picha

JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

JAVASCRIPT OUT PUT

Hapa tutajifunza namna ambavyo unaweza kuonyesha matokeo ya code javascript. Yaani ilikwamba hizo code ulizoandika zionyeshe matokeo yanayotarajiwa. Kama umejifunza kuhusu PHP tunatumia print ama echo. Sasa vipi kwenye javascript nini tutatumia. Endelea na somo hili hadi mwisho.

 

Kabla hatujaendelea na somo zaidi, naamini unatumia text editor. Kama unatumia simu unaweza kutumia trebEdit. Kama unatumia komputa unaweza kutumia sublime text. Unaweza pia kutumia notepad, notepad plus, ama text editor yeote. Hakikisha pia una ufahamu kuhusu html angalau basic level.

 

Ni njia zipi javascript hutumia kuonyesha output

Kuna njia 4 ambazo hutumika kwenye javascript kuonyesha output. Njia hizo ni:-

  1. Kwa kutumia innerHTML

  2. Kwa kutumia document.write()

  3. Kwa kutumia window.alert()

  4. Kwa kutumia console.log()

 

  1. Kwa kutumia innerHTML  propert

Property hii hutumika kwa ajili ya ku badili maudhui ya kwenye html element, ama ku modify maudhui, ama kuweka maudhui mapya kwenye elemeny ya html. Mara nyingi hutumika kwenye element <p> lakini inawekza pia kutumika kwenye <div> na maeneo mengine.

 

Hii hutumika katika kufikia element za HTML. kwanza utahitajika element husika kuipa id, kisha utatumia hiyo id ili uweze kuifikia kwa kutumia javascript.

Mafano:

 

<!DOCTYPE html>

<html lang="swa">

<body>

<p id="mfano"></p>

 

<script>

   document.getElementById("mfano").innerHTML = 'haloo javascript';

</script>

 

</body>

</html>

Kwanza element p tumeipa id ya mfano <p id="mfano"></p> Hii inamaanisha maudhui ya kwenye element p yatapatikana baada ya id ya mfano kufikiwa kwenye javascript. Ili kuweka id kwenye html element ni kama unavyotaka kuweka html attributes. Utaanza kuweka tag ya element mafano <p kisha itafata attribute id <p id itafuatiwa na alama ya = <p id = thamani ya id yaani value itakuwa ndani ya alama hizi “” kisha funga element yako <p id="mfano"></p>   Baada ya hapo kinachofuawata ni kuweka code za javascript.

 

Tambuwa kuwa code zote za javascript huwekwa ndani ya tag za javascript. Tag za javascript ni <script> hii ni ya kufungua na </script> hii ni ya kufunga. Sasa kinachofuwata ni kuitumia id ili kuweza kupata matokeo ya javascript.

 

Hapa tutatumia document.getElementById() ili kuweza kuifikia id ya element yetu. Kwenye mabano hapo weka id yetu ambayo ni mfano document.getElementById("mfano") baada ya hapo kinachofuata ni kytumiaproperty ya innerHTML  ili kuweza kuipa maudhui mapya elemebt yetu. Inafuata alama ya = kisha maudhui yako utaweka hapo. Kama ni string yaani mkusanyiko wa herufi na namba ama herufi tupu maudhui hayo yatakuwa ndani ya funga na fugua semi “”. Mfano wetu juu hapo tunataka kuonyesha maneno haloo javascript. Hivyo itakuwa document.getElementById("mfano").innerHTML = 'haloo javascript'; Kma ingelikuwa namba tungeweka document.getElementById("demo").innerHTML = 5 + 6;              

 

Angalia mfano:-

<!DOCTYPE html>

<html lang="swa">

<body>

<p id="mfano"></p>

<div id="mfano2"></div>

<script>

   document.getElementById("mfano").innerHTML = 'haloo javascript';

   document.getElementById("mfano2").innerHTML = 5 + 6;

</script>

</body>

</html>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 945

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 8: Aina za data zinazotumika kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 24: Jinsi ya kutengeneza online keyboard

Katika project hii utakwenda kufunza jinsi utakavyoweza kutengeneza keyboard ya online kwa kutumia javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript

Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 7: Jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia logical operator kwenye javascript. Katika somo hili tutakwenda kutumia mahesabu.

Soma Zaidi...