Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.
Switch statement haina utifauti na if else ama kiweka if. Chukulia mfano huu hapa
Unatakiwa uandae program ya dictionary, yenyewe utaandika neno kwa kiswahili kisha utaletewa kiongereza chake.
Ili kutengeneza program hii tutakwendabkutumia maneno yafuatayo kama mfano
Father - baba
Mother - mama
Sister - dada
Uncle - mjomba
Aunt - shangazi
Nephew or cousin - mpwa
Cousin - binamu
Brother - kaka
Sasa program hii tutaanza kuitengeneza kwa kutumia if tupu, kama ambavyo tuliona katika somo lililotangaulia. Pia unaweza kutumia else if kama tulivyojifunza.
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
if(neno == 'baba'){
document.write("<b style='color:blue'>Father</b>");
}
if(neno == 'mama'){
document.write("<b style='color:blue'>mother</b>");
}
if(neno == 'dada'){
document.write("<b style='color:blue'>sister</b>");
}
if(neno == 'mjomba'){
document.write("<b style='color:blue'>uncle</b>");
}
if(neno == 'shangazi'){
document.write("<b style='color:blue'>aunt</b>");
}
if(neno == 'mpwa'){
document.write("<b style='color:blue'>nephew or cousin</b>");
}
if(neno == 'kaka'){
document.write("<b style='color:blue'>brother</b>");
}
</script>
</body>
</html>
Hapo utaona kuna changamoto kuu 2
Sasa ili tuweze kupambana na hali hii ndipo tutatumia switch ambapo itaturahisishia kuthibiti changamoto hizo.
Jinsi ya kutengeneza switch
Utaanza na neno switch likifuatiwa na mabano switch () ndani ya mabano utaweka statement katika hii statement utaweka kile ambacho unakwenda kukitest. Inaweza kuwa variable ama chochote kila kitakachokuwepo kwenye statement hio. switch(statement) baada ya hapo itafuatiwa mabano{} kisha ndipo tutaanza kutest condition ambayo tutaiita value kwa kutumia neno case 'condition' utamalizia na nukta pacha : baada ya hapo utafuata kuandika statement yako yaani nini kitokee kwenye hiyo case.
switch(statement){
case value 1:
statement
case value 2:
statement
case value 3:
statement
}
Sasa wacha tuone mfano wetu wa kwanza kwa kutumia switch
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
switch(neno){
case'baba':
document.write("<h1>Father<h1>")
case'mama':
document.write("<h1>Mother<h1>")
case'dada':
document.write("<h1>Sister<h1>")
case'kaka':
document.write("<h1>Brother<h1>")
case'mjomba':
document.write("<h1>Uncle<h1>")
case'shangazi':
document.write("<h1>Aunt<h1>")
case'mpwa':
document.write("<h1>Nephew or niece<h1>")
}
</script>
</body>
</html>
Saaa hapo utaona kuna changamoto mbili kwenye hizo code:-
Kwanza code baada ya kuonyesha matokeo ya inputi zinaendelea kufanya kazi. Utaona hapo nimeweka neno baba sasa ikaniletea jibu father kisha ikaendelea kukaliza na list iliyobaki kutokea kwa baba.
Ili kutatua changamoto hii tutatumia break keyword yaani baada ya matokeo code zinatakiwa zi stop kufanya kazi.
Pili hapo hatukuweza kuthibiti endapo mtu ataandika ambacho hakina mfanano. Kwa mfano hapo uliandika mbuzi haitaleta majibu yeyote.
Ili kutatua tatizo hili tutatumia default keyword ambayo mi sawa na else kama tulivyoona somo lililotangalia. Hivyo basi kanuni nzima itakuwa hivi. Hii default itafanyabkazi endapo mtu ataandika kitu chochote ambacho hakipo kwenye list.
switch(statement){
case value 1:
statement
Break;
case value 2:
statement
break;
case value 3:
statement
break;
}
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let neno = prompt("weka neno la kiswahili kwa herufi ndogo");
switch(neno){
case'baba':
document.write("<h1>Father<h1>")
break;
case'mama':
document.write("<h1>Mother<h1>")
break;
case'dada':
document.write("<h1>Sister<h1>")
break;
&">...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...Ksomo hili litakwenda kukufundisha kuhusu object kwenye javascript, kazi zake na sheria zake katika kuiandika.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.
Soma Zaidi...