JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
MATENDO YA KIHESABU
Somo hili litakwenda kukujulisha namna ya kutumia matendo ya kihesabu katika javascript. matndo ya kihesabu ni muhimu sana katika kutengeneza program za kikompyuta.
Katika program za kihesabu alama za matendo ya kihesabu huitwa operator na namba ambazo hutumika kwenye hesabu huitwa operand.
Matendo ya kihesabu (operator) ni kama:-
-
Kujumlisha +
-
kutoa -
-
kigawanya /
-
kuzidisha *
-
modulus % hii hutumika kwenye kugawanya na kubakia
-
increment ++
-
decrement –
1. Kujumslisha
Kama tulivyoona hapo juu kujumlisha namba tunatumia alama ya jumlisha ambayo ni +.
Mfano 1
<script>
var a = 4
var b = 5
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itatupa matokeo ya 9
Pia unaweza kutumia alama hii ya kujumlisha kuunganisha string zaidi ya moja. String ni mkusanyiko wa namba na herufi ama herufi tupu. Angalia mfano wa hapo chini
Mfano 2
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itakupa matokeao haya
Utaona neno juma na Ali yameungana kutengeneza jumaAli. Katika hali ya kawaida ya kiuandishi yanatakiwa yasomeke juma Ali kwa kuacha nafasi katikati yao. katika javascript ktatuwa changamoto hii tutatumia alama ya kujumlisha +” “ + angalia mfano hapo chini:-
Mfano 3
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a +" "+ b
document.write(c)
</script>
Hii itatupa matokeo haya
Pia unaweza kujumlisha string na namba. Angalia mfano hapo chini
Mfano 4
<script>
var a = 'bongo';
var b = 5;
var c = a + b;
document.write(c)
</script>
Hi itatupa matokeo haya:
Mfano 5
<script>
var a = '7';
var b = 5;
var c = a - b;
document.write('Jibu ni' + " "+ c)
</script>
Hii itakupa matokeo haya
Katika mfano huo hapo juu jibu 75 yaa ni 7 na 5 na sio namba sabini na tano. Ni kwa sababu namba 7 imetumika kama string na ndio maana utaiona ipo ndani ya alama hizi '7'
2. Kutoa
Ili kutoa namba tunatumia alama ya - kama inavyotumika kwenye hesabu. Utaweza kutoa namba kubwa kutoa ndogo, ama nndogo kutoa kubwa na jibu litakuja k...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 web hosting 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard
Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.
Soma Zaidi...