picha

Vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba

Posti hii inahusu zaidi vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba,ni vipimo vya moja kwa moja kutoka maabara na vingine sio vya maabara.

Vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba.

1.Wachumba na akina Mama kabla ya kubeba mimba wanapaswa kupima vipimo ili kuweza kuangalia kama kuna Magonjwa yoyote ambapo akibeba mimba atapata shida kwake na kwa mtoto.

 

2.Kwanza kabisa Mama anapaswa kupima kama ana Magonjwa yoyote ya zinaa kama vile kaswende kisonono na Magonjwa mengine kama hayo kwa sababu Mama akibeba mimba akiwa nayo mimba inaweza kutoka au Mama anaweza kupata mtoto mfu kwa hiyo ni lazima kupima magy hayo kabla ya kubeba mimba.

 

3.Pia mama na wachumba wanapaswa kupima temperature, msukumo wa damu, mapigo ya moyo, na upumuaji, Magonjwa ya moyo, sukari kwa kufanya hivyo ni maandalizi mazuri ikitokea kuna ugonjwa wowote unatibika mara moja na Mama akija kubeba mimba anakuwa salama na mtoto atakuwa salama kabisa.

 

4.Pia Mama anapaswa kupima kundi la damu yake na kulijua wazi na pia kupima kiwango cha damu na pia kupima kama kuna mambukizi ya virus vya ukimwi kwa kufanya hivyo ataweza ikiwa mama siku ya kujifungua akiishiwa damu ni rahisi kujua damu yake au akikutwa na Maambukizi ni njia nzuri ya kumkinga mtoto kwa hiyo ni vizuri kabisa kupima Mama kabla ya kubeba mimba.

 

5.Kwa hiyo tumeona wazi faida za kupima kabla ya kubeba mimba kwa akina mama na wachumba kwa sababu tunaepuka madhara mbalimbali kwa watoto na kuwakinga na Magonjwa kabla hawajazaliwa ili wazaliwa kabisa kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa mtoto ukimweka kwenye mazingira mazuri ya kuzaliwa atazaliwa salama.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2118

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Njia za kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.

Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Soma Zaidi...
Siku za kupata ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata ujauzito

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.

Soma Zaidi...
Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Soma Zaidi...