JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
MATENDO YA KIHESABU
Somo hili litakwenda kukujulisha namna ya kutumia matendo ya kihesabu katika javascript. matndo ya kihesabu ni muhimu sana katika kutengeneza program za kikompyuta.
Katika program za kihesabu alama za matendo ya kihesabu huitwa operator na namba ambazo hutumika kwenye hesabu huitwa operand.
Matendo ya kihesabu (operator) ni kama:-
-
Kujumlisha +
-
kutoa -
-
kigawanya /
-
kuzidisha *
-
modulus % hii hutumika kwenye kugawanya na kubakia
-
increment ++
-
decrement –
1. Kujumslisha
Kama tulivyoona hapo juu kujumlisha namba tunatumia alama ya jumlisha ambayo ni +.
Mfano 1
<script>
var a = 4
var b = 5
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itatupa matokeo ya 9
Pia unaweza kutumia alama hii ya kujumlisha kuunganisha string zaidi ya moja. String ni mkusanyiko wa namba na herufi ama herufi tupu. Angalia mfano wa hapo chini
Mfano 2
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a + b
document.write(c)
</script>
hii itakupa matokeao haya
Utaona neno juma na Ali yameungana kutengeneza jumaAli. Katika hali ya kawaida ya kiuandishi yanatakiwa yasomeke juma Ali kwa kuacha nafasi katikati yao. katika javascript ktatuwa changamoto hii tutatumia alama ya kujumlisha +” “ + angalia mfano hapo chini:-
Mfano 3
<script>
var a = 'juma';
var b = 'Ali'
var c = a +" "+ b
document.write(c)
</script>
Hii itatupa matokeo haya
Pia unaweza kujumlisha string na namba. Angalia mfano hapo chini
Mfano 4
<script>
var a = 'bongo';
var b = 5;
var c = a + b;
document.write(c)
</script>
Hi itatupa matokeo haya:
Mfano 5
<script>
var a = '7';
var b = 5;
var c = a - b;
document.write('Jibu ni' + " "+ c)
</script>
Hii itakupa matokeo haya
Katika mfano huo hapo juu jibu 75 yaa ni 7 na 5 na sio namba sabini na tano. Ni kwa sababu namba 7 imetumika kama string na ndio maana utaiona ipo ndani ya alama hizi '7'
2. Kutoa
Ili kutoa namba tunatumia alama ya - kama inavyotumika kwenye hesabu. Utaweza kutoa namba kubwa kutoa ndogo, ama nndogo kutoa kubwa na jibu litakuja k...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript
Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo
Soma Zaidi...Game 1: Jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawili kwa kutumia html, css na javascript
Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript
Soma Zaidi...