image

JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

AINA ZA DATA ZINAZOTUMIKA KWENYE JAVASCRIPT

Aina za data ambazo javascript inatumia ni sawa na zile ambazo zinapatikana kwenye programming language nyingine kama php. Javascript inatumia aina zifuatazo:-

 

  1. Namba

javascript ni tofauti na programming language zingine kama php ambapo namba kuna zenye desimali na zisizo. Kwenye javascript namba ni namba iwe na desimali ni namba ama isiwe na desimali. 

 

Mfano 1: 

<script>

let x1 = 3.04; // desimali

let x2 = 5;  // bila ya desimali

document.write(x1, '<br>', x2);

 

</script>

 

Itakupa matokeo haya:

  1. String

String ni mkusanyiko unaojumuisha namba, herufi na alama. Aina hii inachukuwa amala zote, namba zote na herufi zote. Mfano ukisema “bongoclass” hii ni string. Au ukisema “admin5@bongoclass.com” hii pia ni string ambayo ina namba, 5 alama @ pamoja na herufi. Kumbuka string siku zote inakaa ndani ya alama za kufunga na kufungua semi, kama ilivyo mifano hapo juu.

 

Mfano 2

<script>

let a = "bongoclass";

let b = ".com";

document.write(a, b);

 

</script>

Hii itakupa matokeo haya:-

  1. Boolean

Kama ilivyo kwenye programming language zingine, bulean inabeba matokeo mawili tu true au false. Ainahii ya data pia hutumika kwenye javascript. Tulishaona mifano kadhaa katika somo lililotangulia wakati tunajifunza namna ya kutumia logic.

 

Mfano 3

Tunaelewa kuwa 3 ni kubwa kuliko 2. Hivyo tunatarajia itupe jibu la true kuwa ni kweli tatu ni kubwa kuliko mbili.

<script>

 

document.write(3 >2);

 

</script>

Mfano 4

Tunaelewa kuwa 5 ni kubwa kuliko 4 sasa endapo tutaandika 4 ni kubwa kuliko 5 inatakiwa itupe majibu false yaani sio kweli kuwa 4 ni kubwa kuliko 5.

<script>

 

document.write(4 >5);

 

</script>

 

  1. Array

Array ni mkusanyiko wa data za aina moja ambazo huweza kufikiwa kwa jina moja. Katika javascript pia tunatumia array. Siku zote array huanzia na 0. Kwa kuwa ni mkusanyiko wa data, basi ile ya kwanza kutajwa hupewa namba 0. Na pia array siku zote hukaa ndani ya mabano [], na kila moja inakuwa ndan ya alama ya kufunga semi kama zilivyo string. Na kama list ina item nyingi kila moja hutenganishwa kwa alama ya koma ( , ). Angalia mifano hapo chini

 

Mfano 5:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti);

 

</script>

Kama nilivyokueleza kuwa array huanzia na 0 hivyo basi katika array hapo juu 0 ni mpapani, 1 ni muembe, na 2 ni muarobaini. Na endapo unataka kuisoma array ya 2 basi baada ya kutaja array utaweka mapbano na kuweka 2.

 

Mfano 6:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti[2]);

 

</script>

...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 201


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard
Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 16: Jinsi ya kutumia html form kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 20 Jinsi ya kutumia foOfloop kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu. Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code Soma Zaidi...

JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia. Soma Zaidi...

Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player Soma Zaidi...