Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

1.  Kitovu kutoa maji maji.

Kwa kawaida kitovu cha mtoto kikifungwa kwa siku ya kwanza kinaweza kuonyesha tu maji maji kwa siku ya kwanza na ya pili na baadae uendelea vizuri lakini mama au mlezi akiona maji maji kwenye siku ya kwanza ya pili na kuendelea na maji yanaendelea kutoka siku kwa siku ajue wazi kuna Maambukizi na anapaswa kumpeleka mtoto haraka hospitalini ili kuweza kupewa matibabu na kuepuka kuwepo kwa Tetunus kwa mtoto.

 

2.Pia mama kwa wakati huu ajiepusha na kutumia madawa ya miti shamba kwenye kitovu cha mtoto kwa sababu anaweza kuleta matatizo makubwa au mengine zaidi kwa sababu miti shamba utumia mda mrefu kuponyesha na pengine haiponyeshi kabisa na mda unaenda kwa hiyo mtoto anapoletwa hospitalini hali inakuwa mbaya zaidi.

 

3. Dalili nyingine ni kubwa kitovu cha mtoto kinavuja damu kupita kiasi.

Hii pia ni Dalili mojawapo ambapo kitovu kinakuwa kinatoa damu inawezekana ni siku chache baada ya kuzaliwa kwa mtoto au siku nyingi kidogo kwa hiyo damu utoka kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria ambao ushambulia sehemu za mishipa ambayo iko kwenye kitovu na damu utoka, kw hiyo.Mama au mlezi wanapaswa kumpeleka mtoto hospitalini kwa matibabu zaidi na epuka matibabu ya kienyeji kwa wakati huu.

 

4. Kuwepo kwa harufu mbaya kwenye sehemu ya kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine kunakuwepo na harufu mbaya kwenye kitovu cha mama pakiandamana na usaha ambao unatoa harufu mbaya, kwa sababu ya kuwepo usaha sio vizuri kubinya usaha ili uweze kutoka kwa sababu huwezi kujua kuwa usaha unatokea sehemu gani kwa sababu kuwepo kwa usaha lazima kuwa kuna kitu kimeoza.

 

5. Ngozi inayozunguka kitovu huwa nyekundu.

Kwa kawaida kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu utakuta ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa nyekundu na pia ukijaribu kugusa utaona mtoto anaumia na kulia kwa hiyo moja kwa moja mzazi au mlezi wa mtoto anapaswa kujua kubwa kuna Maambukizi kwenye kitovu na pia mama hapaswi kufanya chochote kwenye ngozi ya kitovu cha mtoto tofauti na kwenda hospitalini.

 

6. Kuwepo kwa vipele kwenye ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto.

Kwa wakati mwingine ngozi inayozunguka kitovu cha mtoto inakuwa na vipengele, vipengele hivyo kwa wakati mwingine vinakuwa na usaha au pengine vinakuwa havina au kwa wakati mwingine vinakuwa na maumivu kwa sababu ukimgusa mtoto anaanza kulia hivi vipele kwa wakati mwingine vinaandamana na homa.

 

7. Kwa wakati mwingine mtoto analia sana na kushindwa kunyonya na pengine anasinzia sana kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye kitovu. Kwa hiyo akina mama na walezi wa watoto wanapaswa kujua kubwa hawapaswi kuweka chochote ili kutibu maambukizi au kupasua chochote kwenye kitovu cha mtoto.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 10472

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo chini ya umri wa miaka mitano ili kuweza kuweka afya yake kwenye njia safi.

Soma Zaidi...
Sababu za kutangulia kwa kitovu wakati Mtoto anazaliwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kutangulia kwa kitovu wakati wa mtoto anapozaliwa.

Soma Zaidi...
Changamoto kubwa za tendo la ndoa kwa wanaume

Posti hii inahusu zaidi changamoto ya tendo la ndoa kwa wanaume,wanaume wamekuwa wakipata changamoto ya tendo la ndoa na kuwafanya kushindwa kujiamini na kukosa kabisa raha kwenye maisha yao

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza uke

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya ngozi wakati wa ujauzito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye ngozi wakati wa ujauzito, ni mabadiliko yanayotokea kwenye ngozi ya Mama wakati wa ujauzito.

Soma Zaidi...
Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.

Soma Zaidi...
mambo ambayo utaulizwa mama mjamzito ukifika kituo cha afya unatakiwa utoe majibu sahihi.

Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Madhara ya mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtoto alizaliwa na uzito mkubwa.

Soma Zaidi...