Menu



JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Katika somo hili tutajifunza ulinganivu wa thamani (value) kwa kutumia logic operator. Somo hili ni muhiimu sana kwa wanaotarajia kujikita zaidi kwenye matumizi ya javascript.

 

Kwa wale wanaokumbuka hesabu hapa tutaangalia matumizi ya alama zifuatazo kwenye javascript. Alama hizo ni kama zinazoonyehswa hapo chini.

 

Kwa wale ambao tumepita shule zamani alama hizo zinamaanisha hivi

Pia kuna hizi

 

Hebu tuone maana yake kila moja wapo. Pia tutajifunza zaidi kila tutakavyokwenda mbele ya somo hili. kwa sasa tutajifunza kwa ufupi maana zake tu.

 

Tutatumia mifano kama ifuatavyo:-

  1. alama ya ==

Tunajuwa kuwa 4 sio sawa na 5. Sasa kama kweli tunataka itupe jibu la false. code hizo hapo chini zinamaanisha 4 ni sawa sawa na 5, ambapo ni uwongo yaani false. 

<script>

   let x = 4;

   let b = 5;

 

   //alama ya sawa sawa ==

   document.write( x == b)

</script>

 

Kwa kuwa 100 ni sawa sawa na 100 tunahitaji tuone majibu kuwa true yaani kweli

<script>

   let x = 100;

   let b = 100;

 

   //alama ya sawa sawa ==

   document.write( x == b)

</script>

 

 

  1. Alama ya ===

Katika mfano hapo chini 5 == ‘5’ hii ni true kwa kuwa thamani zao wote ni sawa ni 5.

<script>

   //alama ya sawa sawa ==

   document.write( 5 == '5')

</script>

Lakini 5===’5’ itatupa majibu false kwa sababu 5 ya kwanza ni namba na 5 ya pili ni string kwa sababu ipo ndani ya alama za string. Hivyo thamani zao ni saswa lakini aina zao sio sawa moja ni namba na nyingine ni string.

<script>

   //alama ya sawa sawa ==

   document.write( 5 === '5')

</script>

lakini hii 5===5 itatupa majibu ya true kwa sababu thamani zao ni sawa na zote ni data za aina moja yaani namba.

<script>

   //alama ya sawa sawa ==

   document.write( 5 === 5)

</script>

 

  1. Alama ya != (sio sawa na)

kwa kuwa 5 sio sawa na 2 basi code hii tunatarajia itupe jibu la true 5 !=2 kwa sababu alama != inamaanisha sio sawa na. Yaani 5!=2 ina maana 5 sio sawa na 2

<script>

   //alama ya !=

   document.write( 5 != 2)

</script>

Au 2 != 2 hii itatupa jibu false yaani sio kweli kwa sababu 2 ni sawa na 2.

<script>

   //alama ya !=

   document.write( 2 != 2)

</script>

  1. Alama ya !== (sio sawa kwa thamani au sio sawa kwa aina)

3 na 2 sio sawa kwa thamani hivyo 3 !== 2 itatupa jibu la true

<script>

   //alama ya !==

   document.write( 2 !== 3)

</script>

Lakini 2 !== ‘2’ hii pia itatupa jibu la true kwa sababu 2 sio sawa na ‘2’ kwani mbili ya kwanza ni namba na mbili ya pili ni shtring, ndio maana ipo kwenye alama za semi. 

<script>

   //alama ya !==

   document.write( 2 !== '2')

</script>

 

...

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: Masomo File: Download PDF Views 340

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 16: Jinsi ya kutumia html form kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

Soma Zaidi...
Game 3: Mchezo wa kufikiria namba kwa kutumia javascript

Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba

Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop

Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...