JAVASCRIPT - somo la 18: Jinsi ya kutumia switch case kwenye javascript
Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.
Switch statement haina utifauti na if else ama kiweka if. Chukulia mfano huu hapa
Unatakiwa uandae program ya dictionary, yenyewe utaandika neno kwa kiswahili kisha utaletewa kiongereza chake.
Ili kutengeneza program hii tutakwendabkutumia maneno yafuatayo kama mfano
Father - baba
Mother - mama
Sister - dada
Uncle - mjomba
Aunt - shangazi
Nephew or cousin - mpwa
Cousin - binamu
Brother - kaka
Sasa program hii tutaanza kuitengeneza kwa kutumia if tupu, kama ambavyo tuliona katika somo lililotangaulia. Pia unaweza kutumia else if kama tulivyojifunza.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
if(neno == 'baba'){
document.write("<b style='color:blue'>Father</b>");
}
if(neno == 'mama'){
document.write("<b style='color:blue'>mother</b>");
}
if(neno == 'dada'){
document.write("<b style='color:blue'>sister</b>");
}
if(neno == 'mjomba'){
document.write("<b style='color:blue'>uncle</b>");
}
if(neno == 'shangazi'){
document.write("<b style='color:blue'>aunt</b>");
}
if(neno == 'mpwa'){
document.write("<b style='color:blue'>nephew or cousin</b>");
}
if(neno == 'kaka'){
document.write("<b style='color:blue'>brother</b>");
}
</script>
</body>
</html>
Hapo utaona kuna changamoto kuu 2
- Kwanza kila wakati tumerudia rudia kuweka condition if(neno==)
- Pili hata ukitumia else ili kuhusisha manono yasio na mfanano haitakaa sawa. Maana result ya else itakuwa inajirudia
Sasa ili tuweze kupambana na hali hii ndipo tutatumia switch ambapo itaturahisishia kuthibiti changamoto hizo.
Jinsi ya kutengeneza switch
Utaanza na neno switch likifuatiwa na mabano switch () ndani ya mabano utaweka statement katika hii statement utaweka kile ambacho unakwenda kukitest. Inaweza kuwa variable ama chochote kila kitakachokuwepo kwenye statement hio. switch(statement) baada ya hapo itafuatiwa mabano{} kisha ndipo tutaanza kutest condition ambayo tutaiita value kwa kutumia neno case 'condition' utamalizia na nukta pacha : baada ya hapo utafuata kuandika statement yako yaani nini kitokee kwenye hiyo case.
switch(statement){
case value 1:
statement
case value 2:
statement
case value 3:
statement
}
Sasa wacha tuone mfano wetu wa kwanza kwa kutumia switch
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
switch(neno){
case'baba':
document.write("<h1>Father<h1>")
case'mama':
document.write("<h1>Mother<h1>")
case'dada':
document.write("<h1>Sister<h1>")
case'kaka':
document.write("<h1>Brother<h1>")
case'mjomba':
document.write("<h1>Uncle<h1>")
case'shangazi':
document.write("<h1>Aunt<h1>")
case'mpwa':
document.write("<h1>Nephew or niece<h1>")
}
</script>
</body>
</html>
Saaa hapo utaona kuna changamoto mbili kwenye hizo code:-
Kwanza code baada ya kuonyesha matokeo ya inputi zinaendelea kufanya kazi. Utaona hapo nimeweka neno baba sasa ikaniletea jibu father kisha ikaendelea kukaliza na list iliyobaki kutokea kwa baba.
Ili kutatua changamoto hii tutatumia break keyword yaani baada ya matokeo code zinatakiwa zi stop kufanya kazi.
Pili hapo hatukuweza kuthibiti endapo mtu ataandika ambacho hakina mfanano. Kwa mfano hapo uliandika mbuzi haitaleta majibu yeyote.
Ili kutatua tatizo hili tutatumia default keyword ambayo mi sawa na else kama tulivyoona somo lililotangalia. Hivyo basi kanuni nzima itakuwa hivi. Hii default itafanyabkazi endapo mtu ataandika kitu chochote ambacho hakipo kwenye list.
switch(statement){
case value 1:
statement
Break;
case value 2:
statement
break;
case value 3:
statement
break;
}
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
switch(neno){
case'baba':
document.write("<h1>Father<h1>")
break;
case'mama':
document.write("<h1>Mother<h1>")
break;
case'dada':
document.write("<h1>Sister<h1>")
break;
case'kaka':
&n...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 20 Jinsi ya kutumia foOfloop kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css
Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba
Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...Offline data handle kwa kutumia javascript
Katika somo hili tutaenda kujifunza namna ya kuhifadhi taarifa za mtumiaji endapo mtandao utakuwa haupo ()
Soma Zaidi...