picha

JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

MATENDO YA KIHESABU

Somo hili litakwenda kukujulisha namna ya kutumia matendo ya kihesabu katika javascript. matndo ya kihesabu ni muhimu sana katika kutengeneza program za kikompyuta. 

 

Katika program za kihesabu alama za matendo ya kihesabu huitwa operator na namba ambazo hutumika kwenye hesabu huitwa operand.

 

Matendo ya kihesabu (operator) ni kama:-

  1. Kujumlisha +

  2. kutoa -

  3. kigawanya /

  4. kuzidisha *

  5. modulus % hii hutumika kwenye kugawanya na kubakia

  6. increment ++

  7. decrement –

 

1. Kujumslisha

Kama tulivyoona hapo juu kujumlisha namba tunatumia alama ya jumlisha ambayo ni +. 

 

Mfano 1

<script>

   var a = 4

   var b = 5

   var c = a + b

  document.write(c)

</script>

 

hii itatupa matokeo ya 9

 

Pia unaweza kutumia alama hii ya kujumlisha kuunganisha string zaidi ya moja. String ni mkusanyiko wa namba na herufi ama herufi tupu. Angalia mfano wa hapo chini

 

Mfano 2

<script>

   var a = 'juma';

   var b = 'Ali'

   var c = a + b

  document.write(c)

</script>

 

hii itakupa matokeao haya

Utaona neno juma na Ali yameungana kutengeneza jumaAli. Katika hali ya kawaida ya kiuandishi yanatakiwa yasomeke juma Ali kwa kuacha nafasi katikati yao. katika javascript ktatuwa changamoto hii tutatumia alama ya kujumlisha +” “ + angalia mfano hapo chini:-

 

Mfano 3

<script>

   var a = 'juma';

   var b = 'Ali'

   var c = a +" "+ b

  document.write(c)

</script>

 

Hii itatupa matokeo haya

Pia unaweza kujumlisha string na namba. Angalia mfano hapo chini

 

Mfano 4

<script>

   var a = 'bongo';

   var b = 5;

   var c = a  + b;

  document.write(c)

</script>

 

Hi itatupa matokeo haya:

Mfano 5

<script>

   var a = '7';

   var b = 5;

   var c = a  - b;

  document.write('Jibu ni' + " "+ c)

</script>

 

Hii itakupa matokeo haya

Katika mfano huo hapo juu jibu 75 yaa ni 7 na 5 na sio namba sabini na tano. Ni kwa sababu namba 7 imetumika kama string na ndio maana utaiona ipo ndani ya alama hizi '7'   

 

2. Kutoa

Ili kutoa namba tunatumia alama ya - kama inavyotumika kwenye hesabu. Utaweza kutoa namba kubwa kutoa ndogo, ama nndogo kutoa kubwa na jibu litakuja kwenye negative yaani hasi. Angalia mifano hapo chini

 

">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-19 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 835

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 20 Jinsi ya kutumia foOfloop kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method

Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.

Soma Zaidi...