JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
MATENDO YA KIHESABU
Somo hili litakwenda kukujulisha namna ya kutumia matendo ya kihesabu katika javascript. matndo ya kihesabu ni muhimu sana katika kutengeneza program za kikompyuta.
Katika program za kihesabu alama za matendo ya kihesabu huitwa operator na namba ambazo hutumika kwenye hesabu huitwa operand.
Matendo ya kihesabu (operator) ni kama:-
-
Kujumlisha +
-
kutoa -
-
kigawanya /
-
kuzidisha *
-
modulus % hii hutumika kwenye kugawanya na kubakia
-
increment ++
-
decrement –
1. Kujumslisha
Kama tulivyoona hapo juu kujumlisha namba tunatumia alama ya jumlisha ambayo ni +.
Mfano 1
<script>
var a = 4
var b = 5
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itatupa matokeo ya 9
Pia unaweza kutumia alama hii ya kujumlisha kuunganisha string zaidi ya moja. String ni mkusanyiko wa namba na herufi ama herufi tupu. Angalia mfano wa hapo chini
Mfano 2
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itakupa matokeao haya
Utaona neno juma na Ali yameungana kutengeneza jumaAli. Katika hali ya kawaida ya kiuandishi yanatakiwa yasomeke juma Ali kwa kuacha nafasi katikati yao. katika javascript ktatuwa changamoto hii tutatumia alama ya kujumlisha +” “ + angalia mfano hapo chini:-
Mfano 3
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a +" "+ b
document.write(c)
</script>
Hii itatupa matokeo haya
Pia unaweza kujumlisha string na namba. Angalia mfano hapo chini
Mfano 4
<script>
var a = 'bongo';
var b = 5;
var c = a + b;
document.write(c)
</script>
Hi itatupa matokeo haya:
Mfano 5
<script>
var a = '7';
var b = 5;
var c = a - b;
document.write('Jibu ni' + " "+ c)
</script>
Hii itakupa matokeo haya
Katika mfano huo hapo juu jibu 75 yaa ni 7 na 5 na sio namba sabini na tano. Ni kwa sababu namba 7 imetumika kama string na ndio maana utaiona ipo ndani ya alama hizi '7'
2. Kutoa
Ili kutoa namba tunatumia alama ya - kama inavyotumika kwenye hesabu. Utaweza kutoa namba kubwa kutoa ndogo, ama nndogo kutoa kubwa na jibu litakuja k...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 18: Jinsi ya kutumia switch case kwenye javascript
Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...