JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

AINA ZA DATA ZINAZOTUMIKA KWENYE JAVASCRIPT

Aina za data ambazo javascript inatumia ni sawa na zile ambazo zinapatikana kwenye programming language nyingine kama php. Javascript inatumia aina zifuatazo:-

 

  1. Namba

javascript ni tofauti na programming language zingine kama php ambapo namba kuna zenye desimali na zisizo. Kwenye javascript namba ni namba iwe na desimali ni namba ama isiwe na desimali. 

 

Mfano 1: 

<script>

let x1 = 3.04; // desimali

let x2 = 5;  // bila ya desimali

document.write(x1, '<br>', x2);

 

</script>

 

Itakupa matokeo haya:

  1. String

String ni mkusanyiko unaojumuisha namba, herufi na alama. Aina hii inachukuwa amala zote, namba zote na herufi zote. Mfano ukisema “bongoclass” hii ni string. Au ukisema “admin5@bongoclass.com” hii pia ni string ambayo ina namba, 5 alama @ pamoja na herufi. Kumbuka string siku zote inakaa ndani ya alama za kufunga na kufungua semi, kama ilivyo mifano hapo juu.

 

Mfano 2

<script>

let a = "bongoclass";

let b = ".com";

document.write(a, b);

 

</script>

Hii itakupa matokeo haya:-

  1. Boolean

Kama ilivyo kwenye programming language zingine, bulean inabeba matokeo mawili tu true au false. Ainahii ya data pia hutumika kwenye javascript. Tulishaona mifano kadhaa katika somo lililotangulia wakati tunajifunza namna ya kutumia logic.

 

Mfano 3

Tunaelewa kuwa 3 ni kubwa kuliko 2. Hivyo tunatarajia itupe jibu la true kuwa ni kweli tatu ni kubwa kuliko mbili.

<script>

 

document.write(3 >2);

 

</script>

Mfano 4

Tunaelewa kuwa 5 ni kubwa kuliko 4 sasa endapo tutaandika 4 ni kubwa kuliko 5 inatakiwa itupe majibu false yaani sio kweli kuwa 4 ni kubwa kuliko 5.

<script>

 

document.write(4 >5);

 

</script>

 

  1. Array

Array ni mkusanyiko wa data za aina moja ambazo huweza kufikiwa kwa jina moja. Katika javascript pia tunatumia array. Siku zote array huanzia na 0. Kwa kuwa ni mkusanyiko wa data, basi ile ya kwanza kutajwa hupewa namba 0. Na pia array siku zote hukaa ndani ya mabano [], na kila moja inakuwa ndan ya alama ya kufunga semi kama zilivyo string. Na kama list ina item nyingi kila moja hutenganishwa kwa alama ya koma ( , ). Angalia mifano hapo chini

 

Mfano 5:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti);

 

</script>

Kama nilivyokueleza kuwa array huanzia na 0 hivyo basi katika array hapo juu 0 ni mpapani, 1 ni muembe, na 2 ni muarobaini. Na endapo unataka kuisoma array ya 2 basi baada ya kutaja array utaweka mapbano na kuweka 2.

 

Mfano 6:

<script>

let mti = ["mpapai", "muembe", "muarobaini"]

document.write(mti[2]);

 

">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 638

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop

Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.

Soma Zaidi...
Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css

Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player

Soma Zaidi...
Game 1: Jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawili kwa kutumia html, css na javascript

Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo

Soma Zaidi...
Game 3: Mchezo wa kufikiria namba kwa kutumia javascript

Hii ni game ambayo utafikiria namba, ambayo inatakiwa iwe sawa na namba ambayo game imeiweka.

Soma Zaidi...