

 var hesabu 0;

 var muda setInterval(function (){

   hesabu += 1;

...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 201


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Game 3: Mchezo wa kufikiria namba kwa kutumia javascript
Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript
Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 16: Jinsi ya kutumia html form kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard
Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator Soma Zaidi...