JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

AINA ZA DATA ZINAZOTUMIKA KWENYE JAVASCRIPT

Aina za data ambazo javascript inatumia ni sawa na zile ambazo zinapatikana kwenye programming language nyingine kama php. Javascript inatumia aina zifuatazo:-

 

  1. Namba

javascript ni tofauti na programming language zingine kama php ambapo namba kuna zenye desimali na zisizo. Kwenye javascript namba ni namba iwe na desimali ni namba ama isiwe na desimali. 

 

Mfano 1: 

<script>

let x1 = 3.04; // desimali

let x2 = 5;  // bila ya desimali

document.write(x1, '<br>', x2);

 

</script>

 

Itakupa matokeo haya:

  1. String

String ni mkusanyiko unaojumuisha namba, herufi na alama. Aina hii inachukuwa amala zote, namba zote na herufi zote. Mfano ukisema “bongoclass” hii ni string. Au ukisema “admin5@bongoclass.com” hii pia ni string ambayo ina namba, 5 alama @ pamoja na herufi. Kumbuka string siku zote inakaa ndani ya alama za kufunga na kufungua semi, kama ilivyo mifano hapo juu.

 

Mfano 2

<script>

let a = "bongoclass";

let b = ".com";

document.write(a, b);

 

</script>

Hii itakupa matokeo haya:-

  1. Boolean

Kama ilivyo kwenye programming language zingine, bulean inabeba matokeo mawili tu true au false. Ainahii ya data pia hutumika kwenye javascript. Tulishaona mifano kadhaa katika somo lililotangulia wakati tunajifunza namna ya kutumia logic.

 

Mfano 3

Tunaelewa kuwa 3 ni kubwa kuliko 2. Hivyo tunatarajia itupe jibu la true kuwa ni kweli tatu ni kubwa kuliko mbili.

<script>

 

document.write(3 >2);

 

</script>

Mfano 4

Tunaelewa kuwa 5 ni kubwa kuliko 4 sasa endapo tutaandika 4 ni kubwa kuliko 5 inatakiwa itupe majibu false yaani sio kweli kuwa 4 ni kubwa kuliko 5.

<script>

 

document.write(4 >5);

 

</script>

 

  1. Array

Array ni mkusanyiko wa data za aina moja ambazo huweza kufikiwa kwa jina moja. Katika javascript pia tunatumia array. Siku zote array huanzia na 0. Kwa kuwa ni mkusanyiko wa data, basi ile ya kwanza kutajwa hupewa namba 0. Na pia array siku zote hukaa ndani ya mabano [], na kila moja inakuwa ndan ya alama ya kufunga semi kama zilivyo string. Na kama list ina item nyingi kila moja hutenganishwa kwa alama ya koma ( , ). Angalia mifano hapo chini

 

Mfano 5:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti);

 

</script>

Kama nilivyokueleza kuwa array huanzia na 0 hivyo basi katika array hapo juu 0 ni mpapani, 1 ni muembe, na 2 ni muarobaini. Na endapo unataka kuisoma array ya 2 basi baada ya kutaja array utaweka mapbano na kuweka 2.

 

Mfano 6:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti[2]);

 

">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 600

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba

Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript

Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method

Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 20 Jinsi ya kutumia foOfloop kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo

Soma Zaidi...