picha

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1.  Kitovu kutoa maji maji.

Kwa kawaida kitovu cha mtoto kikifungwa kwa siku ya kwanza kinaweza kuonyesha tu maji maji kwa siku ya kwanza na ya pili na baadae uendelea vizuri lakini mama au mlezi akiona maji maji kwenye siku ya kwanza ya pili na kuendelea na maji yanaendelea kutoka siku kwa siku ajue wazi kuna Maambukizi na anapaswa kumpeleka mtoto haraka hospitalini ili kuweza kupewa matibabu na kuepuka kuwepo kwa Tetunus kwa mtoto.

 

2.Pia mama kwa wakati huu ajiepusha na kutumia madawa ya miti shamba kwenye kitovu cha mtoto kwa sababu anaweza kuleta matatizo makubwa au mengine zaidi kwa sababu miti shamba utumia mda mrefu kuponyesha na pengine haiponyeshi kabisa na mda unaenda kwa hiyo mtoto anapoletwa hospitalini hali inakuwa mbaya zaidi.

 

3. Dalili nyingine ni kubwa kitovu cha mtoto kinavuja damu kupita kiasi.

Hii pia ni Dalili mojawapo ambapo kitovu kinakuwa kinatoa damu inawezekana ni siku chache baada ya kuzaliwa kwa mtoto au siku nyingi kidogo kwa hiyo damu utoka kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao ushambulia sehemu za mishipa ambayo iko kwenye kitovu na damu utoka, kw hiyo.Mama au mlezi wanapaswa kumpeleka mtoto hospitalini kwa matibabu zaidi na epuka matibabu ya kienyeji kwa wakati huu.

 

4. Kuwepo kwa harufu mbaya kwenye sehemu ya kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine kunakuwepo na harufu mbaya kwenye kitovu cha mama pakiandamana na usaha ambao unatoa harufu mbaya, kwa sababu ya kuwepo usaha sio vizuri kubinya usaha ili uweze kutoka kwa sababu huwezi kujua kuwa usaha unatokea sehemu gani kwa sababu kuwepo kwa usaha lazima kuwa kuna kitu kimeoza.

 

5. Ngozi inayozunguka kitovu huwa nyekundu.

Kwa kawaida kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu utakuta ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa nyekundu na pia ukijaribu kugusa utaona mtoto anaumia na kulia kwa hiyo moja kwa moja mzazi au mlezi wa mtoto anapaswa kujua kubwa kuna Maambukizi kwenye kitovu na pia mama hapaswi kufanya chochote kwenye ngozi ya kitovu cha mtoto tofauti na kwenda hospitalini.

 

6. Kuwepo kwa vipele kwenye ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa na vipengele, vipengele hivyo kwa wakati mwingine vinakuwa na usaha au pengine vinakuwa havina au kwa wakati mwingine vinakuwa na maumivu kwa sababu ukimgusa mtoto anaanza kulia hivi vipele kwa wakati mwingine vinaandamana na homa.

 

7. Kwa wakati mwingine mtoto analia sana na kushindwa kunyonya na pengine anasinzia sana kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu. Kwa hiyo akina mama na walezi wa watoto wanapaswa kujua kubwa hawapaswi kuweka chochote ili kutibu maambukizi au kupasua chochote kwenye kitovu cha mtoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 12637

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa

Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mar

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo yanayowapata watoto waliozaliwa kabla ya wakati au mapema (premature)

Kuzaa kabla ya wakati ni kuzaliwa ambayo hufanyika zaidi ya wiki tatu kabla ya kuzaliwa kwa mtoto au kuzaliwa mapema ni moja ambayo hutokea kabla ya mwanzo wa wiki ya 37 ya ujauzito. Kawaida, ujauzito hudumu kama wiki 40.

Soma Zaidi...
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?

Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.

Soma Zaidi...
tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba

Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?

Soma Zaidi...
Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango

Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali.

Soma Zaidi...