picha

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1.  Kitovu kutoa maji maji.

Kwa kawaida kitovu cha mtoto kikifungwa kwa siku ya kwanza kinaweza kuonyesha tu maji maji kwa siku ya kwanza na ya pili na baadae uendelea vizuri lakini mama au mlezi akiona maji maji kwenye siku ya kwanza ya pili na kuendelea na maji yanaendelea kutoka siku kwa siku ajue wazi kuna Maambukizi na anapaswa kumpeleka mtoto haraka hospitalini ili kuweza kupewa matibabu na kuepuka kuwepo kwa Tetunus kwa mtoto.

 

2.Pia mama kwa wakati huu ajiepusha na kutumia madawa ya miti shamba kwenye kitovu cha mtoto kwa sababu anaweza kuleta matatizo makubwa au mengine zaidi kwa sababu miti shamba utumia mda mrefu kuponyesha na pengine haiponyeshi kabisa na mda unaenda kwa hiyo mtoto anapoletwa hospitalini hali inakuwa mbaya zaidi.

 

3. Dalili nyingine ni kubwa kitovu cha mtoto kinavuja damu kupita kiasi.

Hii pia ni Dalili mojawapo ambapo kitovu kinakuwa kinatoa damu inawezekana ni siku chache baada ya kuzaliwa kwa mtoto au siku nyingi kidogo kwa hiyo damu utoka kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao ushambulia sehemu za mishipa ambayo iko kwenye kitovu na damu utoka, kw hiyo.Mama au mlezi wanapaswa kumpeleka mtoto hospitalini kwa matibabu zaidi na epuka matibabu ya kienyeji kwa wakati huu.

 

4. Kuwepo kwa harufu mbaya kwenye sehemu ya kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine kunakuwepo na harufu mbaya kwenye kitovu cha mama pakiandamana na usaha ambao unatoa harufu mbaya, kwa sababu ya kuwepo usaha sio vizuri kubinya usaha ili uweze kutoka kwa sababu huwezi kujua kuwa usaha unatokea sehemu gani kwa sababu kuwepo kwa usaha lazima kuwa kuna kitu kimeoza.

 

5. Ngozi inayozunguka kitovu huwa nyekundu.

Kwa kawaida kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu utakuta ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa nyekundu na pia ukijaribu kugusa utaona mtoto anaumia na kulia kwa hiyo moja kwa moja mzazi au mlezi wa mtoto anapaswa kujua kubwa kuna Maambukizi kwenye kitovu na pia mama hapaswi kufanya chochote kwenye ngozi ya kitovu cha mtoto tofauti na kwenda hospitalini.

 

6. Kuwepo kwa vipele kwenye ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa na vipengele, vipengele hivyo kwa wakati mwingine vinakuwa na usaha au pengine vinakuwa havina au kwa wakati mwingine vinakuwa na maumivu kwa sababu ukimgusa mtoto anaanza kulia hivi vipele kwa wakati mwingine vinaandamana na homa.

 

7. Kwa wakati mwingine mtoto analia sana na kushindwa kunyonya na pengine anasinzia sana kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu. Kwa hiyo akina mama na walezi wa watoto wanapaswa kujua kubwa hawapaswi kuweka chochote ili kutibu maambukizi au kupasua chochote kwenye kitovu cha mtoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 11805

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Madhara ya tumbaku na sigara

Post hii itakwenda kuangalia madhara ya tumbaku na sigara anayoweza kuyapata mvutaji

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya watoto mapacha

Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.

Soma Zaidi...
Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Soma Zaidi...
Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi

Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.

Soma Zaidi...
Sababu za ugumba kwa wanawake

Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni saba

Soma Zaidi...
UTI na ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI kwa wajawazito

Soma Zaidi...
Mabaka yanayowasha chini ya matiti.

Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n

Soma Zaidi...
DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI

Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.

Soma Zaidi...
Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Soma Zaidi...