JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.
Katika somo hili tutajifunza ulinganivu wa thamani (value) kwa kutumia logic operator. Somo hili ni muhiimu sana kwa wanaotarajia kujikita zaidi kwenye matumizi ya javascript.
Kwa wale wanaokumbuka hesabu hapa tutaangalia matumizi ya alama zifuatazo kwenye javascript. Alama hizo ni kama zinazoonyehswa hapo chini.
Kwa wale ambao tumepita shule zamani alama hizo zinamaanisha hivi
Pia kuna hizi
Hebu tuone maana yake kila moja wapo. Pia tutajifunza zaidi kila tutakavyokwenda mbele ya somo hili. kwa sasa tutajifunza kwa ufupi maana zake tu.
Tutatumia mifano kama ifuatavyo:-
-
alama ya ==
Tunajuwa kuwa 4 sio sawa na 5. Sasa kama kweli tunataka itupe jibu la false. code hizo hapo chini zinamaanisha 4 ni sawa sawa na 5, ambapo ni uwongo yaani false.
<script>
let x = 4;
let b = 5;
//alama ya sawa sawa ==
document.write( x == b)
</script>
Kwa kuwa 100 ni sawa sawa na 100 tunahitaji tuone majibu kuwa true yaani kweli
<script>
let x = 100;
let b = 100;
//alama ya sawa sawa ==
document.write( x == b)
</script>
-
Alama ya ===
Katika mfano hapo chini 5 == ‘5’ hii ni true kwa kuwa thamani zao wote ni sawa ni 5.
<script>
//alama ya sawa sawa ==
document.write( 5 == '5')
</script>
Lakini 5===’5’ itatupa majibu false kwa sababu 5 ya kwanza ni namba na 5 ya pili ni string kwa sababu ipo ndani ya alama za string. Hivyo thamani zao ni saswa lakini aina zao sio sawa moja ni namba na nyingine ni string.
<script>
//alama ya sawa sawa ==
document.write( 5 === '5')
</script>
lakini hii 5===5 itatupa majibu ya true kwa sababu thamani zao ni sawa na zote ni data za aina moja yaani namba.
<script>
//alama ya sawa sawa ==
document.write( 5 === 5)
</script>
-
Alama ya != (sio sawa na)
kwa kuwa 5 sio sawa na 2 basi code hii tunatarajia itupe jibu la true 5 !=2 kwa sababu alama != inamaanisha sio sawa na. Yaani 5!=2 ina maana 5 sio sawa na 2
<script>
//alama ya !=
document.write( 5 != 2)
</script>
Au 2 != 2 hii itatupa jibu false yaani sio kweli kwa sababu 2 ni sawa na 2.
<script>
//alama ya !=
document.write( 2 != 2)
</script>
-
Alama ya !== (sio sawa kwa thamani au sio sawa kwa aina)
3 na 2 sio sawa kwa thamani hivyo 3 !== 2 itatupa jibu la true
<script>
//alama ya !==
document.write( 2 !== 3)
</script>
Lakini 2 !== ‘2’ hii pia itatupa jibu la true kwa sababu 2 sio sawa na ‘2’ kwani mbili ya kwanza ni namba na mbili ya pili ni shtring, ndio maana ipo kwenye alama za semi.
<script>
//alama ya !==
document.write( 2 !== '2')
</script>
-
Alama ya > (kubwa kuliko)
Nmambari 5 ni kubwa kuliko nambari 4 hivyo 5 > 4 ni swa hivyoitatupa jibu la true kwa kuwa alama > inamanisha kubwa kuliko
<script>
//alama ya >
document.write( 5 >...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 ai web app 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard
Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.
Soma Zaidi...