JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
AINA ZA DATA ZINAZOTUMIKA KWENYE JAVASCRIPT
Aina za data ambazo javascript inatumia ni sawa na zile ambazo zinapatikana kwenye programming language nyingine kama php. Javascript inatumia aina zifuatazo:-
-
Namba
javascript ni tofauti na programming language zingine kama php ambapo namba kuna zenye desimali na zisizo. Kwenye javascript namba ni namba iwe na desimali ni namba ama isiwe na desimali.
Mfano 1:
<script>
let x1 = 3.04; // desimali
let x2 = 5; // bila ya desimali
document.write(x1, '<br>', x2);
</script>
Itakupa matokeo haya:
-
String
String ni mkusanyiko unaojumuisha namba, herufi na alama. Aina hii inachukuwa amala zote, namba zote na herufi zote. Mfano ukisema “bongoclass” hii ni string. Au ukisema “admin5@bongoclass.com” hii pia ni string ambayo ina namba, 5 alama @ pamoja na herufi. Kumbuka string siku zote inakaa ndani ya alama za kufunga na kufungua semi, kama ilivyo mifano hapo juu.
Mfano 2
<script>
let a = "bongoclass";
let b = ".com";
document.write(a, b);
</script>
Hii itakupa matokeo haya:-
-
Boolean
Kama ilivyo kwenye programming language zingine, bulean inabeba matokeo mawili tu true au false. Ainahii ya data pia hutumika kwenye javascript. Tulishaona mifano kadhaa katika somo lililotangulia wakati tunajifunza namna ya kutumia logic.
Mfano 3
Tunaelewa kuwa 3 ni kubwa kuliko 2. Hivyo tunatarajia itupe jibu la true kuwa ni kweli tatu ni kubwa kuliko mbili.
<script>
document.write(3 >2);
</script>
Mfano 4
Tunaelewa kuwa 5 ni kubwa kuliko 4 sasa endapo tutaandika 4 ni kubwa kuliko 5 inatakiwa itupe majibu false yaani sio kweli kuwa 4 ni kubwa kuliko 5.
<script>
document.write(4 >5);
</script>
-
Array
Array ni mkusanyiko wa data za aina moja ambazo huweza kufikiwa kwa jina moja. Katika javascript pia tunatumia array. Siku zote array huanzia na 0. Kwa kuwa ni mkusanyiko wa data, basi ile ya kwanza kutajwa hupewa namba 0. Na pia array siku zote hukaa ndani ya mabano [], na kila moja inakuwa ndan ya alama ya kufunga semi kama zilivyo string. Na kama list ina item nyingi kila moja hutenganishwa kwa alama ya koma ( , ). Angalia mifano hapo chini
Mfano 5:
<script>
let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]
document.write(mti);
</script>
Kama nilivyokueleza kuwa array huanzia na 0 hivyo basi katika array hapo juu 0 ni mpapani, 1 ni muembe, na 2 ni muarobaini. Na endapo unataka kuisoma array ya 2 basi baada ya kutaja array utaweka mapbano na kuweka 2.
Mfano 6:
<script>
let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]
document.write(mti[2]);
</script>
-
Object
Object ni data ambayo inakuwa na sifa pamoja na aina. Object inakuwa na jina na thamani, ikitenganishwa na alama ya coma. Pia object huandikw...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 web hosting 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Game 3: Mchezo wa kufikiria namba kwa kutumia javascript
Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript
Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo
Soma Zaidi...Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.
Soma Zaidi...