Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1.  Kitovu kutoa maji maji.

Kwa kawaida kitovu cha mtoto kikifungwa kwa siku ya kwanza kinaweza kuonyesha tu maji maji kwa siku ya kwanza na ya pili na baadae uendelea vizuri lakini mama au mlezi akiona maji maji kwenye siku ya kwanza ya pili na kuendelea na maji yanaendelea kutoka siku kwa siku ajue wazi kuna Maambukizi na anapaswa kumpeleka mtoto haraka hospitalini ili kuweza kupewa matibabu na kuepuka kuwepo kwa Tetunus kwa mtoto.

 

2.Pia mama kwa wakati huu ajiepusha na kutumia madawa ya miti shamba kwenye kitovu cha mtoto kwa sababu anaweza kuleta matatizo makubwa au mengine zaidi kwa sababu miti shamba utumia mda mrefu kuponyesha na pengine haiponyeshi kabisa na mda unaenda kwa hiyo mtoto anapoletwa hospitalini hali inakuwa mbaya zaidi.

 

3. Dalili nyingine ni kubwa kitovu cha mtoto kinavuja damu kupita kiasi.

Hii pia ni Dalili mojawapo ambapo kitovu kinakuwa kinatoa damu inawezekana ni siku chache baada ya kuzaliwa kwa mtoto au siku nyingi kidogo kwa hiyo damu utoka kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao ushambulia sehemu za mishipa ambayo iko kwenye kitovu na damu utoka, kw hiyo.Mama au mlezi wanapaswa kumpeleka mtoto hospitalini kwa matibabu zaidi na epuka matibabu ya kienyeji kwa wakati huu.

 

4. Kuwepo kwa harufu mbaya kwenye sehemu ya kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine kunakuwepo na harufu mbaya kwenye kitovu cha mama pakiandamana na usaha ambao unatoa harufu mbaya, kwa sababu ya kuwepo usaha sio vizuri kubinya usaha ili uweze kutoka kwa sababu huwezi kujua kuwa usaha unatokea sehemu gani kwa sababu kuwepo kwa usaha lazima kuwa kuna kitu kimeoza.

 

5. Ngozi inayozunguka kitovu huwa nyekundu.

Kwa kawaida kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu utakuta ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa nyekundu na pia ukijaribu kugusa utaona mtoto anaumia na kulia kwa hiyo moja kwa moja mzazi au mlezi wa mtoto anapaswa kujua kubwa kuna Maambukizi kwenye kitovu na pia mama hapaswi kufanya chochote kwenye ngozi ya kitovu cha mtoto tofauti na kwenda hospitalini.

 

6. Kuwepo kwa vipele kwenye ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa na vipengele, vipengele hivyo kwa wakati mwingine vinakuwa na usaha au pengine vinakuwa havina au kwa wakati mwingine vinakuwa na maumivu kwa sababu ukimgusa mtoto anaanza kulia hivi vipele kwa wakati mwingine vinaandamana na homa.

 

7. Kwa wakati mwingine mtoto analia sana na kushindwa kunyonya na pengine anasinzia sana kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu. Kwa hiyo akina mama na walezi wa watoto wanapaswa kujua kubwa hawapaswi kuweka chochote ili kutibu maambukizi au kupasua chochote kwenye kitovu cha mtoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 10285

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kondo la nyuma (placenta)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kupasuka kwa kondo la nyuma (plasenta) (abruptio placentae) ni tatizo lisilo la kawaida lakini kubwa la ujauzito.Kondo la nyuma (Placenta) ni muundo ambao hukua ndani ya uterasi wakati wa ujauzito ili kumlisha mtoto ana

Soma Zaidi...
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?

Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.

Soma Zaidi...
Siku za hatari, siku za kubeba mimba

Hizi ni siku hatari kwa mwanamke ambazo ni ahisi kwake kubeba mimba, siku nitakueleza ni zipi na ni zipi sifa zake

Soma Zaidi...
Je dalili ya kuuma tumbo huanza baada ya wiki ngapi Toka mwanamke apate ujauzito?

Maumivu ya tumbo ni moja katika dalili za ujauzito. Maumivu wanawake wengi hushindwa kujuwa kuwa ni ujauzito ama laa. Na hii ni kwa sababu kwa wanawake wengi maumivu ya tumbo ama changu ni jalivya kawaida kwao.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba changa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba changa

Soma Zaidi...
Dalili za kujifungua

Makala hii itakwenda kukufundisha dalili za kujifunguwa, hatuwa za kujifunguwa na kuzalisha, pia utajifunza mabo muhimu kabla na wakatii wa kujifungua.

Soma Zaidi...
Ni ipi siku ya kupata ujauzito, na nitajuwaje kama nimepata ujauzito?

Hapa utajifunza siku nzuri kushoriki tendo la ndoa kupata ujauzito, dalili za siku hiyo na kuitafuta kwa mahesabu

Soma Zaidi...
Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia

Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba

Soma Zaidi...